Msaada: Dawa ya Genital warts

Jessyjide

Member
Joined
Jul 19, 2016
Posts
39
Reaction score
15
Nina ndugu yangu anasumbuliwa mwaka sasa, Hosp kibao kaenda vinapungua tu, Ila haviishi kabisa, kuna wakati vinarudi vingi.
 
uwiiiii!!!
Masikin mpe pole sana
Hizo genital warts huwa hazina dawa ila huwa zinakatwa au kuchomwa kitaalam......Na pia inasemekana kua vinaweza kukatwa au kuchomwa ila vikarudi tena mpaka vitakapoamua kuondoma vyenyewe

Mimi nilishapata hilo tatizo dr msuya (Arusha-st thomas) alinisaidia kwa hilo
Ila baada ya kufanyiwa hivyo vilirud tena mara moja,dr alichoniambia nibadilishe mfumo wangu wa maisha akimaanisha nile vyakula vya afya.... mfano mboga za majani kwa wingi brocoli,couliflower,na vingine vyote vya afya na kufanya sana mazoezi kwa sana

Aliniambia hivyo kwa sababu nilitakiwa niimarishe immunity system yangu ili niweze kupambana na hilo tatizo na matatizo mengine pia
Kwa hiyo jaribu kutumia huo ushauri na wewe.
 
Daaaaah hilo Janga kuna mtu namfahamu aliteseka sana mixer kutoa harufu mbaya huko chini lakini akaja kuponea kwenye tiba asilia
 
vinasababishwa na nini hsswa???
 
wekeni picha tuone au kwa kiswahili linaitwaje hilo tatzo!
 
vinasababishwa na nini hsswa???

Mara nyingi vinasababishwa na wadudu wanaoitwa human papilloma virus (HPV). Wadudu hawa uambukizwa kwa kugusana ngozi kwa ngozi au kwa kujamiana (ngono).

Kama alivyosema mchangiaji moja, warts hazina tiba isipokuwa zinaweza kutoweka zenyewe baada ya muda (yawezekana miaka 2 kwa wadada), au kuunguzwa kwa kemikali au kukatwa. Unashauriwa kumwona daktari mahili wa ugonjwa huu kwasababu baadhi ya aina ya wadudu wa HPV wanabadirisha mfumo wa cell na kusababisha cancer hasa kwa wadada! Hivyo mgonjwa atatakiwa akafanyiwe Pap test ili kuangalia aina ya wadudu aliopata!
 
Ushauri hapo msiamini sana yale mataulo mnayokuta lodges na kujifutia sehemu za siri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…