Msaada...Dawa ya visiki shambani?

Sekibuju

JF-Expert Member
Joined
Jul 23, 2012
Posts
315
Reaction score
132
Tafadhali waungwana... Naomba msaada kwa yeyote anayefahamu dawa ya visiki shambani...
 
iv unakil timamu wewe? dawa ya visiki ni kung'o fulstop

Ni kweli najua kuving'oa pia ni dawa, lkn nilishasikia tetesi kwamba kuna dawa ya kupaka kweny visiki na vinaisha vyenyewe. Kwny shamba kubwa na jipya visiki ni vingi sana na kuving'oa ni gharama kubwa.
 
Ni kweli najua kuving'oa pia ni dawa, lkn nilishasikia tetesi kwamba kuna dawa ya kupaka kweny visiki na vinaisha vyenyewe. Kwny shamba kubwa na jipya visiki ni vingi sana na kuving'oa ni gharama kubwa.

Huoni kuwa hiyo ni dawa yenye kemikali kali sana inaweza kukusababishia madhara baadaye?
 
Inaonyesha niko nyuma sana ya wakati...., duh
 
... Dawa isiyo kuwa na madhara yoyote ni kutumia jembe, shoka, panga, fyekeo n.k
Kila siku za weekend jaribu kutumia vifaa hivyo hapo shambani kwako' natumaini baada ya mwaka moja tatizo litaisha.
Gharama itakuwa ndogo sana ukitumia na ukishiriki wewe mwenye kuviondoa hivyo visiki.
 
Samahani nawatoa nje kidogo na mimi naomba kama kuna mtu anajua dawa au namna ya kumaliza konokono wale wenye shell za brown na michirizi mweupe kwenye bustani za mboga na maua! Wananitesa sana
 
Ni kweli najua kuving'oa pia ni dawa, lkn nilishasikia tetesi kwamba kuna dawa ya kupaka kweny visiki na vinaisha vyenyewe. Kwny shamba kubwa na jipya visiki ni vingi sana na kuving'oa ni gharama kubwa.

hakuna dawa ya ivo, kata miziz kadhaa wakati wa kiangazi alaf rundika kuni apm na nyasi 'choma mota ndim njia bora na yenye manufaa kwa shamba
 
hakuna dawa ya ivo, kata miziz kadhaa wakati wa kiangazi alaf rundika kuni apm na nyasi 'choma mota ndim njia bora na yenye manufaa kwa shamba

Nashukuru sana mkuu.
 
Tafadhali waungwana... Naomba msaada kwa yeyote anayefahamu dawa ya visiki shambani...
Unaweza kuanzia hapa (nimeinyofoa mahala fulani):
 
Mkuu SMU nashukuru kwa mchango wako lkn mbona nahisi inaweza nipa kazi kubwa na kukawa na uwezekano wa kutofanikiwa...
 
Si kuving'oa? Au sijaelewa ni visiki gani? Vile vinavyoleta shida sana unavichomea moto hapo hapo....
 
Mimi nina shamba jipya huu ni mwaka wa pili nalilima, lina visiki sana. Nimewauliza wenyeji wangu dawa ni nini na wakaniambia dawa ni kucharanga hayo majani kwenye hivyo visiki kila wakati yakuapo. Wanasema kadri ukatavyo charanga hayo machipuka, mizizi inafanya kazi ya ziada kuleta chakula cha kuchipua hayo majani hadi inachoka na hatimaye kufa/kuoza na kufanya hicho kisiki kung'oka/kung'olewa kwa urahisi. Nafanya hivyo kila mara niendapo shamba na naanza kuona ukweli wake. Wanasema ukiendelea hivyo in two years shamba linakuwa safi na unaweza hata ingiza trekta! Utashangaa. JARIBU HIYO NA WEWE!
 
Mzee mwqenzangu mie nimeishia kucheka tu baada ya kujua aina ya shamba na visiki vilivyomo shamabni humo, Paloma huwa wewe visiki unavimalizaje? Duh hii kali bhana
Inaonyesha niko nyuma sana ya wakati...., duh
 
Last edited by a moderator:

Ahsante mkuu.
 
mkuu sijakuelewa. kwani shamba kubwa si pia linahitaji capital kubwa?ushauri wangu ni upange mkakati, kila msimu unang'oa visiki kwenye ukubwa fulani wa shamba, slowly, litakuwa safi. hongera sana, kuwa na shamba ni kuona mbali kuliko kuwa na king'amuzi.
 
Ni kweli najua kuving'oa pia ni dawa, lkn nilishasikia tetesi kwamba kuna dawa ya kupaka kweny visiki na vinaisha vyenyewe.

ukiipata ujipake na wewe ili uishe usisumbuke tena na visiki shambani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…