Msaada - HGE Galanos High School

Mnyankole

Member
Joined
Aug 18, 2010
Posts
23
Reaction score
5
Wakuu naomba msaada wenu. Mdogo wangu kachaguliwa kwenda Form V (HGE) huko Galanos high school, Tanga.
Kuna yeyote anayejua kama shule hii ina mazingira mazuri ya kusoma hiyo combination ya HGE? Namaanisha kama kuna walimu wazuri na mazingira mengine ya kielimu yanayoweza kumfanya mwanafunzi afanye vizuri kimasomo.
Pia naomba kujua shule hii iko maeneo gani, ni hapo Tanga mjini au wilayani? Naomba msaada wenu.
 
Shule ni nzuri kimazingira na ufundishaji pia.Ila sina uhakika na History.Jamaa yangu anasoma EGM pale anaifurahia mno kwa kuwa na mafunzo mazuri.
 
Shule iko poa sana iko Tanga jijini maeneo ya Nguvu mali!! Advance huwa hatutegemei walimu sana ni kukomaa tu bt shule iko safi sana mi nimesoma pale miaka ya nyuma kidogo.
 
Nimesoma pale .. Nilitoka na one kali sana.
Yani huyo mdogo wako usije ukamhamisha hata kama akilia kuwa shule ngumu wanalima wewe ziba masikio mwambie aPige kitabu .. Historia ya galanos ipo hivi.. Ukifika pale especially HGe una div II tayari.. Ukiingia darasani basi wewe una div I.
Utayakumbuka maneno yangu shule nzuri sana hata kama hakuna waalim shule Ote za gvt hazinaga waalim atakaowakuta ni hao hao . Kumbuka mwanafunzi anafaulu kwa juhudi zake mwenyewe na wala sio za mwalim. Ingekuwa waalim wanafaulisha basi mwanaisha kikwete asingapata zero pale feza.
I hope nimekusaidia kidogo
 
Ni miongoni mwa shule nzuri sana kwa hiyo comb kwa hapa Bongo,akifika mizani ya Tanga aombe ashushwe kituo kiitwacho Majani mapana,akishuka hapo kama hana mizigo mingi anaweza kutembea kwa miguu au bodaboda ni 1000/= tu, kwa mantiki hiyo shule ipo mjini,nakumbuka enzi hizo tukiita Galax tulikuwa tukitembea kutoka shuleni hapo hadi Usagara sekondari(hosteli zao) kubadilishana hili na lile na ndugu zetu wa pale.ambapo usagara hosteli ni kama mita 160 toka stendi kuu ya TANGA JIJI.HIVYO NI rahisi kukutana na wanafunzi wa USAGARA,TANGA TECH(Shule kongwe YA SERIKALI kuliko zote TANGANYIKA) hvyo kama atatumia fursa nzuri na konection na hzo shule kufaulu BAM nadhani itakuwa rahisi sana kwake shule hizo ni PCM zaidi.Walimu wengi pale ni wazuri sana coz mazingira ya kazi ni pendwa sana.
 
Galanos School Penda Watoto..twakupenda, twakusifuuu. Huo ndio wimbo wa shule. Tulikuwa ni lazima tuimbe kila jumatatu wakati wa kupandisha bendera. Enzi za Kinala hizo. Galanos ilikuwa Bonge ya shule. Sijui kwa sasa.
 
Galanos ni bonge la shule mimi mwenyewe niliomba nichaguliwe huko lakn hawakunichagua.
mpeleke dogo akasugue
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…