... Miaka kadhaa nyuma nilukutana na changamoto kama hii : Nilikutana na mlimbwende mmoja kwenye harusi ya jamaa yangu na nikamzimikia kweli. Kila nikimsomesha wapiii, na baada ya miezi kadhaa nika give up,maisha yakasonga. Baadae nikapata mdada mwingine tunaendelea naye for some time, maybe a year, tukaachana.One day nikakutana na yule mlimbwende na surprisingly this time kum test kidogo tuu anakubali, na tukapanga kesho tufanye yalee mambo yetu. Kesho yake tukakutana, kikaanza kinywaji then tukaingia room, sasa wakati ndo tunaanza kupasha kabla ya mechi simu ikaanza kuita nikawa nachuna, yule mlimbwende anahisi nipokee kwanza labda ni muhimu, nikapokea, kumbe ni yule demu wangu tuliyeachana naye, nikataka kukata simu but akaniwahi kwamba.. '' wewe huyo uliyenaye hapo ni muathirika, na kama unafikiri ni uongo mpigie rafiki yako fulani muulize '' akakata simu!! Aisee nilipaniki hatari, mlimbwende akaniuliza vipi tena?? Nikamdanfanya kumetokea ajali na mdogo wangu yuko mahututi, mchezo ukaishia pale na akaondoka zake. Nitampigia jamaa yangu kupata uhakika, akasema ni kweli huyo ni muathirika, aisee huo mwezi ulikuwa mchungu sana kwangu... Baada ya hapo nikawa kila miezi sita napima but was found OK. Baadae, after a year or so yule mlimbwende akafariki kwa hilo tatizo.