Msaada huu mmea unaitwaje?

Castor Bean/Oil Plant (Ricinus Communis).

Kwa kiswahili sijui ndio wanaita mnyonyo.

Mbegu zake zinatumika kutengeneza Castor Oil mafuta (laxative) yenye matumizi mbali mbali.

Pia mbegu zake zinaweza kuwa processed chemically kutengeneza "Ricin". Hii ni sumu ambayo inaua taratibu na ni nontraceable. Yani ukipewa hii sumu haufi hapo hapo na hata ukifa baada ya siku kadhaa hata ukifanyiwa autopsy ni ngumu ku establish kama sumu ndio chanzo cha kifo.
 
so sio dawa ni sumu
Sent using Jamii Forums mobile app
 
unatibu nini msaada

Sent using Jamii Forums mobile app
Huo nimewahi kuona zamani watu wakiogeshea watoto na maji ya moto kwa kusema inatibu degedege na pia kuna wengine hutengeneza mafuta ila hapo juu kuna mtu chaliifrancisco kafafanua vizuri inatengenezewa castor oil haya yanatumika kwa mambo mengi sana kukanda sehemu mbali mbali za miwili ikiwa ni kilainishi cha viungo.
 

Dah, nilijua utahitimisha kwamba inaongeza nguvu za kiume!

Noma sana.
 
Castor oil plant, mbegu au mafuta ya mbegu ni mazuri kwa kulainisha choo,

NB. yapo yanauzwa famasi 100mls, usije ukala mbegu ukazidisha kiwango utaharisha hadi utumbo, utaishi chooni kabisa
 
Kwa kuongezea katika uchakataji aliofanya chaliifrancisco Mnyonyo ni dawa na njia bora ya asili ya kupanga uzazi.

Mwanamke atatumia mbegu yake kwa kumeza masaa saba kabla ya "Tendo la ndoa" endapo yupo katika hatari na siku zake. 🙈
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…