Msaada: Huyu ni nyoka wa aina gani?

Huyo ni koboko ila ni Bado mtoto sasa hapo baba na mama yake itakuwa wanamtafuta mtoto jipange mkuu
Na je ukimkanyaga bahati mbaya ataelewa ni bahati mbaya na hatakua na shida na wewe ?
 
Upo maeneo ya wapi tujue eneo hilo Kuna nyoka wa aina gani wenye rangi hiyo.
Nilipo Mimi Kuna nyoka rangi Kama huyo anafanana Sana na black namba lakini si yeye.
Mfunue mdomo ukiona ana rangi nyeusi mdomoni kwa ndani ujue huyo ni black namba (koboko).

Note: Kuna nyoka wengi Wana rangi hiyo. Usingemponda ponda tungeona vizuri shingo yake na kichwa tungemtambua.
 
ndio mdomoni alikua mweusi mkuu na mara mbili alikua anajikunja na kuruka kama anajifyatua hivi je kwa tabia hiyo je pia inaweza kutufahamisha jamii yake
 
Mmeita mpaka zimamoto kumuua brown house snake! Angekua green mamba je ambaye akiingia bustanini haumuoni au black mamba mwenye Kasi
Mnaua tu ndio maana nature inawapiga na mavita,maradhi,matetemeko nk
 
mkuu kama watakua ni black mamba je natakiwa kukabiliana nao kwa mtindo upi ili kuwa katikanafasi ya kuwashinda.
 
Asante mkuu, kwa bahati mbaya kichwa chake nilikiponda kabisa wakati nakabiliana nae. Ila hapa ni Morogoro
Kama ni Morogoro basi atakuwa ni BROWN HOUSE SNAKE ambao wanapenda sana kukaa kwenye makazi ya watu wakila panya, mijusi. Ni nyoka wasio na sumu na ni completely harmless to humans. wanapatikana kwa wingi sana Morogoro mjini.
Nadhani nimekusaidia mkuu
 
Mkuu choma mpira kwenye eneo lako watahamq wote,Ila huyo sio Koboko.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…