Msaada: Huyu ni tapeli au sio wakuu?

We jamaa ubongo wako unachelewa sana ku-load.

Aya mtumie basi hizo taarifa zote anazozitaka. Assume kama hakuna mtu uliyemshirikisha au kumuomba msaada wa mawazo katika hili humu JF.

Sent using Jamii Forums mobile app
Nahisi jamaa alishatuma hizo taarifa sasa ana wasiwasi kama ataweza kupigwa. Anavyoelezea na kung'ang'ania inaonyesha alishatuma na hapa amekuja kuuliza kiana kama kuna madhara.
 
πŸ˜…πŸ˜…πŸ˜…, nami ilinitokea nikiwa mwaka wa 2 kama hii ya kwako aisee, nikapiga hesabu nikaona hii pesa ndefu sana siwezi ihifadhi kwenye a/c yangu, acha nimshirikishe mzee wangu...Lakini kabla ya kumshirikisha nikamshtua rafiki yangu mmoja hv akanambia naye alitumiwa, hivyo ni matapeli...
 
Nahisi jamaa alishatuma hizo taarifa sasa ana wasiwasi kama ataweza kupigwa. Anavyoelezea na kung'ang'ania inaonyesha alishatuma na hapa amekuja kuuliza kiana kama kuna madhara.
Hivi mtu akimwambia usiende sehem flani hapafai na wewe ukamuuliza hapafai kwasababu gani unakuwa umekosea

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kabla huja tuma fanya uchunguzi wa kumtosha maana now days kuna kitu kinaitwa IDENTIFY THEFT ...be careful ndugu yetu..watakuibia identify yako na waitumie kufanya uharifu(inturn itaonekana umefanya wewe)

Sent using Jamii Forums mobile app
 
No easy investment like that....

Jr[emoji769]
 
Hivi mtu akimwambia usiende sehem flani hapafai na wewe ukamuuliza hapafai kwasababu gani unakuwa umekosea

Sent using Jamii Forums mobile app
Umekuwa unaonyesha kutoamini kama hao watu ni matapeli. Umeambiwa ni matapeli halafu wewe bado unang'ang'ania kuwa hata ukipeleka contacts zako hakuna madhara! Hata kama hakuna madhara kwa nini upoteze muda na matapeli..
 
taarifa za mtu ni kitu sensitive kuliko maelezo, ndio maana sio kila mahali unaweza kuandika no zako za simu,
usitoe taarifa zako hovyo, maana unaweza kuibiwa utambulisho halafu mtu akatumia kufanya uhalifu kama jamaa mmoja alivyoeleza hapo juu, na pia kwa jinsi techinolojia inavyoendelea kwa kasi huwezi jua kuwa hawa matapeli watafanyia nini hizi taarifa mbali na mambo ambayo tayari unayajua
 
Kwa kifupi achana na watu/dili za kwenye mitandao utakuja kulia kilo cha mbwa Koko πŸ•πŸ•
 
Sasa mtu anapigwa kwa kutoa business plan, namba ya simu, na identity card number? Nimeuliza watu wengi wamesema hizo info hapo juu hazina madhara

Sent using Jamii Forums mobile app

Hivi kweli mkuu unaamini passport number haina madhara? Yaani hapo unampa mtu ID yako ambayo anaweza kuitumia kufanya uhalifu... kwemye ulimwemgu huu wa technology kamwe usitoe passport details zako eti kisa tu hupigwi hela ipo siku utashangaa INTERPOL wako mlangoni kwako
 
Mwambie akutumie wewe funds za kufunguwa kampuni Tanzania.
 
Wacha ukaidi na ushamba, watu wote washakwambia huyo ni tapeli inaonesha huwaamini bado. Ukimpigia skype au video call utapata kumuona na utaweza kujuwa ni choka mbaya. Account ukimpa anaweza kuibia pesa watu akazitia humo kwanza halafu akazitowa wewe bila ya kujuwa. Matokeo yake utatafutwa wewe! Kitu gani hufahamu hapo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…