Msaada jinsi ya kuandika maandishi mahali na kuyahifadhi ili baadae kuyachapisha au kuyahamishia mahali pengine

Msaada jinsi ya kuandika maandishi mahali na kuyahifadhi ili baadae kuyachapisha au kuyahamishia mahali pengine

Ukishayaandika shikilia kidogo utaona option ya copy, copy ukayahifadhi hata kwenye sms muda wowote utayapata.
 
katika kuandika hio story nilianza mwaka 2000 nikasimulia kisha 2001 hivo hivo mpaka 2013 ndio nasema masimulizi yakifikia 2025 naileta
Duh! mkuu uko sirias na hii kazi. Bila shaka nitahitaji kujifunza mengi kutoka kwako.
 
hapa nimeandika kupitia Notes ya simu yangu Kama nilivyoelekezwa na Mkuu Mwachiluwi, nafainyaje hii ili kuipost
Mwachiluwi Nomadix
Screenshot_20250211_223817_Samsung Notes.jpg
 
hapa nimeandika kupitia Notes ya simu yangu Kama nilivyoelekezwa na Mkuu Mwachiluwi, nafainyaje hii ili kuipost
Mwachiluwi Nomadix
View attachment 3233783
Shikilia hayo maandishi yatatokea maneno select all yabonyeze

kisha yatatokea maneno copy yabonyeze

kisha uende unapotaka kuyapost mfano humu JF shikilia sehemu unapotaka kupost yatatokea maneno paste
 
Shikilia hayo maandishi yatatokea maneno select all yabonyeze

kisha yatatokea maneno copy yabonyeze

kisha uende unapotaka kuyapost mfano humu JF shikilia sehemu unapotaka kupost yatatokea maneno paste
OK ngoja niende huko
 
Simulizi: Sekunde 921
Mtunzi: kijana masikini
Sehemu ya kwanza.

Kabla sijamjibu chochote Alex niliingia ndani na kuanza kutafuta picha ya sadati huku jasho jingi likinitoka, japo akili yangu ilikuwa ikiniambia kabisa kwamba pichi niliweka ndani ya kabati lakini mboni za macho yangu zilishindwa kabisa kuiona.

"Dah nafanyaje sasa"
Niliongea huku nikiitazama saa yangu ya mkononi.

"Kim.. Kim.. Kim ujue unachojaribu kukifanya ni kitu hatari sio kwako tu bali kwa familia kwa ujumla hususani dada yako"

Aliongea Alex huku akitanguliza kiniita mara tatu kwa jina langu la Kim ambalo ni ufupisho wa KIjana Masikini

Nilimgeukia Alex na kumtazama, alikuwa amesimama mlangoni akionekana kutokuridhia kabisa juu ya jambo nililodhamiria kulifanya.

"Alex, jasiri hufa mara moja tu ila muoga hufa mara nyin....

yeees nimeweza asante sana wote mliojitokeza kunisaidia.
sheremaya Edo kissy
 
Kabla sijamjibu chochote Alex niliingia ndani na kuanza kutafuta picha ya sadati huku jasho jingi likinitoka, japo akili yangu ilikuwa ikiniambia kabisa kwamba pichi niliweka ndani ya kabati lakini mboni za macho yangu zilishindwa kabisa kuiona.

"Dah nafanyaje sasa"
Niliongea huku nikiitazama saa yangu ya mkononi.

"Kim.. Kim.. Kim ujue unachojaribu kukifanya ni kitu hatari sio kwako tu bali kwa familia kwa ujumla hususani dada yako"

Aliongea Alex huku akitanguliza kiniita mara tatu kwa jina langu la Kim ambalo ni ufupisho wa KIjana Masikini

Nilimgeukia Alex na kumtazama, alikuwa amesimama mlangoni akionekana kutokuridhia kabisa juu ya jambo nililodhamiria kulifanya.

"Alex, jasiri hufa mara moja tu ila muoga hufa mara nyin....
swadakta umeweza hongera mkuu
 
Back
Top Bottom