Msaada jinsi ya kuongeza "confidence"

Mhafidhina07

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2014
Posts
3,340
Reaction score
4,659
Habari zenu wanajamvi,

Leo ningependa kufundishwa njia zitakazo niwezesha kuwa mtu wa kujiamini niwapo mbele ya watu. Nasikitika sana juu ya tatizo hili ambalo toka utotoni mwangu hii nimegundua jinsi malezi yangu yalikuwa ndiyo chanzo cha kupungua kujiamini kwani nilikuwa napigwa sana hivo kuuliza kitu ama kuongea ilikuwa ngumu kwangu hivo mpaka sasa nimekuwa muhanga mkubwa.

Naomba kujuzwa mbinu zitakazonifanya niwe bora zaidi katika kujiamini,
Kwani now najiandaa kwenda chuo nikiwa na tatizo hili ndani ya kichwa changu.
 

Pole mkuu, hili mbona ni tatizo la wengi sana. Sio kila mtu anaweza kusimama mbele za watu akaweza kujieleza. Cha muhimu ni kuamua na kuanza kuzoe kuongea mbele za watu unaanza na hata wachache. Kila kitu ni mazoea
 
Pole sana mkuu.

Mpaka hapo natumai tayari umeshaanza kufanikiwa katika safari yako ya kutatua tatizo lako kwasababu tayari umeshajua ni kipi kiini cha tatizo.

Mimi ninacho kushauri aanza kujiamini kuazia sasa, na pia jiupushe sana na kujilinganisha na watu wengine kwasababu moja ya sababu ambazo zinasababisha watu wapoteze confidence ni kujilinganisha na watu wengine.

Kitu kingine amini kwamba uwezo wako katika kujua vitu flani unaweza kuwa mkubwa kuliko vile wewe mwenyewe unahisi, kwa mfano unaweza kuwa unajua kitu darasani lakini kwakuwa unadhani kuna watu wanaweza wakawa wanajua zaidi yako ukakaa kimya kumbe katika uhalisia wewe ndiyo unajua zaidi ya wengine.

(Unaweza ku Google kitu kinaitwa imposter's syndrome utanielewa ninacho maanisha)
 
Heshima kwenu wakuu!

Mimi ni mwanafunzi niliemaliza kidato cha sita mwaka huu nataraji kujiunga chuo mwezi wa kumi na moja. Tatizo langu kubwa siwezi kuongea mbele za watu napata shida sana pindi niongeapo katika umati wa watu au hata watu wachache mfano watu wa tano huwa natetemeka sana mpaka kupoteza point zangu muhimu hivYo naombeni msaada because muda huu nataka kwenda chuo kwenye presentation shida.
 
Usiwe unaangalia watu usoni pindi unapoongea hii nayo itakusaidia kidogo
zingine ngoja waje masaikolojisti.
 
gud mkuu
 
Kufanyia birthday watoto tngu wakiwa udogon inawajengea confidence sna
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…