Msaada jinsi ya kuongeza "confidence"

Ni confidence, siyo ulivyoandika wewe.

Soma kitabu cha Dale Carnegie "How to win friends and influential people" kitakusaidia sana kupita maelezo. Kitabu hicho ni my all time favorite kati ya vitabu vya "how to...".

hivyo ukaamua kufanya kinyume chake au hukuelewa???jinsi ulivyo hapa jf utadhani umesoma kitabu How to make enemies and irritate people
 
fanya haya uwapo mbele za watu ukiwa unazungumza.
1.Amini unachozungumza wewe hakuna anyejua zaidi kuliko wewe hata kama ni maprofs kama wakina kitila na wanasheria kama Lissu.
2.Ongea kwa hatua na kufanya unachozungumza watu wakisikie kwa makini acha kutetemeka.
3.uwapo mbele za watu mfano lecture room pendelea kuangalia at the back and not at the people's heads
4.Jiamini kuwa unachosema ni cha ukweli sambamba na kuwa na ukweli wa jambo husika mfano ukifahamu ya kuwa 1+1=2 hakuna atakaye kukosoa hata kama ni prof na kwa kuwa huo ndio ukweli basi utalisema hilo ukiwa na IMANI ya dhati na tabasamu zito.
5.Usipanic uwapo machoni pa wengi mara tu baada ya kukosea unachozungumza.
6.PENDEZA KAMA KIJANA MSOMI ILI WAO WANAOKUSIKILIZA WAKUOGOPE ILI UWATETEMESHE.
ukivaa hovyo utatetemeka na kuloose confidence.Ni hayo tu kama yapo mengine subiri mafundi waje.
#NikoTayariKwaUKUTA sep 1.
 
Jamaa tatizo lake anasema hata kwa watu watano ila humu wengi mnazungumzia kujiamini kwenye umati wa watu wengi.

Mie naona bado hajafunguka vizuri kuelezea tatizo lake. Maana nishawahi kukutana na mtu ana tatizo la kuonea aibu hadi wanaume wenzake.
 
Wadau wameongea mengi mazuri. Binafsi, hilo tatizo nilikuwa nalo, lakini sasa limepungua kwa 95%. Nilipewa tips zote, hazikunisaidia. Nilichoamua ni kujitatmini mwenyewe. Mara ya kwanza, niliamua kutumia hasira. Yani, nikishakuwa nimezungukwa na watu wanaonitazama, lazima nijikumbushe makusudi kitu kinachoniudhi, maana fact ni kuwa aibu mara nyingi, kama si zote, itakupelekea ucheke au utabasamu, na ukicheka au kutabasamu, utaonekana tu kuwa una aibu. Sasa, hapo nikishakuwa na hasira, nakuwa serious, ila naepuka kuonesha uso wa hasira bhasi siwezi kucheka bila sababu. Hapo naweza kupresent part yangu na nikakaa mbele ya darasa hata lisaa zima bila kuonesha aibu. Baadaye, aibu ikapungua kwa kiasi kikubwa kwa njia hiyo, nikajikuta nazoea mikusanyiko.

Baadaye, nikaamua kuachana na hiyo, nikaanza kukaza macho kwa yeyote atayeniangalia hadi aone aibu yeye. Nikigundua unanitolea macho, mimi nakuangalia mwanzo mwisho, hata kama ni dakika 2, lazima utakwepesha mwenyewe, either kwa kuangalia chini au pembeni. Hapo nishakuwa na confidence, huwezi rudia tena. Nikiona mbishi kuona aibu, naweza hata nikaonesha ishara (facial expression) fulani, kama kunyanyua nyusi. Ukicheka, nimemaliza.

Kwenye presentation, huwa nafanya uhakika kazi nimeielewa vizuri. Assignment nilikuwa napenda kuandaa mimi (kugooglekutype nk), ili siku ya kuwasilisha niwe comfortable, nipate marks nzuri binafsi. Swali lolote litakaloulizwa na audience, nilijibu accordingly. Sometimes nilikuwa najiandaa kwa kusoma grammar kidogo nipunguze broken. Nilikuwa navaa vizuri hadi niamini nimependeza siku ya presentation. Hakikisha upo smart kila idara.

Kwenye group discussion nipo kuna changamoto. Hapo mpo jinsia tofauti, na kama ni mwaka wa kwanza hamjui wenzako. Kuna wajuaji, washushuaji, attackers, wapenda sifa, nk. Sasa hapo lazima uwe vizuri psychologically, kuwa normal, usiact toa point zako au hoja yako na itetee. Hapo aibu unaweza kuiondoa kwa kuzuga na simu tu, kujifanya unagoogle, unachat, au unasoma text, nk. (Sasa simu inasaidia). Ukiona mtu anakukodolea macho, hasa wa jinsia jirani, na wewe mwangalie mwanzo mwisho, akizid mkonyeze. Nilijikuta nakuwa confident hata kwenye course tunazoshea, kama development studies tupo kwenye hall kubwa takribani watu 200, naweza nyanyua mkono ili niulize au kujibu swali nikiwa back bencher. Marafiki zangu wakawa wananikataza eti "nawashazisha," wakawa wanaona aibu wao tena.
 
Duh! Jf inasaidia sana, hili tatz lang kbs yan ... ila m shida yang kubwa ni kweny salamu hasa kumsalimia KE gender aliyenizid umri kidogo. Huwa najing'ata mpk basi
 
angalia njia mbalimbali za kuweza kujiamini (confidence) hizi hapa:

kujizoeza kujiamini
Njia moja muhimu sana kisaikolojia ya kujenga hali ya kujiamini ni kupenda kusikiliza maneno ya kutia moyo na yenye ujasiri kutoka kwa watu maarufu. Kwa mfano, viongozi wenye msimamo, watetezi wa haki za binadamu, wanasiasa wanaotetea maslahi ya nchi bila hofu na kadhalika. Hotuba na maneno yao yakipata sehemu kubwa katika akili ya mtu, lazima yatajenga hali ya kujiamini kama wale anaowasikiliza.

kubali matokeo
Ifahamike kuwa ukiwaza kwa kina sana juu ya mahitaji yako, zao litakalofuata hapo ni akili kukuletea sababu za kushindwa kufanikisha mambo unayoyataka. Sababu hizo ukizipa nguvu sana ya kuziwaza zitakupa jibu la haiwezekani. Unapokuwa na mawazo yenye mlango huo wa kutokufanikiwa, uwezo wako wa kujiamini hushuka na kujikuta unashindwa katika mambo uyafanyayo. Katika maisha lazima mtu akawa na wakati wa kuachia mawazo yake na kukubaliana na matokeo yaliyopo hasa pale hali ya kushindwa inapokuwa kubwa.

Pata Msaada toka kwa watu wengine
jambo jingine la muhimu katika kuhitimisha uwezo wa mtu kujiamini ni kupata msaada wa mawazo kutoka wa watu wengine ambao ni makini katika maisha yao. Kama kuna jambo ambalo linakuwa gumu katika mawazo yako na limekosa ufumbuzi kiasi cha kukufanya usijiamini, washirikishe wengine wakusaidie na kukutia moyo wa kuendelea kukabiliana na hali yako ya kutojiamini.

Mwonekano sahihi
Namna mtu mwenyewe anavyouweka mwili wake linaweza kuwa ni tatizo la kumfanya ashindwe kujiamini. Kwa mfano,mtu kama si mlemavu lakini akajikuta anatembea miguu upande, mabega juu, kichwa chini au juu sana au kutembea akiwa anadundika kama mpira, ni vibaya kwa vile kitaalamu huchangia kumuondolea mtu ujasiri mbele za watu.
Ushauri wangu ni kwamba mtu anatakiwa kuupa mwili wake umuhimu na kuuweka kama alivyoumbwa, haifai kuwa mtu wa kuinama na kuficha uso, kusimama tenga pale unapoitwa au kuwa mbele za watu. Si vema pia kujipapasa mwilini au kutazama pembeni. Ni vizuri kila mtu kulinda mwonekano wake wa asili mbele za wenzake.

Kutembea haraka
Njia rahisi ambayo imethibitika kuweza kumuondolea mtu hali ya kutokujiamini ni kutembea kwa mwendo wa haraka. Haipendezi unapokuwa njiani kutembea kama mgonjwa, uliyechoka. Ukiwa hivyo ni rahisi sana kuwafanya watu wakukodolee macho ambayo yatakufanya wewe uhisi tofauti. Utembeaji wa haraka una faida nyingi, lakini kubwa kabisa ni kuwafanya watu wengine wakuone wewe ni mtu wa kazi usiyetaka kupoteza muda wako, mtu makini na mwenye mipango. Kitaalamu mwendo unaoruhusiwa ni wa asilimia 25, usizidi sana kiasi cha kuonekana kama unakimbia.

pingana na wengine
Mtu akijiona duni mwenyewe ni rahisi kwake kudhani kuwa watu wengine ndiyo wenye mambo ya kweli na hivyo kujikuta akifuata mkumbo na kupotoshwa katika ukweli. Ili mtu aweze kuwa sahihi katika mawazo ya vile anavyoamini ni lazima awe na tabia ya kupingana na wenzake. Ni jambo baya kukubaliana na watu katika mawazo yao bila kupinga katika kile unachoamini, kufanya hivyo kunaweza kuyafanya maneno ya uongo ya wengine yakaaminika na kuuacha ukweli wa mtu asiyejiamini ukipuuzwa kwa sababu tu hakuwa na ujasiri wa kukabiliana na hoja za wenzake.
 
Soma kitabu cha Dale Carnegie "How to develop self -confidence & influence people by public speaking"
Ndani ya kitabu kuna how to:-
-develop poise
-gain self-confidence
-improve your memory
-make your meaning clear
-begin and end a talk
-interest and charm your audience
-improve your diction
-win an argument without making enemies
Ni vyema ukapata hardcopy for own library.
 
Hivi vitabu huwa vinapatikana wapi?

Sent from my TECNO-J5 using JamiiForums mobile app
Kwenye maduka ya vitabu.
Kwa mfano kwa Mwanza vinapatikana pale mataa (nyerere/station/posta road) au waweza tembelea maduka ya vitabu ya Taasisi za Dini.
Nakumbuka mara ya mwisho niliviona pale Catholic Books Center Nyerere road Mwanza.
 
Pole sana nduguyangu. Tatizo la kupiga watoto ni baya kuliko maelezo. Wazazi wetu hawajajua tu. Na kuathirika na malezi ya ki tumwa na kikoloni, walidhani wanaafanya kitu kizuri. Research zinaonesha bakora zinasaidia pale tu zinapotumika sawasawa. Lakini kutumika sawa sawa ndio vipi? Ni sawasawa na kusema pombe nzuri kama ikitumika kidogo.

Confidence inaongezeka pale unapojua mambo vizuri. Kwahiyo jitahidi unapojifunza kitu kijue bila kubabaisha. Kila kitu. Ka namna hiyo hutaogopa kutetea hoja yako na watu watakubaliana na wewe tu.
 
Kitwange kama vipi, Mimi nilijenga confidence chuo kwenye presentation baada ya kupata mvinyo, nilipresent vizuri sana kwa Mara ya kwanza. Hadi namaliza mwaka wa Tatu nilikuwa hodari wa presentation kwani kila group likiniteua mimi kuwasilisha. Wengi hawakujua confidence na ujiniazi unatokea wapi.
 
Hilo tatizo linanitesa Sana
Ngoja nikupe siri kubwa ya kuongeza confidence. Kalili maneno ambayo unaweza kuongea zaidi ya dakika tatu, halafu nenda kasimame kwenye kioo kikubwa unachojiona angalau nusu ya mwili wako (kuanzia kiunoni hadi kichwani). Halafu anza kuongea yale maneno uliyokalili huku ukiitazama sura yako kwenye kioo, tena ikazie macho kweli na uitizame machoni. Nakuhakikishia, siku ya kwanza hutaweza kuongea maneno hayo zaidi ya dakika moja huku ukiiangalia sura yako. Lazima utaionea aibu sura yako. Jitahidi kufanya mazoezi haya mara kwa mara ili uweze kuongea kwa muda mrefu ukiwa unaiangalia sura yako. Baada ya hapo, utakuwa na confidence nzuri tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…