Msaada jinsi ya kuongeza "confidence"

Msaada jinsi ya kuongeza "confidence"

Ngoja nikupe siri kubwa ya kuongeza confidence . Kalili maneno ambayo unaweza kuongea zaidi ya dakika tatu halafu nenda kasimame kwenye kioo kikubwa unachojiona angalau nusu ya mwili wako( Kuanzia kiunoni adi kichwani).Halafu anza kuongea yale maneno uliyokalili uku ukiitazama sura yako kwenye kioo tena ikazie macho kweli na uitizame machoni.Nakuhakikishia siku ya kwanza hutaweza kuongea ayo maneno zaidi ya dakika moja uku ukiiangalia sura yako.Lazima utaionea aibu sura yako. Jitahidi kufanya ayo mazoezi mara kwa mara ili uweze kuongeza uwezo wa kuongeauku ukiitizama sura yako.Zingatia kuongea kwa sauti kubwa.Baada ya apo utakuwa na confidence nzuri tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
shukran mkuu
 
Hiyo no.9 ni sawa kabisa
  1. Shiriki sana katika Midahalo.
  2. Penda sana kujumuika na Watu na changia bila kujishtukia.
  3. Penda sana kuwafuatilia wale wote ambao kwako unawaona ni Mfano wako wa Watu wanaojiamini.
  4. Jenga tabia ya kuwa mbishi au kuanzisha ubishi hasa katika kadamnasi ya Watu.
  5. Jifunze kuwa Mtu wa utani utani mwingi.
  6. Hakikisha knowledge bank yako ni ya kutosha kwani 99.9% Confidence hunogeshwa na IQ kubwa ya Mlengwa.
  7. Jikite mno katika kufanya mazoezi ya kati au magumu kwani mara nyingi Confidence hujengwa na uimara wa mwili kwani mwili legelege huzaa " jitu " lisilojiamini siku zote.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nadhani kusudio halisi la dini watu hawalifahamu sawa sawa. Pata neno jipya kwamba tunamwabudu Mungu kwa ajili ya afya njema. Afya njema ni pamoja na kujiamini.

Tumia hekima ya Mungu kutatua tatizo lako kwa kujifunza neno lake na kufanya ibada. Tatizo hilo litakwesha.

Habari zenu wanajamvi,

Leo ningependa kufundishwa njia zitakazo niwezesha kuwa mtu wa kujiamini niwapo mbele ya watu. Nasikitika sana juu ya tatizo hili ambalo toka utotoni mwangu hii nimegundua jinsi malezi yangu yalikuwa ndiyo chanzo cha kupungua kujiamini kwani nilikuwa napigwa sana hivo kuuliza kitu ama kuongea ilikuwa ngumu kwangu hivo mpaka sasa nimekuwa muhanga mkubwa.

Naomba kujuzwa mbinu zitakazonifanya niwe bora zaidi katika kujiamini,
Kwani now najiandaa kwenda chuo nikiwa na tatizo hili ndani ya kichwa changu.
 
Habari zenu wanajamvi,

Leo ningependa kufundishwa njia zitakazo niwezesha kuwa mtu wa kujiamini niwapo mbele ya watu. Nasikitika sana juu ya tatizo hili ambalo toka utotoni mwangu hii nimegundua jinsi malezi yangu yalikuwa ndiyo chanzo cha kupungua kujiamini kwani nilikuwa napigwa sana hivo kuuliza kitu ama kuongea ilikuwa ngumu kwangu hivo mpaka sasa nimekuwa muhanga mkubwa.

Naomba kujuzwa mbinu zitakazonifanya niwe bora zaidi katika kujiamini,
Kwani now najiandaa kwenda chuo nikiwa na tatizo hili ndani ya kichwa changu.
Mkuu ukipata Majibu Nasisi utusaidie wenye Changamoto kama yako hiii
 
Habari zenu wanajamvi,

Leo ningependa kufundishwa njia zitakazo niwezesha kuwa mtu wa kujiamini niwapo mbele ya watu. Nasikitika sana juu ya tatizo hili ambalo toka utotoni mwangu hii nimegundua jinsi malezi yangu yalikuwa ndiyo chanzo cha kupungua kujiamini kwani nilikuwa napigwa sana hivo kuuliza kitu ama kuongea ilikuwa ngumu kwangu hivo mpaka sasa nimekuwa muhanga mkubwa.

Naomba kujuzwa mbinu zitakazonifanya niwe bora zaidi katika kujiamini,
Kwani now najiandaa kwenda chuo nikiwa na tatizo hili ndani ya kichwa changu.
Kula mneli tu Sana Sana skanka
 
wadau wameongea mengi mazuri,binafsi hlo tatzo nilikuwa nalo lakini saiv limepungua kwa 95%,mimi nilipewa tips zote hazikunisaidia,nilichoamua ni kujitatmini mwenyewe.mimi mara ya kwanza niliamua kutumia hasira yani nikishakuwa nimezungukwa na watu wanaonitazama bhasi lazima nijikumbushe makusudi kitu kinachoniudhi maana fact ni kuwa aibu mara nyingi kama si zote itakupelekea ucheke au utabasamu na ukicheka au kutabasamu utaonekana tuu kuwa una aibu.sasa hapo nikishakuwa na hasira kias nakuwa serious ila naavoid kuonesha usoni hasira bhasi siwezi kucheka bila sbabu,hapo naweza kupresent part yangu na nikakaa mbele ya darasa hata lisaa zima bila kuonesha aibu.badae aibu ikapungua kwa kias kikubwa kwa mbinu hyo nikajikuta nazoea mikusanyiko.

badae nikaamua kuachana na hiyo,nikaanza kukaza macho kwa yeyote atayeniangalia hadi aone aibu yeye.nikigundua unanitolea mimacho na mimi nakuangalia mwanzo mwisho hata kama ni dkk 2,lazima utakwepesha mwenyewe either kwa kuangalia chini au pembeni,hapo nishakuwin confidence huwez rudia tena.nikiona mbishi kuona aibu naweza hata nikaonesha ishara(facial expression)fulani kama kunyanyua nyusi,ukicheka nimemaliza.

kwenye presentation huwa namake sure kazi nimeielewa vizur assignment,nilikuwa napenda kuandaa assignment mimi(kugoogle😀😀kutype nk) ili siku ya kuwasilisha niwe confortble,nipate maks nzuri individually,swali lolote litakaloulizwa toka kwa audiance nilijibu accordingly,sometimes nilikuwa najiandaa kwa kusoma grammar kidogo nipunguze broken,nilikuwa navaa vizuri hadi niamini nimependeza siku ya presentation,make sure upo smart kila idara.

kwenye group discussion napo kuna challenge,hapo mpo jinsia tofauti halafu kama ndo first year hamjuani,kuna wajuaji,washushuaji,attacker,wapenda sifa nk.sasa hapo lazima uwe vzuri psychologically,kuwa normal usiact toa point zako au hoja yako na itetee,hapo aibu unaweza kuitoa kwa kuzuga na simu tuu,unajifanya unagoogle,unachati,au unasoma text nk(saiv simu inasaidia) ukiona mtu anakukodolea macho hasa wa jinsia jirani;na wewe mwangalie mwanzo mwisho,akizid mkonyeze😀😀.nilijikuta nakuwa confident hata kwenye course tunazoshea kama development studies tupo kwenye hall kubwa takribani watu 200 naweza nyanyua mkono ili niulize au kujibu swali nikiwa back bencher,marafiki zangu wakawa wananikataza eti "nawashazisha" wakawa wanaona aibu wao tena.
we dogo umenifanya tang jana nikitembea majiani mwendo wa kukodoleana mimacho tu na nnaopishana nao ..mtu akinianagalia na mie na muangalia mwisho hua anatoa yeye mwenyewe salam na anakua dhaifu kwangu kiukweli hii comment yako imenizidisha ujasiri sana ..kwakweli nimeisave kwenye folder kwa matumizi ya baadae ...ikitokea confidence imepungua hua lazima nikipitie kimsemo chako ili niwe imara zaid
 
Piga kinywaji kidogo tatizo litaisha utanishukuru baadaye
 
Ni confidence, siyo ulivyoandika wewe.

Soma kitabu cha Dale Carnegie "How to win friends and influence (influential) people" kitakusaidia sana kupita maelezo. Kitabu hicho ni my all time favorite kati ya vitabu vya "how to...".
Naomba unisaidie hiki kitabu ndugu
 
Ni confidence, siyo ulivyoandika wewe.

Soma kitabu cha Dale Carnegie "How to win friends and influence (influential) people" kitakusaidia sana kupita maelezo. Kitabu hicho ni my all time favorite kati ya vitabu vya "how to...".
Bi mkubwa hongera kwa kupitia hiyo kitabu
 
"If you hear a voice inside you says don't paint then by all means paint and the voice will be silenced"
 
Pia tafuta kitabu cha Atomic habits by James clear usome.Pia Acha nyeto mpaka ugain confidence jaribu kuongea mbele ya watu mdogo mdogo utaweza alafu nawe siku utashangaa utakuwa motivational speaker mzuri kuinua wengine
 
Pia tafuta kitabu cha Atomic habits by James clear usome.Pia Acha nyeto mpaka ugain confidence jaribu kuongea mbele ya watu mdogo mdogo utaweza alafu nawe siku utashangaa utakuwa motivational speaker mzuri kuinua wengine
Tujaribu kuhandle small group of people the way tunatarajia kuhsndle group kubwa of people.

Mara nyingi sana hatujali pale thnapoongea na watu wachache alafu tunakuja kujali pale tunapotaka kuongea na watu wengi.

Kama unataka kuwa mzungumzaji mwenye pints mbele ya watu wengi basi hakikisha unakuwa mzungumzaji mzuri mwemye points mbele ya watu wachache kwanza hata wewe na mkeo na wanao au na marafiki kazini.

Unataka kuwa na confIdence mbele ya watu wengi hakikisha unakuwa na confidence mbele ya watu wachache kwanza.

Kama unatakka kuwa mchekeshaji mbele ya watu wengi hakikisha unskuwa mchekeshaji mbele ya watu wachache kwanza.

"The way you do something it's the way you do everything"
 
Back
Top Bottom