Msaada juu ya kufuatilia mirathi

Msaada juu ya kufuatilia mirathi

Kama taratibu zote zimefanyika na mahakama ikatoa hati ya usimamizi kwa aliyeteuliwa/chaguliwa lakini Baada ya miaka miwili au mitatu ikatokea labda ndugu wengine hawakuridhika inakuwaje hapo?
Inabidi hao ndugu waende mahakamani wakiwa na sababu za msingi au zinazofaa kumuondoa huyo msimamizi.

Hivyo basi mahakama lazima iridhike na sababu walizotoa na kama itaona sawa kumuondoa msimamizi ili kuokoa mali zilizoachwa na marehemu, hakika lazima itafanya hivyo.


Ingawa mahakama huwa inapewa utashi mkubwa sana wa kumuondoa msimamizi yani unaweza peleka hizo sababu na bado zikapigwa chini na mahakama.
 
1. Inatakiwa mkae kikao cha familia kumchagua mtu wa kufuatilia cheti cha kifo (kama hakipo) mnaandika mhutasari wa kikao.
2. Unaenda ofisi ya serikali ya mtaa kuchukua barua ya utambulisho inayokutambulisha wewe kuwa umechaguliwa kufuatilia cheti.
3. Unapeleka Mahakamani kuthibitishwa.

KUFUATILIA MIRATHI
1. Mnarudia hatua ya kwanza hapo juu saivi kichwa cha habari kinakuwa kufuatilia MIRATHI ya marehemu fulani.
2. Unarudia hatua ya pili hapo juu
3. Unaenda mahakamani ukiwa umeambatanisha mhutasari na barua ya familia inyokupendekeza kuwa umechaguliwa kufuatilia MIRATHI, barua iandikwe kwenda kwa hakimu wa mahakama husika ya kumuomba kumpitisha msimamizi wa MIRATHI
Kinachofuata ni mteremko tu kuwa unapewa utaratibu nini cha Kufanya...!!
 
Inabidi hao ndugu waende mahakamani wakiwa na sababu za msingi au zinazofaa kumuondoa huyo msimamizi.

Hivyo basi mahakama lazima iridhike na sababu walizotoa na kama itaona sawa kumuondoa msimamizi ili kuokoa mali zilizoachwa na marehemu, hakika lazima itafanya hivyo.


Ingawa mahakama huwa inapewa utashi mkubwa sana wa kumuondoa msimamizi yani unaweza peleka hizo sababu na bado zikapigwa chini na mahakama.
Ni ndugu ambao wamejitokeza na kudai kuwa wao ni watoto WA marehemu na vithibitisho wanavyo lakini sisi kama familia tulishafungua tayari, vipi kuhusu hawa wengine waliojitokeza
 
Ni ndugu ambao wamejitokeza na kudai kuwa wao ni watoto WA marehemu na vithibitisho wanavyo lakini sisi kama familia tulishafungua tayari, vipi kuhusu hawa wengine waliojitokeza
Mzee aliacha wosia Mkuu?
 
Okay!

Vipi mali mshagawana mkuu?

Kama bado jaribuni kuwafikiria hao ndugu zenu Mkuu.

Inamaana mnaweza kukaa kama familia mkaelewana ili na wao waweze kupata chochote.

Sema familia zetu hizi unakuta zina roho mbaya sana ishu kama hiyo kuna watakaogoma kuwaelewa kabisa na kupelekea migogoro ya hapa na pale.
 
Kama taratibu zote zimefanyika na mahakama ikatoa hati ya usimamizi kwa aliyeteuliwa/chaguliwa lakini Baada ya miaka miwili au mitatu ikatokea labda ndugu wengine hawakuridhika inakuwaje hapo?
Inawabidi wapeleke malalamiko yao mahakamani!
 
Je kuna umuhimu au ulazima wa kuwa na Kaza Hukumu katika Mirathi?
 
Back
Top Bottom