Msaada katika tuta> Ubabe wa shule binafsi

manmasai

New Member
Joined
Jun 11, 2008
Posts
4
Reaction score
0
--------------------------------------------------------------------------------
Salaam Wakubwa humu jamvini

jamani kuna swala linanisumbua, hivyo naomba michango yenu kimawazo....

eti ni kwa nini baadhi ya shule binafsi nchini zinaendeshwa kama miradi ya kuku, kwani wamiliki wake wanashindwa kuwa na mipango endelevu na taratibu nzuri za kiuendeshaji. taratibu hizo zinaweza kuwa za kifedha, uongozi na utawala ikiwa ni pamoja na utoaji wa maamuzi mbalimbali mazito juu ya hatma ya wanafunzi bila kujali utu.

Mfano hai ni huyu Mrs. Bayi mbaye ni Mke wa Bw. Bayi nani Mwenyekiti wa Bodi ya shule ya sekondari ya Filbert Bayi. Jamani huyu mama amekuwa na mtindo wa kujichukulia mamlaka makubwa mikono mwake kiasi cha kufukuza wanafunzi bila kuzingatia sheria na taratibu mbalimbali.

tafadhali mawazo (ideas) needed
 
Kama nani amefukuzwa bila mpango ? Unaweza kutaja jina lake ? Manmasai umeshasema ni shule binafsi kwahiyo nyingi zinaendeshwa kwa interest za hao wanaomiliki shule lazima ufuate misingi na sheria wanazozitaka wao wanasema wenyewe interneshno starndads , mimi nimesoma shule binafsi kwa muda na bahati nzuri mmoja wa wazazi wangu alikuwa mmiliki wa shule hizo kwahiyo kuna kasheshe sana msee wangu usiseme huko rushwa ndio mtindo mmoja
 
shy ni kweli ila kama mtu hawezi kuendesha mradi wa shule, basi asifanye. sio uungwana mtu kuwa diktekta hata katika mambo yenye maslahi na uhai wa mtu.
 

Hayo ni matatizo ya kutoheshimu sheria. Kwa maoni yangu ni kuwa mara unapoamua kuanzisha shule binafsi na ukaandikisha watoto wa watu inakoma kuwa ya binafsi 100%. Hii ni kwa sababu wazazi wa watoto wanakuwa nao ni wabia wa hiyo shule. Vinginvyo shule hizo zingefundisha watoto wa wamiliki tu! Kwa sababu ya kiburi na rushwa, sheria hazifuatwi na shule kama yalivyo mambo mengine hapa Tz (ikiwemo ikulu) zinaendeshwa kama private bedroom. Hayo ni makosa makubwa sana! Kama serikali imeshindwa, wazazi kwa pamoja wanaweza kuchukua hatua au la, kila mmoja achukue hatua kivyake vyake! Kuna shule moja ambayo imepoteza idadi kubwa ya wanafunzi na walimu kwa sababu ya ubabe wa mwenye shule! Wakiendekeza mchezo watazifunga tu!
 
Tabia mbaya/nzuri haijifichi ktk utendaji wa mtu. Kuna watu wameongoza taasisi za serikali kwa ufanisi mkubwa na wengine wameongoza taasisi binafsi kwa ufanisi mkubwa. Ninachotaka kusema ni kwamba pande zote mbili watendaji wazuri na wabaya wapo.Taasisi binafsi nyingine zimeanzishwa kama fasheni ipitavyo na zimeanzishwa na watu ambao hawakujiandaa/hawajui utawala/uongozi wa taasisi walizozianzisha.
 
wengi wenye shule binafsi ni wafanyabiashara ambao hawana lingine zaidi ya kujianzishia shule kupata pesa za haraka haraka ndio maana walimu wanawatoa nje au wengine walimu wao hawana uzoefu na mambo ya ufundishaji mwisho kabisa wengi wanachukulia hili kama miradi
 
Kama ndivyo alivyo basi anapata kiburi kwa sababu labda ni shule ya mumewe!hata hivyo kama kuna mtu amefukuzwa bila kufuatwa kwa taratibu basi anaweza kudai haki yake ya msingi!
 
mimi nina mwanangu anasoma Academic international school A level. juzi juzi wakati wa sakata la migomo ya waalimu,waalimu wa shule hiyo nao waliiomba menejimenti ya shule iwaongeze mishahara. ikaenda menejimenti ya shule wakasema hawana hela za kuongeza kwa sababu tayari ada inayotozwa ni kubwa kidogo na hawangependa kuwaongezea wazazi mzigo zaidi.ada kwa term kwa wanafunzi wa sekondari ni shs 900,000 mbali na usafiri na vitu vingine.

waalimu wakatishia kuhamia shule nyingine,kuona hivyo menejimenti ya shule ikatuandikia barua wazazi kutuelezea sakata hilo na kwamba imeamiliwa kuanzia Jan 2009 ada itaongezwa na kuwa milioni moja kwa term i.e ongezeko la Shs 100,000 kwa ajili ya kuwalipa waalimu

Ndugu zangu hii kweli imekaa sawa? hawa watu hawajui wazazi tunaumia,kwanini mzigo huu wabebeshwe wazazi?
 

Swali lako Kawaulize CCM!!!
 
πŸ˜€ Pole sana ndugu yangu. Na wengi ni wakeleketwa na makada wa CCM.
Ngoja nikupe mfano hai.
Kuna shule moja kule Bukoba inaitwa Amani/Peace Primary and secondary school inamilikiwa na Kada wa chama cha mapinduzi ambaye amewahi kuwa mwenyekiti wa chama cha mafisadi tanzaniaπŸ˜•
Shule hii ina wanafunzi wengi saaaaaaaaaana kupita hata capacity ya shule. Lakini aachi kupokea mwanafunzi katu.
Hata ukienda kuulizia shule bado siku moja shule kufungwa ilimradi una shekeli mkononi utapokelewa.
Pamoja na sheria zetu sijui kama viongozi wa wizara ya elimu wanakwenda kufanya ukaguzi wa shule ile.
Hizi shule tunazipenda sawa lakini zina shida nyingi na wanafunzi wanasoma katika mazingira magumu.
Binafsi nilisoma shule moja ya mtu binafsi miaka ya 1974 kule Tarime katika shule moja inaitwa Shirati. (Sasa hivi shule hii ni marehemu maana haipo tena) kwa kweli tuliishi maisha ya shida miaka yote 4. Na hakuna aliyekuea akitusikiliza.πŸ™
 

Pole. Lakini biashara ndio inavyoenda, costs zinakua passed on to the consumer eventually.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…