specialist88
JF-Expert Member
- Aug 31, 2014
- 1,140
- 618
Habari wana JF.
Ndugu zangu kuna shida inamsumbua jirani yangu,nimeona niilete hapa jukwaani ili tuone namna yakumsaidia huyu binadamu mwenzetu.
Kuna familia moja (majirani zangu) walipata mtoto wao (first born) wakike-mwaka jana mwanzoni. Kwa bahati mbaya, mtoto wao alizaliwa na tatizo la kuwa na kichwa kikubwa, kichwa kinaongezeka kadri muda unavyoenda. Mtoto amefanyiwa operation, amewekewa mpira wa kutolea maji kichwani lakini wapi! Kichwa bado hakipungui.
Hii familia imehangaika katika hospitali za KCMC, SELIAN na MUHIMBILI lakini wapi! Tatizo bado lipo pale pale! Kibaya zaidi hii ni familia isiyo na kipato kikubwa, mke ni mwalimu na baba ni mfanya biashara ndogo ndogo tu.
Kwakweli, hii familia imehangaika vya kutosha mpaka nawaonea huruma! Kila siku wao ni hospitali. Imefikia hatua mpaka baba mtoto ameacha biashara yake angalau amsaidie mke wake kukaa na mtoto, maana mke wake hawezi kumbeba kumpeleka hospitali kwa jinsi alivyo mzito huyo mtoto, maana kwa sasa tumbo la mtoto nalo limeanza kuwa kubwa.
-----------------------------------
Sasa naomba ndugu zangu, kama kuna mtu/ watu wenye uwezo wa kiushauri, kipesa au mwenye kuweza kum-connect na watu wanaoweza kumsaidia (kama wafadhili, mashirika yanayopelekaga watoto nje au India kufanyiwa matibabu) naomba wajitokeze kuisaidia hii familia tafadhali.
Nawaomba ndugu zangu jamani tuisaidie hii familia.
Ndugu zangu kuna shida inamsumbua jirani yangu,nimeona niilete hapa jukwaani ili tuone namna yakumsaidia huyu binadamu mwenzetu.
Kuna familia moja (majirani zangu) walipata mtoto wao (first born) wakike-mwaka jana mwanzoni. Kwa bahati mbaya, mtoto wao alizaliwa na tatizo la kuwa na kichwa kikubwa, kichwa kinaongezeka kadri muda unavyoenda. Mtoto amefanyiwa operation, amewekewa mpira wa kutolea maji kichwani lakini wapi! Kichwa bado hakipungui.
Hii familia imehangaika katika hospitali za KCMC, SELIAN na MUHIMBILI lakini wapi! Tatizo bado lipo pale pale! Kibaya zaidi hii ni familia isiyo na kipato kikubwa, mke ni mwalimu na baba ni mfanya biashara ndogo ndogo tu.
Kwakweli, hii familia imehangaika vya kutosha mpaka nawaonea huruma! Kila siku wao ni hospitali. Imefikia hatua mpaka baba mtoto ameacha biashara yake angalau amsaidie mke wake kukaa na mtoto, maana mke wake hawezi kumbeba kumpeleka hospitali kwa jinsi alivyo mzito huyo mtoto, maana kwa sasa tumbo la mtoto nalo limeanza kuwa kubwa.
-----------------------------------
Sasa naomba ndugu zangu, kama kuna mtu/ watu wenye uwezo wa kiushauri, kipesa au mwenye kuweza kum-connect na watu wanaoweza kumsaidia (kama wafadhili, mashirika yanayopelekaga watoto nje au India kufanyiwa matibabu) naomba wajitokeze kuisaidia hii familia tafadhali.
Nawaomba ndugu zangu jamani tuisaidie hii familia.