Msaada kiwanda kidogo cha maziwa

Baijan

Member
Joined
Nov 23, 2014
Posts
11
Reaction score
5
Naomba ushauri nataka kujua vitu gan vinahitajika kwa ajili ya kiwanda kidogo cha kusindika maziwa na product zake zingine na mtaji ni sh ngapi inabid nitafute maana nataka nianze na iyo ila plan kubwa nataka kudeal na mazao ya kilimo kuyaprocess kwenye viwanda vidogo nitakavyoweza kuanzisha kadiri ya mungu atakavyojalia asante
 

Kabla ya yote, onana na jamaa wa TFDA ili wakuambie 'sera' zao kuhusu mradi huu.
Maana, unaweza ukawekeza sana, halafu jamaa hawa wakaja kupiga kufuli kiwanda chako.
Jamaa hawa kero sana hawa..!!
 
Kabla ya yote, onana na jamaa wa TFDA ili wakuambie 'sera' zao kuhusu mradi huu.
Maana, unaweza ukawekeza sana, halafu jamaa hawa wakaja kupiga kufuli kiwanda chako.
Jamaa hawa kero sana hawa..!!

Nikweli,hawa jamaa ni kero kweli.
Unaweza kupewa masharti ya Bakhressa ukapewa wewe maskini.Ili mradi tu wakubwa walindwe.
Kwanza kupata kibali chao ndio kazi,kuna watu wamesota muda mrefu mpaka wakabadilisha mawazo.
 
Familia yetu tuna idea kama yako lakini plan ni pale tutakapoweza kuzalisha maziwa yetu at least kuanzia lita 300 hadi 1000 kwasasa tuna lita 80 kwa siku Mungu akijaalia mwakani mwezi wa 6 tutakuwa na uwezo wa kuzalisha lita 150. Tuko meli moja ushauri utakaotolewa utasaidia wengi
 
Asante kwa mawazo yenu ila kuna mtu kaniambia nipitie sido kwamba ndo kila kitu na inakua rahis nikipita huko ni kweli??
 
Asante kwa mawazo yenu ila kuna mtu kaniambia nipitie sido kwamba ndo kila kitu na inakua rahis nikipita huko ni kweli??
Nikweli,pale Sido ukahudhurie mafunzo ya usindikaji,maana hata hao TFDA wanauliza kama mhusika anaelim yoyote yenye cheti kwa kazi hiyo.
Na pale SIDO unakuwa umewezeshwa kutambulika kama mjasiriamali mdogo ambayo ni credit kwako pia.
Watu tunashindwa kujua ila pale SIDO ni hazina kubwa sana vijana,sema tu watu tunaona kama hakuna kitu.
Watu wengi wenye kupita pale wanakuwa wanajua njia zote na mbinu zote za biashara husika.Na pia SIDO wana vitengo maalum vya kusaidia wahitimu wao either in group au mmoja mmoja.

Na vote pia nenda SIDO
 
Ni kweli hata Mimi nilikuwa na mpango wa kuanzisha kiwanda kidogo cha sabuni nikaambiwa nianzie sido
 
Mimi ninavyo jua TFDA au TBS hutoa kibali kwa bidhaa ambayo tiyari imeisha anza kazi, TBS hawawezi kukupa kibali halafu ndo ukaanze kutafuta mitambo even TFDA kwa sababu wanakuja kukagua production yako ndo wakupe kibali, so chakufanya hata ukiwaona watakupatia mwongozo tu na wewe utaanza kazi n then watakuja kukagua kuona kama unafuata mashariti yao ndo sasa upewe kibali rasimi au la.

Huwezi pewa kibali kabla hujaanza productions na TBS hivyo hivyo ni lazima uanze kwanza ndo waje kukagua na wana tabia ya kufanya ukaguzi wa kushitukiza utashangaa gari inafunga break mlangoni kwako, so unatakiwa kuhakikisha walio kuambia unayafuata yote.
 
Tatzio ni kwamba mie sielewi TBS na TFDA majukum yao ni yapi kwenye hili.
Maana kuna vitu naona wanaingiliana.
Maana TFDA nao pia lengo ni kuangalia ubora,na TBS ni yaleyale sasa wenye kujua watufafanulie.
Maana najua vipo viwanda ambapo TFDA walitoa kibali TBS wakazuia.Na hoja ni moja
 

Pia ni lazima uwaone kwanza kabla hata hujaanza kujenga hata tofali moja la kiwanda chako.
Jamaa hawa wana taratibu zao za ujenza wa viwanda, na ramani ya kiwanda chako lazima iwe inafuata 'process flow' yao TFDA.
Ukijenga tofauti tu, na wakija kukagua na kukuta 'process flow' sio kama wanavyotaka, wanakufungia kiwanda mpaka utakapo rekebisha jengo..!!!!
Hivyo, lazima uwaone kabla ya kuanza kujenga kiwanda.
TBS nao ni hivyo hivyo, watakwambia jengo lako halikidhi 'viwango' vya kutunza 'afya' ya walaji wa bidhaa zako...!!!!!
Ogopa sana TFDA...!!!!
 

Hapa ndio nasema kwamba TFDA na TBS kwa hii kazi wote wanafanya kitu kimoja na kufanya mlolongo kuwa mreeeeeefu.
Kila siku watu wanalalamikia hivi vibali vyao,maana mmoja akikupitisha usishangae mwingine akakufelisha
 
Wazo zuri na Hongera sana, ushauri wangu unahitaji upate roadmap na njia pekee ni kutengeneza business plan mkuu wangu. I can volunteer to guide you and any one who need to come with such kind of projects. Thanks
 
TFDA ni regulator yeye anajikita katika safety of the product Wakati TBS yeye anajikita katika ubora yaani quality,
 

Kozi zao ni za muda gani ada sh. ngapi?
 
TFDA ni regulator yeye anajikita katika safety of the product Wakati TBS yeye anajikita katika ubora yaani quality,

Nakubaliana mkuu,ila ukaguzi wao ni uleule wote unafanana,sema tu wewe umeandika kizungu kingi .
Safety of the product na hao wengine quality of the product,sasa ukiangalia ni yale yale tu,wote wanapita katika mchakato mmoja ule ule.
Mtafute mtu aliewahi kufanyiwa ukaguzi na hao wote atakuambia mahitaji yao yanafanana.
 

Kaka,TFDA na TBS ni taasisi mbili tofauti na ziko chini ya wizara mbili tofauti.
TFDA iko chini ya wizara ya afya na ustawi wa jamii na inasghurika na ubora wa dawa na chakula na usalama kwa mlaji LAKINI TBSA ipo chini ya wizara ya Viwanda,Biashara na Masoko yenyewe inashughulika na viwango vya ubora vya bidhaa vyote katika sekta zote

Naweza nikakusaidia namna ya kufuata procedure na kusajiriwa na hawa jamaa.
Asante
 
Asante mkuu,nitaktafuta,nikifungua Bakery mwakani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…