Msaada: Kodi kwa kuanzisha kampuni

duet

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2013
Posts
534
Reaction score
149
Salaam,
Ndugu wadau nahitaji msaada wa kujulishwa ni kodi zipi (kama zipo) hulipwa wakati wa kuanzishwa kwa kampuni? Na je kiasi cha mtaji wakati wa kuanzisha kampuni kina athari yoyote katika ulipaji kodi hizo (kama zipo)? Nitashukuru endapo nitapata majibu ya uhakika na ya kitaalamu.
 
Kodi zipo kaka hasa kama huna TIN number watakuhuliza kuhusu mtaji wako aina ya kampuni then watakuhuliza kama eneo ni lako au umekodisha kama umekodisha watataka nakala ya mkataba ikiwa ni pamoja na risiti za malipo ya eneo hilo kwa tra kama halijalipiwa kodi basi watakupgia hesabu ya kodi unayolipa then watakalculate kwa kodi hiyo lakini ningekushauri uende TRA Watakupa ushauri mzuri
 
Unapopatiwa TIN kuna kodi za aina mbili. Moja ni withholding Tax from Rent (10% of rent), kama nyumba ni ya kwako utawasilisha risiti ya malipo ya kodi ya majengo uliyolipa hivyo hutalipa kodi hiyo. kodi ya pili unakadiriwa kwa mwaka wa kwanza. makadirio yake hutegemea mambo kadhaa kama amount of share capital, type of business, ect. Kodi itakayokadiriwa inagawanywa katika vipindi vinne vya mwaka ambapo utaruhusiwa kulipa kwa vipindi vinne kwa mwaka. Nadhani utakuwa umeelewa kwa kiwango fulani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…