Msaada: Kozi gani nzuri ya kusomea Wizara ya Utalii/ Maliasili

Msaada: Kozi gani nzuri ya kusomea Wizara ya Utalii/ Maliasili

She Quoted you

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2020
Posts
687
Reaction score
1,184
Hello jF,

Mdogo wangu amemaliza shule form four amefaulu vizuri.

Hataki kwenda advance ila anataka asomee course/diploma inayohusiana na mambo ya utalii/maliasili mfano chuo. Cha Mweka Kilimanjaro.

Naombeni msaada Ni Kozi gani nzuri zenye future katika hii sekta?
 
Duuh kwani anapassion ya mambo ya utalii!?? Na Je anataka aje aajiriwe au Ajiajiri katika mambo ya utalii!??
 
Unazungumzia maliasili ipi?
Maliasili kuna misitu, nyuki na wanyamapori, utalii ni kitu inajitegemea.
Hivyo kama ameamua upande huo wa MWEKA make atasoma wildlife au tourism, nje na hizo anakuwa amebakisha misitu, teknolojia ya viwanda vya misitu na ufugaji nyuki. Kwa hiyo kama ataona kuna kinachomfaa miongoni mwa hivyo achague kimojawapo.
Kikubwa achague kulingana na passion na baada ya kuvielewa vyote vinahusu nini na fursa zake ni zipi.
Kila la kheri.
 
Unazungumzia maliasili ipi?
Maliasili kuna misitu, nyuki na wanyamapori, utalii ni kitu inajitegemea.
Hivyo kama ameamua upande huo wa MWEKA make atasoma wildlife au tourism, nje na hizo anakuwa amebakisha misitu, teknolojia ya viwanda vya misitu na ufugaji nyuki. Kwa hiyo kama ataona kuna kinachomfaa miongoni mwa hivyo achague kimojawapo.
Kikubwa achague kulingana na passion na baada ya kuvielewa vyote vinahusu nini na fursa zake ni zipi.
Kila la kheri.
Unaweza kuelezea mkuu hizo kozi zinahusu nini na fursa zake ni zipi?? Mimi pia nataman kufahamu
 
Ushaur wangu asisomee hayo madude....kazi za kuajiriwa sio...akitaka kujiajir upande huo lqlazima awe na mtaji wenye uhakika,la sivyo ataishia kupata stress tu
 
Ushaur wangu asisomee hayo madude....kazi za kuajiriwa sio...akitaka kujiajir upande huo lqlazima awe na mtaji wenye uhakika,la sivyo ataishia kupata stress tu
Asante..un ashauri asomee kipi cha kujiajiri boss?
 
Ushaur wangu asisomee hayo madude....kazi za kuajiriwa sio...akitaka kujiajir upande huo lqlazima awe na mtaji wenye uhakika,la sivyo ataishia kupata stress tu
Hivi hauwezi kuanzisha outsource company kwenye utalii ili uwafanyie kazi company kubwa mfano za kuwatafutia watalii,logistic,security nk nawe uwe unapata kidogo? Hao ma afusa utalii haiwezekani awe anadili na watalii wa hali ya chini na kila kitu kiwe cha kukodi, mfano gari, malazi no.
Ninafikiria mie mwenyewe kumpeleka mjomba wangu chuo cha utalii na eneo lake la kazi liwe Kigoma ambapo ni nyumbani.
Je haiwezekani kabisa akajiajili kwa out source.
 
Unaweza kuelezea mkuu hizo kozi zinahusu nini na fursa zake ni zipi?? Mimi pia nataman kufahamu
Hapo kuna kozi kama ya Ufugaji Nyuki hii inahusika na masuala yote yanayohusu usimamizi wa rasilimali nyuki na teknolojia yake. Hii ni kozi maalum na adimu maana Diploma level inatolewa Tabora pekee na Bachelor level ni UDSM na SUA, unaweza kuajiriwa taasisi mbalimbali za maliasili, mazingira, viwanda, biashara na kilimo. Pia, unaweza kujiajiri kwa kufuga nyuki kuzalisha asali, nta, sumu ya nyuki, maziwa ya nyuki, chavua, uchavushaji wa mazao n.k.
Kozi nyingine ni ya Misitu, huko utajifunza kila kitu kuhusu rasilimali misitu kama vile Forest ecosystems, economics, resources assessment and management na engineering. Na unaweza ukasoma kozi zingine ndani ya hiyo kozi kama vile usimamizi wa wanyamapori na ufugaji nyuki pamoja na tourism. Hii pia inatolewa kwa level ya Diploma Moshi, Arusha, na UDOM, kwa Bachelor ni SUA pekee. Ni kozi muhimu sana na mwajiri mkuu ni Serikali lakini kuna NGOs nyingi sana zinahusika na masuala ya misitu kwa uchache ni WWF, TFCG, IUFRO n.k.
Kozi zote zinafaa sana, ila ukipiga kitabu kwa bidii kutoka ni nje nje.
Zingine kama Utalii na Usimamizi wa Wanyamapori ni kozi za maliasili pia.. Natumaini kuna wataalam wanaweza kuzielezea vizuri pia.
Kila la Kheri.
Pia aione She Quoted you
 
Back
Top Bottom