Msaada: Kuandika Wosia

SHIEKA

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2011
Posts
8,240
Reaction score
4,265
Nawasalimu wanasheria wote wa jukwaa hili.
Mimi nataka kuandika wosia wangu. Nauliza, je, wosia unaandikwa kwa msaada wa wakili/mwanasheria au unajiandikia
mwenyewe ukiwa chumbani mwako? Na je, ipo format/template maalum ya kisheria ya kuandika wosia au mtu unajiandikia tu kulingana na mawazo yako kichwani?

Naomba sana kusaidiwa kwa jambo hili. Mimi naishi Moshi.
Asanteni
 
nenda kwa wakili akupe mwongozo au format...naamini haitakuwa gharama sana.....lakini kwa ufupi vitu muhimu ni....
1.lazima umeandikwa kwa kalamu ya wino au umechapwa.....
2.tarehe ya siku hiyo.......
3.na mashahidi wawili ambao asiwe mtu wa karibu kama mtooto au mke n.k (mwenye kuweza kurithi)
4.uwe siri warithi wasifahamu..n.k ..lakini hayo ndio muhimu.....

kwa maelezo zaidi nipm.....
 

Unaeza tu kuandika mwenyewe zingatia tu vitu ulivyotajiwa hapo juu,wakili unaweza kumpa autunze tu kama custodian
 
tatizo lako dogo sana. tafuta kitabu hiki, hakika utarudi na kunipm shukran.

SHERIA KWA KISWAHILI

View attachment 114184

View attachment 114185View attachment 114185
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…