Msaada kuhusu mikopo ktk benki zetu..

MGASON

Member
Joined
Nov 19, 2011
Posts
65
Reaction score
35
Wadau mimi mshahara wagu total ni 650,000 ukiondoa makto take home ni 540,000.naitaji kampuni yetu ipitishie mishahara yetu benki ya crdb au kcb ili turuhusiwe kuchukua mikopo, hivyo naomba mwenye ufahamu anijuze kwa mshahara huo nikikopa milioni 10.

Nitaweza katwa sh ngapi na nitabaki na nini take home?then ni benki gani unaweza kunishauri yenye unafuu hapa dar? hatujaanza kupitishiwa mishahara benki but tumeambiwa tuamue ni benki gani then mwajiri wetu apitishie huko mishahara yetu.

Ushauri plz wadau.
 
Ukikopa 10,000,000 kwa mwaka mmoja at 17 pc interest rate utalipa Tshs 912,047.52 pm. , ukikopa kiasi hicho hicho (10,000,000) kwa miaka miwili utalipa, Tshs 494,422.64 pm, kwa miaka mitatu ni Tshs 356,527.28 pm na kwa miaka minne ni Tshs 288,550.42 na kwa miaka mitano (ambayo ndiyo kikomo) ni Tshs 248,525.76 pm. Kwa mshahara wako unaweza/utaruhusiwa kukopa 5, 000,000 kwa miaka mitatu at 17 pc interest rate kwa miaka mitatu, ambapo utakuwa unalipa Tshs 178,263.64 pm . Benki nzuri ni Azania, crdb ambazo interest rate ni 17 pc/annum.
 

asante sana kaka kwa msaada wako..kama kuna kingine cha zaidi tuendelee kufahamishana mkuu..
 
georgeallen, umeeleza vema mkuu!

Nami nilitaka kumpa maelezo kama hayo!

Kuhusu bank jaribu pia kwenda bank nyengine kama Ecobank, Equity Bank na ABC Banc kujua tofauti ya interest rate zao!
 
Last edited by a moderator:
Nenda kwenye mabenk yasiyokuwa na majina haya makubwa yanazingua ndugu yangu kwa kukusaidia kuna aina mbili za mkopo kwenye mabenki 1>scheme loan na 2>personal loan
scheme loan mara nyingi kampuni yako wananegotiate interest na miaka ya kurudisha lakin personal kampuni yako haijiusishi kwenye negotiation ila wewe ndio utaridhia personal loan interest yake ni kubwa sana
~Bot wameshauri makato yasizidi 50% ya net salary kwhyo kila bank wameweka dsr yao yani debit service ratio na amount ya loan utayochukua kwa mshaara wako haizidi mil 6 kwa sheria za bot na makato kwa mshaara wako yasizidi 40%
 
georgeallen, umeeleza vema mkuu!

Nami nilitaka kumpa maelezo kama hayo!

Kuhusu bank jaribu pia kwenda bank nyengine kama Ecobank, Equity Bank na ABC Banc kujua tofauti ya interest rate zao!

tanx so much brother..
 

na mimi nimenufaika na huu mchanganuo wako
 
Mi najuta nilikopa nmb5m nakatwa162pm 4yrs ntawarudishia7.7m riba ni zaidi ya50% wanachit hata gharama za mkopo. sory
 
Mi najuta nilikopa nmb5m nakatwa140pm 4yrs ntawarudishia7.5m riba50% wanachit hata gharama za mkopo.
Mkuu mbona ukizidisha hiyo 140,000 mara miezi 48 ambayo ni miaka 4 haifiki 7.5M inakuwa 6,720,000
 
Sory ni typing era. Nmb hawakupi mkataba ukausoma wanakusainisha harakaharaka na inshurenc wanaghiribu.sina ham nao
 

Kuna wanaosema NMB ni nzuri kwa watumishi(hasa wa serikali)wanaohitaji mkopo midogo midogo lakini wanasema kuna kauhuni fulani kanafanyika ambapo ukiomba mkopo wa let's say,10,000,000/- kuna makato kadhaa yanafanyika hadi unaweza kuta unapokea chini ya 9,000,000/-.Lakini kwa uzoefu nimekuwa nikiona watu wanalalamika sana juu.

Sasa maswali yangu ni haya"

1. Kwa sasa ni benki gani yenye interest reasonable?
2. Haya makato wanayokata ni ya nini na yana faida gani kwa mkopaji?
3. Suppose nimekopa kwa mkataba wa kurejesha kwa miaka 3,je ikiwa baada ya miaka 2 nitaamua kuja kufuta lile deni watakubali?

Mimi pia nilikuwa na mpango wa kukopa NMB(kwa sababu mshara wangu unapitia humo) ila nimekuwa nasita sana kutokana na yale ninayoona kwa wenzangu waliokopa huko.
 

Loan processing fee: 1.5%ya mkopo; Loan insurance fee: 1-1.5% ya mkopo; Electronic Loan transfer fee-if issuing bank and receiving bank are different (optional): 10,000.00.
 
Loan processing fee: 1.5%ya mkopo; Loan insurance fee: 1-1.5% ya mkopo; Electronic Loan transfer fee-if issuing bank and receiving bank are different (optional): 10,000.00.

Hapo ndipo nasikia mwili kusisimka ndugu yangu.
Loan processing ya nini tena wakati kuna riba riba nalipia,na hiyo insurance ya nini,kwani inarudishwa ikiwa nitarudisha kiasi chote cha mkopo?

Na vipi swali la 3,unaweza kunisaida ufafanuzi mkuu? Mshahara wangu (take home) ni laki 8 na visenti senti je kwa NMB na wezapata max mkopo wa tsh ngapi mkuu?

Samahani lakini kwa maswali mengi ndugu yangu.
 
Wana JF mliomjibu mdau mmefanya vizuri sana.
Hongereni sana tuifanye JF kuwa mahali pa kupata misaada kama hio.Kisima cha maarifa.Pale ambapo great thinkers mnagawa kidogo kwa wengine.
Nimependa sana aliyesema tuachane na mabenki makubwa tujaribu hizi benki mpya ndogo ndogo
Nimefaidika pia sana.

Asanten wote hata unayesoma hii meseji.
 
Muhimu zaidi unapoenda kukopa bank hasahasa personal loan uliza interest wanai-calculate au accumulate how? Mfano. Nmb wanatumia straight line methodi ambayo mteja atachajiwa kiasi sawa toka mwanzo wa mkopo hadi mwisho wa mkopo. Ukikopa 10m, ukalipa interest ya tzs 190,000. So deni litapungua kwa hizo hela, kwahiyo interest inatakiwa iwe pungufu ya ile ya mwanzo, lakini kwa njia hii ya straight line, hata kama utalipa na kubakiwa na deni la laki moja, bado utailipia ile m10 ya mwanzo tofauti na crdb ambao wanatumia reducing balance yaani unalipia unachodaiwa tu.
Muhimu soma mkataba kabla hujausign.
 
Mkuu hapo kwenye red ungefafanua umefaidika kivipi na hizo banki ndogo ndogo walau tupate somo zaidi
 
Provide the following data: unataka kukopa kiasi gani (Loan amount) na kwa muda gani (Loan period in years)? Nafikiri Annual Interest rate ya NMB ni 20%. Kwa Kwa haraka haraka, unaweza kukopa 10,000,000.00 kwa miaka mitano
 
Provide the following data: unataka kukopa kiasi gani (Loan amount) na kwa muda gani (Loan period in years)? Nafikiri Annual Interest rate ya NMB ni 20%. Kwa Kwa haraka haraka, unaweza kukopa 10,000,000.00 kwa miaka mitano

Nilikuwa na wazo la kukopa 10,000,000 ila sipendi kukaa muda mrefu nikidaiwa.Nilifikiria ni rudishe kwa angalau 3
 
Nilikuwa na wazo la kukopa 10,000,000 ila sipendi kukaa muda mrefu nikidaiwa.Nilifikiria ni rudishe kwa angalau 3
Kwa 10,000,000 kwa miaka mitatu at 20% interest rate utakatwa Tshs 371,635. 83 kila mwezi. Total interest kwa miaka yote tatu ni:3,378,890.01. [TABLE="width: 74"]
[TR]
[TD="class: xl65, width: 98, bgcolor: white"][/TD]
[/TR]
[/TABLE]
 
Kwa 10,000,000 kwa miaka mitatu at 20% interest rate utakatwa Tshs 371,635. 83 kila mwezi. Total interest kwa miaka yote tatu ni:3,378,890.01. [TABLE="width: 74"]
[TR]
[TD="class: xl65, width: 98, bgcolor: white"][/TD]
[/TR]
[/TABLE]

Nashuru kwa maelezo mkuu.
Vipi kuna benki gani nyingine yenye angalau interest ndogo (<20%)?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…