Kwa mazingira ya kawaida huo muda wa siku tano ulizozitaja ni mrefu sana mtoto kutocheza kwa jinsi ninavyofahamu.., ukichukulia ukubwa wa mimba..!!)))
Huyo aliyempima na kukuta mapigo yapo chini sana na kumruhusu arudi nyumbani bila kumlaza kwa uchunguzi zaidi sijajua alikuwa na sababu zipi zaidi kufikia uamuzi huo...!!!)))
Sababu zipo nyingi sana zinazoweza pelekea mtoto kutocheza.., nyingi si nzuri ukiondoa ile ya kwamba mtoto anaweza kuwa amelala(Ila si siku tano mfululizo.., watoto huwa wanalala mda mrefu zaidi kuliko mda wanaokuwa macho.., ie zaidi ya masaa 16 ila ni ndani ya mzunguko wa masaa 24).
Kama mimba ni ya kwanza kwa wengine inaweza kuwa ngumu kusikia mtoto akicheza hasahasa ikiwa mtoto anacheza usiku(ie mama akiwa amelala)..!!)))
USHAURI
Aende clinic inayoeleweka aombe kuonana na daktari bingwa wa magonjwa ya kina mama(ie OBSTETRIC GYNAECOLOGIST) kwa msaada wa kitaalam...!!!)))