Msaada kuhusu Silent Ocean (simba wa bahari)

sijaelewa

Senior Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
101
Reaction score
56
Wana JF.

Najua naweza pata msaada hapa. Naomba kwa mwenye uelewa wa namna hawa Silent Ocean wanavyofanya kazi.

Je, wanaweza kunisafirishia mzigo kutoka China bila mimi kwenda huko?

Asante wote mtakao nisaidia katika hili.
 
Wana JF.

Najua naweza pata msaada hapa. Naomba kwa mwenye uelewa wa namna hawa Silent Ocean wanavyofanya kazi.

Je, wanaweza kunisafirishia mzigo kutoka China bila mimi kwenda huko?

Asante wote mtakao nisaidia katika hili.
Mkuu mim nafikiri unatakiwa kwenda china walau mara moja au mbili ukishawajua "supplier" wako hapo ndio inakuwa rahis hata kuwapigia na kufanya order na kuelekeza wapeleke mzigo wako kwa hao silent ocean kwa ajili ya kusafirisha.

Wengine huwa wanawatumia vijana wa hayo makampuni ya usafirishaji kama hao silent na nyinginezo lakin ni risk, chukulia unaishi songea unamtuma ntu alieko Dar akununulie mzigo Dar akutumie kuna changamoto zake ikiwa ni pamoja na kuchagua kama ni vitu vya kuchagua na bei pia.
 
Comment ya kwanza tu inatosha kukukatisha Tamaaa
 
Ndiyo inawezekana..unachotakiwa ni kuwapa address za supplier wako .
 
Inawezekana!

Unalipia Mzigo kwa Supplier wako, then unawapata Details hiyo Shipping Company, wanaenda kagua mzigo wako, wanatoa charge zao, unalipia, wanachukua mzigo toka kwa Supplier au Kiwandani, wanasafirisha, iwe kwa Meli au Ndege!

Binafsi Sijawahi kufanya kazi na hii Kampuni, ila mara ya kwanza niliisikia Kariakoo, kuna jamaa zangu Huwa wanaagiza Simu na vitu ingine, Wanatumia Kampuni hii....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…