Msaada kuhusu ununuzi wa nyumba hii

Msaada kuhusu ununuzi wa nyumba hii

vamda

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2012
Posts
895
Reaction score
571
Salamu wana JF. Kuna mtu ameniomba msaada wa ushauri, nimeshindwa kumshauri maana mambo ya sheria sijui. Rafiki yake anataka kumuuzia nyumba iliyojengwa kwenye eneo ambalo bado halijapimwa. Karatasi ya ununuzi wa eneo hilo iliandikwa bila kushirikisha serikali ya kijiji, yaani iliandikwa kienyeji ingawa kulikuwa na mashahidi. Je afanyeje ili aweze kuinunua nyumba hiyo kihalali ili siku za usoni asipate matatizo? Msaada wa kisheria tafadhali.
 
Kwa kawaida mauziano ya mali zisizo hamishika ni vizuri yakahusisha mamlaka za eneo husika mfano, mwenyekiti wa mtaa nk, lengo kuu ni kujihakikishia kuwa mali inayouzwa na anayeuza anatambulika, lakini kwa kua hilo halikufanyika maana yakae nikua ardhi hiyo haina security ya kutosha, nashauri kabala ya hatua yoyote pateni mtaalamu wa ramani(land surveyor) ili achukue coordinate za eneo husika kujua serikali imelipanga kwa matumizi gani maana kuna cases nyingi unauziwa eneo halijapimwa baadae unaambiwa nusu nzima imeangukia barabarani, endapo eneo litabainika kuwa Katika mpango sahihi sasa mnaweza kufanya mauziano kwa kushirikisha viongozi wa serikali za mtaa husika, ni kawaida hua wanachaji vi pesa kidogo but kw ajili ya security ni vema ufanye hivyo.
 
Back
Top Bottom