Msaada kuhusu Voda Bima

Msaada kuhusu Voda Bima

vvti engine

Senior Member
Joined
Nov 15, 2018
Posts
188
Reaction score
209
Heshima kwenu Wana jukwaa. Kama mada ilivyo, nilipigiwa simu na kitengo Cha huduma kwa wateja Cha Vodabima, wakidai nimekidhi vigezo vyote vya kujiunga na huduma yao ya Vodacom Bima. Maelezo Ni kuwa kwa idadi ya watoto wangu pamoja na mtegemezi mmoja ninatakiwa kulipia huduma hii TSHS. 7,500/= kwa Kila mwezi.

Nikaambiwa kwa kiasi hicho nitapata AINA tatu za bima. (1) Bima ya ajali (2)Bima ya afya au matibabu na Bima ya Maisha. Walinipa maelezo mengi tu Kuhusu michanganuo ya hizo Bima pamoja na mengine mengi. Ninachoomba kufahamishwa hapa Ni ufanisi wa hizi Bima.

Je, kuna mtu yeyote anaye au aliyewahi kuitumia Bima hii ya Vodacom? Vipi Kuhusu utendaji wake na changamoto? Maana wanasema ukitibiwa unatoa pesa yako halafu wao watakurudishia baada ya kuwatumia vielelezo, je Ni kweli wanafanya hivyo? Naomba kuwasilisha.
 
Mimi pia walinipigia na maelezo kama kama hayo,ila sina hakika kama kuna mtu alishapata huduma kama walivo eleza ,
 
Kuna hadi za Tigo,lakini kwa uzoefu ni bora ukakata bima moja tu ya Taifa.
Haya mengine unapoteza muda na hata kutafuta ugomvi na makampuni!

Kumbuka hakuna anayekuonea huruma ktk ulimwengu wa utafutaji,so ukisikia fursa/huduma inajitembeza makinika!
 
Kuna moja ilikuwa ya tigo bima, maelezo yao nikama haya ,ila mteja wao alisumbuka sana, siku ukihitaji uwajibikaji wao ndo shida inaanzia hapo mara peleka risiti za matibabu ofisini kwao, mara nomber wakupayo haipo kwa hewa
 
Heshima kwenu Wana jukwaa. Kama mada ilivyo, nilipigiwa simu na kitengo Cha huduma kwa wateja Cha Vodabima, wakidai nimekidhi vigezo vyote vya kujiunga na huduma yao ya Vodacom Bima. Maelezo Ni kuwa kwa idadi ya watoto wangu pamoja na mtegemezi mmoja ninatakiwa kulipia huduma hii TSHS. 7,500/= kwa Kila mwezi.

Nikaambiwa kwa kiasi hicho nitapata AINA tatu za bima. (1) Bima ya ajali (2)Bima ya afya au matibabu na Bima ya Maisha. Walinipa maelezo mengi tu Kuhusu michanganuo ya hizo Bima pamoja na mengine mengi. Ninachoomba kufahamishwa hapa Ni ufanisi wa hizi Bima.

Je, kuna mtu yeyote anaye au aliyewahi kuitumia Bima hii ya Vodacom? Vipi Kuhusu utendaji wake na changamoto? Maana wanasema ukitibiwa unatoa pesa yako halafu wao watakurudishia baada ya kuwatumia vielelezo, je Ni kweli wanafanya hivyo? Naomba kuwasilisha.
Tatizo bima ni biashara kama zilivo zingine, vitu wanavyofidia ni vile ambavyo wana uhakika vitakutokea kwa nadra sana, so nashauri kama unahitaji bima ya afya kata ya uhakika kutoka kwene taasisi zinazotambulika na vituo vya afya ili ikitokea umepata shida ya kiafya unakuwa huwazi kuhusu hela.

Bima kwa lugha rahisi inakusaidia unapokuwa na dharula na labda kiuchumi hujawa poa, sasa iyo ya kujilipia then uje ufidiwe inaweza isiwe na mantiki kivile... ila the choice is yours
 
Tatizo bima ni biashara kama zilivo zingine, vitu wanavyofidia ni vile ambavyo wana uhakika vitakutokea kwa nadra sana, so nashauri kama unahitaji bima ya afya kata ya uhakika kutoka kwene taasisi zinazotambulika na vituo vya afya ili ikitokea umepata shida ya kiafya unakuwa huwazi kuhusu hela.

Bima kwa lugha rahisi inakusaidia unapokuwa na dharula na labda kiuchumi hujawa poa, sasa iyo ya kujilipia then uje ufidiwe inaweza isiwe na mantiki kivile... ila the choice is yours
Natazingatia ushauri huu. Asante Sana.
 
Kuna moja ilikuwa ya tigo bima, maelezo yao nikama haya ,ila mteja wao alisumbuka sana, siku ukihitaji uwajibikaji wao ndo shida inaanzia hapo mara peleka risiti za matibabu ofisini kwao, mara nomber wakupayo haipo kwa hewa,

Sent from my SM-S920L using JamiiForums mobile app
Asante mkuu. Unapolipia bima, Imani Ni kuwa itakusaidia unapopata tatizo wakati huna pesa wakati huo. Sasa Kama ukipata tatizo ulipe pesa zako halafu wao ndio wakurudishie msaada wao Ni upi?.
 
Tatizo bima ni biashara kama zilivo zingine, vitu wanavyofidia ni vile ambavyo wana uhakika vitakutokea kwa nadra sana, so nashauri kama unahitaji bima ya afya kata ya uhakika kutoka kwene taasisi zinazotambulika na vituo vya afya ili ikitokea umepata shida ya kiafya unakuwa huwazi kuhusu hela.

Bima kwa lugha rahisi inakusaidia unapokuwa na dharula na labda kiuchumi hujawa poa, sasa iyo ya kujilipia then uje ufidiwe inaweza isiwe na mantiki kivile... ila the choice is yours
Ni kweli mkuu. Nitazingatia ushauri wako.
 
Kabda ya kununua bima zingatia Haya yafuatayo............

1. Hakikisha ni kweli unahitaji bima na itaendana na janga ambalo likitokea na hutoweza kulimudu kifedha. mfano matatizo ya afya, janga la wizi, moto au hasara ya kupoteza fedha katika biashara yako.

2. Angalia gharama ya bima kama utaweza kuzimudu na kwa muda mrefu hata kama malipo ni kwa kila mwezi.

3. Zingatia fidia utakayoipata kama itaendana na majanga utakayo yapata. mfano mkataba wa bima unasema fidia itakua ni 10 milioni endapo likitokea janga la moto katika biashara yako, je ukiangalia katika biashara yako janga la moto likitokea fidia ya 10 millioni itakidhi?

4. Zingatia mashari ya mtakaba wa bima na unaeleza nini endapo janga likitokea , utahisika vipi katika hatua za mwanzo na ni viambatanishi vipi vinajitajika katika kuwasilisha madai ya bima.

5. Zingatia ni kampuni ipi ya bima inatoa bima unayohitaji. hapa utaangalia ubora na uhakika wa kupata huduma haraka endapo majanga yakitokea.

6. Zingalia kuchagua wakala (agent) au dalali (Broker) wa bima ambae ni bora katika kutoa huduma za kibima kuanzia mwazo wa mauzo ya bima hadi pale janga likitokea.


Mwishio, bima ni ni mkataba wa ahadi kwa maana ya kwamba kampuni ya bima inakuahidi kukupa fidia endapo janga fulani likitokea na inakutaka wewe kulipa kiasi kidogo cha fedha kwa kipindi hicho cha makubalianio. Katika makubaliano anaweza kuwepo dalali wa bima au wakala ambaye atasimamia katika hatua za manunuzi ya bima na endapo janga husika likitokea.

Kwa Msaada na ushauri wa madai ya bima wasiliana na mimi kupitia number +255 765 827 355
 
Hakuna madai hapa boss, tulikuwa tukijadili habari za vodabima na ufanisi wake tu. Suala la bima mpaka wakili au dalali hili ndio tatizo.
 
Back
Top Bottom