Msaada kujua gharama ya kufyatua tofali 4,800

Pamoja ni michango bora ya wahusika naongeza haya.

Utapata tofali bora na imara ukilinganisha na za kununua. Wafanyabiashara wanatoa hadi tofali 60 kwa mfuko na wewe utatoa 45.

Angalia sana usimamizi wakati wa kufyatua mafundi wataiba cement hadi utachanganyikiwa na kukosa ubora na unafuu uliokusudia.

Hakikisha umwagiliaji mzuri ili kuzifanya imara zaidi.

Ni hayo tu.
 

Ita fundi, tafuta bei ya materials, bei ya mashine kununua au kukodi, vibao pia; take a pen and a paper Piga hesabu!

Mie sijui maswali mengine mnaulizaga mnakuwa na malengo gani!
 
Tofali 45 kwa mfuko? Si mchanga mtupu tu huo jamani....
Tofali 19 kwa mfuko!!! Ndio dili.

Watu mnabwabwaja tu ili muonekane wazee wa viwango, ni aidha mnaishi kwa shemeji hamjui kitu au lengo lenu ni kukatisha tamaa wenzenu!

Mfuko tofali 19!!!!

Mara tofali 25!!!

We unafikiri hiyo tofali ungeuziwa 1000-1200? Mpigaji angefanya biashara kichaa namna hiyo!

Tofali zote unazoona zinauzwa mtaani huko ni wastani wa zaidi ya 40 na kila siku unaona zinaondoka na maghorofa yanainuka... jipe muda kuwauliza wapigaji japo wanaweza wasikwambie ukweli.

Huu mjadala wa ujenzi upo juu ya uwezo wenu hivyo mlipaswa kuuamkia na kukaa kwa kutulia.

Mfuko wa simenti kwa tofali za ujenzi wa nyumba, 32.5R au 42.5R inatoa tofali 40-50 tena ni zenye ubora wa kiwango cha juu.

Na huyu ni mpigaji wa mikono, kwa mashine zinaweza kuzidi hapo na zikafaa tu.

Acheni ubishani na mizaha, hii ni moja ya sababu mnaogopa kujenga.
 
Asante
 
19? Hapa utakuwa umezidisha sana mbwembwe. 30 - 35 kwa mfuko, kama unafyatua mwenyewe ni ratio nzuri tu, wanazouza huko mtaani wanapiga 50 kwa mfuko.

Huu ndo ukweli, nilifyatua tofali zangu 40 kwa mfuko na zilikuwa juu ya kiwango.... za mtaani zote ni 50 na zinatumika kila siku hatuoni hiki wanachoita kupukutika.

Hayo ni mawazo ya mtu asiyewahi kujenga na ndiyo chanzo cha kujipa hofu.
 
Babu.......tofali 45 kwa mfuko.... Mmmmmmmmhmn zitakuwa imara hizo tofali?!
Zinakuwa imara sana, kikubwa fundi apige vizuri kwa kushindilia, aweke cement ya kutosha na kumwagilia vyema
 
Tofali 45 kwa mfuko? Si mchanga mtupu tu huo jamani....
Tofali 19 kwa mfuko!!! Ndio dili.
Acheni maigizo yenu, siyo kila uzi ni wa kuchangia! Nyuzi nyingine zinawazidi uwezo, nendeni kule Jukwaa la Mapenzi au Chitchat. Hapa waachieni watu serious wanaojua nini kinatakiwa kifanyike.

Majukwaa ya Skills kama haya inabidi siku za usoni Mods waweke limitations maana siyo kila mtu anaweza kuchangia, wengine muwe wasomaji tu
 
Umeandika uzi mrefu usiokuwa na faida. Kwa taarifa yako unaweza kufyatua tofali hata 20 kwa mfuko na zisiwe imara kama fundi hatozingatia ratio nzuri ya cement, compaction na umwagiliaji mzuri. Fundi mwingine anaweza kufyatua mpaka tofali 45 na zaidi zikawa imara kwa kuzingatia hayo mambo muhimu matatu
 
Ni shida kweli, kwa vile tu wamepewa uhuru wa kutoa comment basi kila mtu anaamua kusema chochote apendacho hata bila kuwa na uhalisia
 
Utaokoa takribani milioni mbili, kulinganisha na kununua zilizo tayari.

Huwezi okoa milion mbili kwa idadi ya hizo tofali!
Hebu toa mchanganuo tuone hiyo milion mbili inaokolewaje!
 
Upo wapi mkuu?


Kila mfuko mmoja wa cement toa tofali 45.


Mchanga utahitaji wastani wa lorry 18 za ujazo wa 4.7mm3.


Gharama ya kufyatua mfuko mmoja wa cement ina range 5000-7000

Kwa ushauri zaidi nicheki PM
Babu.......tofali 45 kwa mfuko.... Mmmmmmmmhmn zitakuwa imara hizo tofali?!
Tofali 45 kwa mfuko? Si mchanga mtupu tu huo jamani....
Tofali 19 kwa mfuko!!! Ndio dili.
Naona kila mtu kaserereka kwa jinsi anavyoweza.

Ila kitaalamu na kwa kufwata hii document hapa chini tofali 45 au 60 kwa mfuko mmoja wa cement inatia shaka kama kweli unajali ubora.View attachment BROCHURES-FOR-BLOCK-MAKING (1).pdf


NB: Naona attachment inasumbua, isipofunguka google "1 cement bag blocks simba cement" utaletewa link za simbacement fungua ujisomee.

Fungua link ya kwanza.


View attachment 1637341
 
Ok nitaicheck
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…