Msaada kuku anaumwa

mandwa

JF-Expert Member
Joined
Aug 13, 2013
Posts
1,493
Reaction score
361
Habari jamani;

Naomba msaada wa haraka kuku wangu jogoo wa Malawi anaumwa mafua hadi namuonea huruma yamembana kiasi cha kukoroma na kuziba mdomo, sijampatia dawa yeyote naomba mnisaidie aina ya dawa nzuri na bei yake.

Naomba mnisaidie maana nimemnunua ili nipate mbegu akifa nitaumia sana.

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Nenda kwenye duka lolote la madawa ya mifugo na mweleze doctor wa mifugo .atakupatia dawa.bei ni kama 10000.but ukichelewa utampoteza kuku wako
 
Nenda kwenye duka lolote la madawa ya mifugo na mweleze doctor wa mifugo .atakupatia dawa.bei ni kama 10000.but ukichelewa utampoteza kuku wako

Asante mkuu nitafanya hivyo

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Anaweza kuwa amemeza mdudu fulani yuko kama chura (sijui jina lake halisi) mdudu huyu haozi haraka na humsababishia kuku kuwashwa kooni kwa sababu ya sumu yake.

Mara nyingi kuku hukohoa ama kukoroma kama binadamu hasa nyakati za usiku.

Koroga chumvi iwe kali kiasi, mnyweshe. Hii husaidia huyo mdudu kuoza haraka. Fanya hivyo hivyo kila jioni kwa siku tatu.

Waweza pia kufuata ushauri wa kumuona daktari wa mifugo kama ulivyoshauriwa, iwapo kuku wako anaugua mafua ya kawaida.
 

Poa mkuu yaani nilikua sijui kama kuku anaweza akaumwa mafua ya kiasi hiki anakoroma kama binadamu na yametanda mdomoni hadi nauzunika maana nampenda huyu jogoo wa Malawi mkubwa sipendi nimpoteze nitajaribu hiyo chumvi maana pesa ya dawa sina kwa sasa mpaka j2 ndiyo nitapata pesa

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 

kwa hiyo stage aliyo fikia ukimchelewesha tu anaondoka within a few hours.
 
Eti Jogoo wa Malawi unampenda, kisha unamuacha ajitafutie chakula mwenyewe mitaani mpaka anakula wadudu wa Sumu?!
Umevamia fani Eeeeeh!!
 

Mafua ya kuku ni hatari. Kama huna hela kwa sasa chukua kidonge cha tetracycline kipasue changanya kwenye maji umnyweshe haraka. kwa vile ni ugonjwa wa kuambukiza unaweza kuwapa kwenye maji na kuku wengine ili wasishambuliwe mpaka hiyo jumapili utapopata hela ya chanjo.
 

Asante kwa ushauri mzuri

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…