Hujakosea ndugu yangu yoote nimeafiki ila tatizo linalokuja hata kutoa hiyo elimu kuna taabu nyingi,uelewa wa watu unatofautiana na wengi wa wenye kuelewa haraka hawapo ktk nafasi muhimu za kuweza badili njia.Sasa waliobaki ni wale walioktk tabaka la walionazo na walio na influence.
Hatuna ujanja hapa tunatakiwa kulijua soko kwa haraka sana, haraka inayozidi hii haraka ya ubadilikaji wa mambo ili tuweze kuikuta dunia na kuanza kwenda nayo. Na pia hatutoweza fika kwa pamoja nchi nzima na wengine hatutofika kabisa.
Ndio maana ninasema elimu sahihi na kuachia time iamue tutakuwa wapi.Tutakuwa uchochoro wa wenzetu kwa kipindi kwani hatuna ujanja. Cha msingi ni kujaribu punguza madhara ya kupokonywa vyote kabla hatujazibuka. Yaani hata hao vipofu wakitupwa mjini wengi kama watafuata njia tofauti ipo chance baadhi wakapona pengine wataanguka ktk rescue team, wengine wataanguka mashimoni wengine watagongwa, etc.
Hapa kidogo nataka elezea kidogo concept ya adapatability na evolution kwa maan isiyo ya kibayojoa sana. Yaani wapo watakaojifunza mazingira na kuweza jua watakavyojibadili na kuweza yatumia kwa faida ya upande wao. Ila bado hatutafika pamoja na mwishowe tutakuwa na ugonjwa mwingine wa kutibu yaani kuwa na watu wachache walioshikilia uchumi uliokuwa km ilivyo kwa nchi km India, South Africa etc. Si muda mrefu utakuta watu chini ya 10% wakishikilia 99.999% ya uchumi wa nchi inayoweza itwa imepiga hatua. Pengine tutakuwa tumerusha rocket anga za juu, tunauza bidhaa na elimu, tuna neuclear na mengine wanayoweza angalia nayo nguvu ya taifa. Ila yote yakabaki kwa vigogo.
Bado ni bora hata hao wachache waokoe kila kitu then baadaye tuanze fanya mabadiliko ya ndani km dilution ili kupata mchanganyiko safi na baadaye kuweza poteza hii sumu ya ujinga.