Nyenyere
JF-Expert Member
- Sep 9, 2010
- 14,804
- 10,715
Wakuu, nimetakiwa kumsimamia mama mjane juu ya haki zake. Mama huyu aliolewa mwaka 1997 huko Mpanda na mume aliyekuwa na watoto wanne wakubwa. Baada ya mwaka mmoja mume aliyekuwa mfanyakazi alipewa redundance.
Wakaamua kuhamia DSM. Alitangulia mwanamume akatafuta nyumba ya kupanga. Wakati huo walikuwa na mtoto mdogo ambaye alifariki baadaye. Mume alimfuata mke wakaja kuishi DSM ambapo walizaa mtoto mmoja aliye sekondari hata sasa.
Mume alipata kazi ya korokoroni aliyokuwa akiendelea nayo hadi mauti ilipomkuta.
Wakiwa DSM walifanikiwa kujenga nyumba huko mbagala ambapo walikuwa wakiishi hadi mauti yalipomfika mume. Kazi ya mwanamke ni mganga wa tiba za asili.
Shida ni kuwa watoto wale wa mama wa kwanza pamoja na shehe (mume alikuwa mwislamu) wanadai kuwa nyumba waliyoijenga ni mali ya watoto pamoja na vitu vingine vyote. Huyu mama wanasema akabidhiwe kwa ndugu zake wao wauze nyumba watoto wagawane pesa. Wanasema huyu mama akaolewe tena huko kwao ilhali kajijengea nyumba na mumewe ili waishi hati mpaka mauti yawafike.
1. Je, sheria ya kiislamu inasemaje juu ya hili? Huyu mama aliyetumia muda na nguvu zake kujijenga na mumewe ni sahihi afukuzwe hapo?
2. Sheria za nchi zikoje katika hili? Mwanamke keshanyang'wa hati za nyumba na watoto, ingawa anao ushahidi tosha kuwa hiyo nyumba kaijenga na mumewe.
3. Leo ndio kuna kikao cha ukoo cha maamuzi, nahitaji msaada wa haraka katika hili.
MziziMkavu, @hofsfede nsajigwar Mtambuzi, Bikra figganigga VoiceOfReason gscan, Mwangaruka
Wakaamua kuhamia DSM. Alitangulia mwanamume akatafuta nyumba ya kupanga. Wakati huo walikuwa na mtoto mdogo ambaye alifariki baadaye. Mume alimfuata mke wakaja kuishi DSM ambapo walizaa mtoto mmoja aliye sekondari hata sasa.
Mume alipata kazi ya korokoroni aliyokuwa akiendelea nayo hadi mauti ilipomkuta.
Wakiwa DSM walifanikiwa kujenga nyumba huko mbagala ambapo walikuwa wakiishi hadi mauti yalipomfika mume. Kazi ya mwanamke ni mganga wa tiba za asili.
Shida ni kuwa watoto wale wa mama wa kwanza pamoja na shehe (mume alikuwa mwislamu) wanadai kuwa nyumba waliyoijenga ni mali ya watoto pamoja na vitu vingine vyote. Huyu mama wanasema akabidhiwe kwa ndugu zake wao wauze nyumba watoto wagawane pesa. Wanasema huyu mama akaolewe tena huko kwao ilhali kajijengea nyumba na mumewe ili waishi hati mpaka mauti yawafike.
1. Je, sheria ya kiislamu inasemaje juu ya hili? Huyu mama aliyetumia muda na nguvu zake kujijenga na mumewe ni sahihi afukuzwe hapo?
2. Sheria za nchi zikoje katika hili? Mwanamke keshanyang'wa hati za nyumba na watoto, ingawa anao ushahidi tosha kuwa hiyo nyumba kaijenga na mumewe.
3. Leo ndio kuna kikao cha ukoo cha maamuzi, nahitaji msaada wa haraka katika hili.
MziziMkavu, @hofsfede nsajigwar Mtambuzi, Bikra figganigga VoiceOfReason gscan, Mwangaruka
Last edited by a moderator: