Fidel80
JF-Expert Member
- May 3, 2008
- 21,947
- 4,470
Hamjambo wapendwa, hope wote mmeamka bien, kwa wagonjwa na matatizo mbalimbali poleni. Leo nimepata kisa kimenitatiza kidogo naomba kushare nanyi wapendwa tumsaidie huyu ndugu. Huyu mkaka amezaa na mke wa mtu bila mume kujua na wote wanaendelea kumtunza mtoto sasa ana umri wa miaka mitano. Tatizo mdada anaogopa kusema ukweli kulinda ndoa yake, na mkaka (mwizi) anataka atambulike kwa mwanae japo na yeye ana mke.Mke wa mwizi keshaelezwa kuna mtoto nje kakubaliana na hilo japo hajui ni wapi/ kwa nani. Na familia ya mdada inajua kila kitu.Familia ya kiume na mke wa mwizi imekomaa inataka kumuona huyo mtoto. Mume wa dada hana ajualo. Nisaidieni kaka aanzie wapi, na familia ya mkaka mwizi na mdada ni marafiki toka udogoni..
Nawasilisha.
Mwambie kama anataka mwanawe ajue kuwa huyo anae ishi nae sio baba akubali kuutwika mzigo atakapo pigwa talaka.
Akubali kabisa pasipo kipingamizi dili likitibuka amtafutie hifadhi kabisa.
Ila wanawake huwa mnakuwa na akili za ajabu sana wewe mke wa mtu unalitamani janaume la mtu unalikabidhi roho na mapafu linakuzalisha na wewe unakubali kwa kuneng'eneka ukijua lijamaa linakupenda subiri utangwe talaka hapo utajua sura za wanaume zilivyo na utajua kuwa sura sio roho. Litakufungia vioo kama halikujui vile.