Msaada kwa mwenye uzoefu na M-PESA,Tigo pesa na Airtel money.

nemnunu

Member
Joined
Jun 4, 2019
Posts
74
Reaction score
64
Habari
Kama kichwa kinavojieleza, nahitaji kuanzisha huduma ya kifedha ila sina uzoefu wowote, sina lesen wala tin number!
Naomba maelekezo nikihtaji hiv vitu nianzie wap, na gharama zake zipoje?
Je kuna madhara yoyote ya kutumia tin yenye jina la mtu?
Mtaji inatakiwa uanze angalau na shngap ili uanze biashara

Samahanin kwa usumbufu
 
Nipo mbeya
Aha Sawa process zake nikama ifuatavyo, unatakiwa uwe na tin number hii inapatikana TRA bure, ukishapata hiyo unaenda manispaa kukata leseni yabiashara nadhani haifiki laki kwamwaka mzima, baada yahapo unapiga copy hiyo tin number naleseni yako yabiashara pamoja nakopi yakitambulisho nautapeleka ofisi ya mtandao husika watakupa form utajaza nautaambatanisha pamoja nahizo kopi zako, hapo kazi yako itakuwa imekwisha zaidi utawaachia mawasiliano kwaajili yakuku taarifu line zako zikiwa tayari. Kuna baadhi ya mitandao watahitaji napasport size yako moja au mbili utawapatia nadhani nitigo.

Kuhusu kutumia nakala zamtu mwingine sio shida ili mradi makubaliano yenu naananakuwa ninani yako, akikuamini, ukimuamini inakuwa haina tatizo ila kama unaweza nivizuri ukatumia viambata vyako ili hata baadae zikileta shida vitambulisho unakuwa ulitumia vyako mwenyewe so hata kupata msaada inakuwa nivirahisi sana.
 
Asante sana, nimekuelewa vizuri
 
Japo aliyeuliza ni mwingine, mimi pia nimenufaika na maelezo yako mkuu. Kwa uzoefu wako ili uweze endesha biashara yako kwa umakini kwa mitandao yote taja hapo. Ni kiasi gani cha mtaji kinatakiwa kisipungue ?
 
Japo aliyeuliza ni mwingine, mimi pia nimenufaika na maelezo yako mkuu. Kwa uzoefu wako ili uweze endesha biashara yako kwa umakini kwa mitandao yote taja hapo. Ni kiasi gani cha mtaji kinatakiwa kisipungue ?
Wenyewe hawakupangii mtaji kiasi gani uanze nacho ila niwewe mwenyewe ndio utajipangia uanze namtaji kiasi gani. Kwauzuri kabisa kama upo maeneo mazuri basi kisipungue milioni 2 ila milioni 3 itapendeza zaidi
 
Kwanza unatakiwa kuwa na tin namba kutoka TRA na yakulipia sio ya bure, apa utatumia akili kidogo ili wakuchaji pesa kidogo mfano mimi nilienda nikawaambia nimefungua stationary mauzo yangu ni 10000 per day nikawapa nakala ya mkataba wa frem nliopangisha ambayo haikuzid 50,000 kwa mwezi, basi TRA wakanipa form nikaenda kuijaza ikapitia office ya serikali za mtaa nikarudisha nikakadiriwa kodi kama ya 30000 ivi kwa mwaka hatimae nikapewa tin namba ya biashara, next nikaenda halmashauri kufatilia lesen ya biashara, ukienda kwenye halmashaur yako watakwambia nini na nn wanahitaji moja wapo ni iyo tin namba kutoka TRA basi nao ukikamilisha watakufanyia makadirio utalipia baada ya mda kidogo utapewa leseni (ukienda TRA au halmashauri hakikisha umeshajipanga kua biashara gani utaifanya ili kuepuka usumbufu yaan buni ata kwa imagination sio lazima ufungue kwa wakati uo ila vizur zaidi iyo biashara iwe kwenye mipango yako, mfano mm nlibuni tu stationary na saivi nnayo kiukweli lengo la hili ni kupata izo leseni zao tu), ukishapata sasa utaenda office za mitandao unayoka na leseni,tin namba, copy ya kitambulisho, pasport size, kule watakupa form ujaze then watakupa utaratibu mwingine, upande wa voda hawana longo longo wao ni fasta tu na nibure kabisa, ila tigo sasa itategemea na office husika na itachukua mda around 2-5 month. Uo mtiririko kiutendaji ni simple sana ukiwa upo fresh haumalizi ata siku 3, mfano mimi TRA nilimalizana nao kwa siku moja tu.



Ushauri usijaribu kabisa kutumia doc au line iliosajiliwa na mtu mwingine, wakati wa kutumia inakua haina tatizo ila likitokea tatizo lolote ukahitaj msaada wa moja kwa moja kutoka office za mtandao husika utahitajika docmnt zote za usajili na lazima taarifa za iyo line zipelekwe na mhusika nakwambia hivi nikiwa na uzoefu wa kutosha.
 
Mwaka gani mkuu TRA walikukadiria kodi ya 30 Elfu kwa mwaka
 
Mwaka gani mkuu TRA walikukadiria kodi ya 30 Elfu kwa mwaka
Mwaka huu mwanzoni tu mbona nimelipa tsh.36000 apo tawi la shekilango tena uzuri pale na bank ipo pembeni
 
Kwa maana hiyo lesen inatolewa kwa ajil ya biashara nyingne na sio huduma za kifedha moja kwa moja? Lazma uwe na biashara nyingne uliyoplani.
 
Wenyewe hawakupangii mtaji kiasi gani uanze nacho ila niwewe mwenyewe ndio utajipangia uanze namtaji kiasi gani. Kwauzuri kabisa kama upo maeneo mazuri basi kisipungue milioni 2 ila milioni 3 itapendeza zaidi
Mtaji huu ni kwa mitandao yote au mmoja?
 
Kampuni za simu zinahitaji uwe na leseni yoyote halali biashara kutoka sehem mbili, 1. Halmashauri na 2. Tra, sasa wengine tunatumia advantg iyo , kuhusu kukata leseni moja kwa moja ya huduma za fedha kwenye simu kwakweli sijajua
Kwa maana hiyo lesen inatolewa kwa ajil ya biashara nyingne na sio huduma za kifedha moja kwa moja? Lazma uwe na biashara nyingne uliyoplani.
 
Asante ushauri mzuri sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…