Mwendabure
JF-Expert Member
- Mar 10, 2011
- 2,138
- 1,044
Bobby, hapana si beleaf ni hali halisi ya biashara ilivyo. Hata ukienda kukopa kwenye haya mabenki yenye uzoefu wanakuwa na imamni kubwa kumkopesha anaenunua Scania kuliko magari mengine ambayo hayajazoeleka hapa nchini. Hata ukifanya utafiti mdogo wanalipa madeni wengi ni wale wanakopa kununua magari ya Scania. ni ukweli usiopingika kwamba kweli Scania ni ghali kuwekeza lakini resale value iko juu sana. Mfano ukinunua Scania kwa ml 60 baada ya miaka mitano kama unalitunza vizuri utajaliuza kwa ml 40-50! Mungu akupe nini. Taarifa zilizoko ni kwamba Scania Tanzania wana asili mia 80 ya vipuri unavyohitaji! Kwa hivyo uwakilishi wake unaendana na wakakti. Nawasilisha.Babu, nadhani basic economics principle ya demand and supply inaapply hapa, kwamba dealers wa volvo wako wachache kwa kuwa demand ya hizo parts ni chache kwani idadi ya volvo trucks nchini ni ndogo ukilinganisha na idadi ya scania trucks. On the other hand pia huenda hiyo demand kubwa ya parts za scania imesababisha uzalishaji mkubwa counterfeit parts kutoka kwa wale ndugu zetu na hizi mara nyingi huwa bei poa tu hivyo kila mmmoja anaweza.
Sasa kwanini Scania na si volvo? Mimi nadhani ni belief tu, watanzania hawako flexible kihivyo, it takes time wao kujiadjust kwenye mazingira/vitu vipya. Nalinganisha hili na issue ya gear box, manual na automatic. Nakumbuka ilichukua muda sana kwa watanzania kuzikubali automatic gear boxes, ilikuwa ukindesha gari automatic unaonekana ni kituko kabisa lakini sasa hivi hawataki tena manual gear box. Mimi niko kwenye transport pia na mwanzoni mwa mwaka huu nilinunua volvo moja FM 12. Toka nimeinunua hii gari ikitoka safari ni kumwaga oil tu inaondoka tena wakati scania kila zikirudi mambo kibao ya kufanya kabla haijasafiri tena. Anyway, huenda kuna factors nyingi za kuziangalia lakini mm nahamia volvo na Mungu akipenda naongeza nyingine soon.
scania 113-320hp ndio gari kaka zingine uzushi
Bobby, hapana si beleaf ni hali halisi ya biashara ilivyo. Hata ukienda kukopa kwenye haya mabenki yenye uzoefu wanakuwa na imamni kubwa kumkopesha anaenunua Scania kuliko magari mengine ambayo hayajazoeleka hapa nchini. Hata ukifanya utafiti mdogo wanalipa madeni wengi ni wale wanakopa kununua magari ya Scania. ni ukweli usiopingika kwamba kweli Scania ni ghali kuwekeza lakini resale value iko juu sana. Mfano ukinunua Scania kwa ml 60 baada ya miaka mitano kama unalitunza vizuri utajaliuza kwa ml 40-50! Mungu akupe nini. Taarifa zilizoko ni kwamba Scania Tanzania wana asili mia 80 ya vipuri unavyohitaji! Kwa hivyo uwakilishi wake unaendana na wakakti. Nawasilisha.
Mkuu,Mkuu Chesea Ingine, kwanini hayo mabenki unayaondoa kwenye hiyo "belief"?. Wao ni sehemu ya soko na wapo kuwahudumia wateja ambao imani yao ni scania trucks tu na si vinginevyo. Unajua wanaodetermine hali ya sokoni ni wateja na wauzaji (demand & supply) na si vinginevyo kwa hiyo effect ya hiyo hali inacut across kote mkuu including kwenye mabenki. Unasema wanaolipa mikopo wengi ni wale wenye scania huenda sababu ni kuwa wanaonunua scania kwa mkopo ni wengi kuliko wa volvo. Mimi ninahitaji opinion ya kiufundi kwamba Scania ni bora kuliko Scania otherwise kilichopo hapa ni imani na may be ni ulimbukeni tu kama mchangiaji mmoja alivyosema.Nchi zote zilizotuzunguka watu wa scania wana ofisi huko pia lakini hawana scania nyingi kama tulizo nazo sisi. Sitaki kuamini kwamba sisi tunajua kipi kilicho bora kuliko majirani zetu wote.Kuna jamaa wachache ninawafahamu ambao wanajuta kwanini wamepoteza muda wao mwingi kwenye scania bila sababu ya msingi.
...........nimekukubali camaraderie,...........kwa kuunga hoja mkono,tetea kitengo naona umechangamka na tayari uko stand by kwa kupokea order...........duh mchaga utamjua tuuuuuuuuuuu,............................Sio kweli....Scania imekuwepo TANZANIA kwa kitambo sasa. Unakumbuka TAMCO kibaha au ulikuwa bado hujazaliwa? Scania pia ni nzuri kwa utumiaji wa mafuta na efficiency. Model P114 (Pichani) ambazo ni nyingi TZ (Ninazo 8) engine yake ni 12,000CC compared to FUSO ya same efficiency ni 20,000CC...ukitaka kuagiza ni PM