Msaada kwa wafanyabiashara wa mchele

Nkondo 2

Senior Member
Joined
Oct 10, 2016
Posts
181
Reaction score
144
Ndgu wadau nahtaji kufanya biashara ya mchele kuuza kwa bei ya jumla hapa jijini MWANZA, nauliza kwa wenye uzoefu n chimbo gan ambalo naweza kuwa nakusanya mzigo kwa bei nzur ambayo itafanya nkiufikisha mjin niweze kuwa mshindani mzur wa bei katika soko??
 
Huu uzi inabidi tuutumie kwa ajili ya kukusanya taarifa mbali mbali za hii biashara ya mchele, nami nasubiri hapa kupata ujuzi kwa wanaosafiri kwenda IFAKARA, KYELA na kwingineko
 
Labda kwa haraka haraka tu ningeshare kidogo kile kidogo ninachofahamu

Hii biashara mode ya kwanza na nzuri lakini very risky ni kuununua mpunga na kuukoboa kupata huo mchele then ndio uupeleke sokoni

Mode ya pili ambayo ni kuununua mchele kama mchele ina"depend" sana na bei ya mahali unapoununua huo mchele

All in all bei maeneo mengi(siongei tu nimezunguka sana) inarange kutoka 1300 mpaka 1500 kwa kilo
 
Unaweza tueleza risks na faida za kununua mpunga? Na zile za kununua mchele pia?
 
Vipi mkuu kama akienda kununua mpunga shambani kwa wakulima halafu akakoboa mwenyewe kupata mchele atakaoenda kuuza anakotaka?

Kama huna uzoefu ni bora ununue mchele kuliko mpunga, au utafute mtu wa kukusaidia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…