Alvin Slain
JF-Expert Member
- Aug 30, 2011
- 6,375
- 3,663
- Thread starter
-
- #21
Kimsingi tatizo lako ni la kihistoria.
Inawezekana umelelewa na mama wa kambo au walezi/wazazi wakali wenye tabia za kufokea watoto na wasio wapa watoto nafasi ya kujieleza pale wanapokosea.
Jambo hili likakujengea hofo,woga na kutojiamini mpaka hapo ulipofikia.
DAWA/UTATUZI
Anza kwa kutembelea shule ya chekechea imba nao,cheza nao,wape nasaha taratibu ukimaliza makundi ya chekechea unakuja,primary,sekondary,chuo hadi ktk makongamano na warsha.
JISIKIE HURU NAJUA KINACHOKUTESA NI DHANA .
Habari wapendwa!
Hili tatizo la kutetemeka wakati ninapowasiliana na wengine sijui litaisha lini.
Maana ni aibu sana nashindwa kuwasilisha hoja zangu makini sababu ya kutetemeka.
Pumzi zinaisha kabisa na nahisi moto unaniwakia ninapotaka kuongea!!
Yaani nashindwa nifanyeje japokua ni suala muhimu kwangu inabidi nikae kimya ili nisijetetemeka"
Nikiongea naona najichanganya sababu ya kupanic!
Kwa anaemjua Dr yoyote wa Saikolojia mjini Arusha naomba mnisaidie na Ushauri pia.
NB:Moderator Paw Invisible
Msiupeleke huu uzi jukwaa la Doktar.
Habari wapendwa!
Hili tatizo la kutetemeka wakati ninapowasiliana na wengine sijui litaisha lini.
Maana ni aibu sana nashindwa kuwasilisha hoja zangu makini sababu ya kutetemeka.
Pumzi zinaisha kabisa na nahisi moto unaniwakia ninapotaka kuongea!!
Yaani nashindwa nifanyeje japokua ni suala muhimu kwangu inabidi nikae kimya ili nisijetetemeka"
Nikiongea naona najichanganya sababu ya kupanic!
Kwa anaemjua Dr yoyote wa Saikolojia mjini Arusha naomba mnisaidie na Ushauri pia.
NB:Moderator Paw Invisible
Msiupeleke huu uzi jukwaa la Doktar.
Hata ninaposoma hizi post nnakua na hofu utadhani watu wananiona
Punguza pombe
Nadhani ww utakuwa engineer au mwanasayansi maana ndiyo huwa hawajiamini wakiongea mbele za watu
Mimi ni mnywaji sio mlevi
mkuu hilo tatizo linatibika onana na psychologist ungekuwa dsm ungeenda muhimbili session chache tu umepona...
afu pia mkuu you need to orient youself close to people, practise kuongea nao mambo mbali mbali.
anza na marafiki zako wakaribu alafu jichanganye kwenye group za watu hakikisha unaongea mkuu, wewe ni unique hakuna kama ww so jiamini..
asikudanganye mkuu kila mtu hua ana hofu akianza kuongea mbele ya mkusanyiko mwingi wa watu lakini zinatofautiana zile first minutes za kutolarate huo uwogo!!
jiamini jembe ndo key yakutokuogopa!!...afu pia piga prayer sana arif
Mimi ni mnywaji sio mlevi
pole sana mkuu.
Da ndg pole sana una tatizo km langu, mi niko chuoni yaani cku za presentation kwangu huwa ni balaa, nimeshajaribu kuomba ushauri humu jf lkn pamoja na shauri mbalimbali nzuri lkn tatzo bado linanitafuna.
Wkt mwngne hata lecturer akiwa anafndsha ile anapouliza swali akikuangalia tu hofu na kutetemeka kuna tamalaki hata kitu nakifahamu nakuwa na wasiwasi ajabu, na drs langu tuko wachache kiasi kwamba lazma utaongea tu!
Kumbe tupo wengi. Hata mimi nina tatizo hili. Nimekuwa nalo tangu nikiwa shule ya msingi. Nilikuwa bright darasani, lakini ilipokuwa ikifika mwalimu akaninyanyua nisome hata aya moja kwenye kitabu cha kiswahili nilikuwa nashindwa kabisa. Siku moja alikuja mwalimu wa kiswahili mgeni--alihamia shuleni kwetu--akaniambia nisome (tulikuwa tukisoma kwa zamu--kwa wale wanafunzi mliosoma miaka ya 80's mnafhamu hili). Nilishindwa kabisa. Basi siku hiyo aliporejea Staff room, akawauliza walimu inakuwaje mwanafunzi wa drs la sita asijue kusoma. Wakamuambia mimi ndiye genius darasani ila hiyo habari ya kusoma vitabu darasani siiwezi kabisa. Bado hali hiyo ninayo mpaka leo. Kujieleza mbele ya kikundi cha watu 5 au 6 ni shida sana, hasa pale ninapokuwa nimechukua nafasi ya main speaker huku watu wote wakinitazama na kunisikiliza--points zote nilizokuwa nataka kuongea huyeyuka na kijasho jembamba huanza kunitoka.
Mi sipendi kabisa nikiongea mtu aniangalie machoni yaani basi tu !!"""
Pole Apolinary...ila kuna psychologists wengi wanaweza kukusaidia ,labda ufanye utafiti mwenyewe kwenye mtandao utapata nafuu....namfahamu mhindi flani kazini ambaye pia hutetemeka tu kila mara anapo anza kuzungumza.
Alafu hii hali hainiruhusu kujichanganya na wengine naona nitajichanganya!
Amani Usalama hakuna!!!