Msaada matumizi ya till ya mpesa

Orketeemi

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2013
Posts
5,063
Reaction score
12,866
Wakuu habari.
Jana mchana vodacom walinitumia ujumbe huu
MUHIMU!! Ndg wakala, LITE TILL unayotumia itafungwa leo 1/4/2019 na hutaweza kuitumia tena, Ondoa salio lako na commission yako kuepuka usumbufu. Asante.

Walipopigiwa voda walisema ni tatizo la mtandao na kwamba wamewatumia wengi ujumbe huo.

Jion kweli TILL imefungwa.

Kwa wazoefu naomba kujua tatizo hili chanzo chake ni nini? na suluhisho lake inatakiwa nifanye nini?

Wema ni akiba.
 
Kwanini usiwasikiane na voda mkuu

$ There's clear light at the end of the Tannel $
 
Ya kununua kwa mtu mkuu. Afu na mtu huyo naye alinunua mbali

Fuata tu utaratibu wa kusajili line yenye jina lako kwa kufuata sheria na kanuni zilizowekwa. Kutumia line ya uwakala ya mtu mwingine ni kosa kisheria.
 
Vodacome hawatoi laini ya mpesa kwakutumia leseni na tin namba moja kwa laini mbili nadhani hapa ni mpaka ufanye nao maelewano, Till yako kuna mtu kaenda kuomba uwakala kwa nyaraka zilizotumika kuombea hiyo yako hapo lazima laini moja ifungwe ndo mana yako imefungwa, chakufanya mtafute aliyekuuzia amtafute aliyempa hiyo laini muelewane laini yake ifungwe yako ifunguliwe utoe hela yako na utafute uwakala kwa nyaraka zako
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…