Msaada: Maumivu ya Magoti Yaninisumbua!

Msaada: Maumivu ya Magoti Yaninisumbua!

Je, ni dawa gani ningeweza kutumia, ndugu zangu? Msaada wenu unahitajika.
Ni makosa kutafuta dawa pasipo kujua chanzo au kiini kinachopelekea kupata hayo maumivu.

Njia sahihi:
  • Fika hospitali - Acha daktari afanye kazi yake na atakujulisha chamzo au kiini cha tatizo na atakuapa dawa stahiki.
  • Kama kuna dawa zozote umewahi kutumi - Ni vyema ukaweka wazi kwa Daktari husika.
 
Uzito pekee haijitoshelezi.

Huwa ni:
  • Uzito wako
  • Kimo chako
Ndio utapata BMI sahihi.

Yamkini 83kg kwa kimo chako ni uzito sahihi. Hicyo lazima uweke hapa vipimo vyote, uzito na urefu ndio utashauriwa iwapo uzito umezidi au la!

Pole sana kwa hayo maumizvu.
 
Uzito pekee haijitoshelezi.

Huwa ni:
  • Uzito wako
  • Kimo chako
Ndio utapata BMI sahihi.

Yamkini 83kg kwa kimo chako ni uzito sahihi. Hicyo lazima uweke hapa vipimo vyote, uzito na urefu ndio utashauriwa iwapo uzito umezidi au la!

Pole sana kwa hayo maumizvu.
Shuran,

Sent from my 23028RNCAG using JamiiForums mobile app
 
Ndugu Mtandaoni, kuulizia Dawa mtandaoni, sio sahihi, sababu kila mwana_Mtandaoni aliyewahi kuwa na hiyo changamoto atataja dawa yake iliyomsaidia pasipo kutaja kiini cha tatizo lake yeye au wewe.

Hivyo kama wana_mtandaoni 100 kila mmoja akataja dawa yake, utakuwa na aina zaidi ya dawa 100. Je nini kitafuta ndugu Mtandaoni baada ya kuzijua dawa zote hizo.

Nenda hospitali acha mchezo na afya yako.
 
Hamjielewi, bamia hizo afanyiwe upasuaji ziingizwe ndani ya magoti?au sababu bamia zinaleta utelezi,mnahisi ule utelezi moja kwa moja unaenda kwenye magoti? Bamia kwa vidonda vya tumbo sawa.
Hakika una uelewa wa kutosha Sana.Mtu tayari ameshaarika hawezi kutumia bamia zikamsaidia Maana haiendi kutengeneza uteute wa moja kwa moja Kama ambavyo wengi hufikri.Kula bamia ni mhimu kwa kila mtu ili uendelee kuimarisha afya yako ya magoti lakini siyo tiba ya moja kwa moja kwa mtu ambaye tayari magoti yameathirika.Hii no sawa na kuugua malaria halafu ukataka kupona kwa kulala kwenye chandarua badala ya kutibu Kwanza tatizo halafu Sasa ukaendelea kujikinga.
 
Hakika una uelewa wa kutosha Sana.Mtu tayari ameshaarika hawezi kutumia bamia zikamsaidia Maana haiendi kutengeneza uteute wa moja kwa moja Kama ambavyo wengi hufikri.Kula bamia ni mhimu kwa kila mtu ili uendelee kuimarisha afya yako ya magoti lakini siyo tiba ya moja kwa moja kwa mtu ambaye tayari magoti yameathirika.Hii no sawa na kuugua malaria halafu ukataka kupona kwa kulala kwenye chandarua badala ya kutibu Kwanza tatizo halafu Sasa ukaendelea kujikinga.
Yeah,umeleezea vizuri mkuu
 
Maumivu ya goti yanayofanya mtu kushindwa kuchuchumaa yanaweza kusababishwa na mambo kadhaa, ikiwa ni pamoja na:

1. Osteoarthritis: Huu ni ugonjwa wa kupungua kwa tishu laini zinazozunguka viungo vya goti, na kusababisha maumivu, uvimbe, na ugumu wa goti.

2. Patellar tendinitis: Hii ni hali inayosababishwa na kuvimba kwa kano ya patella, ambayo hujulikana kama "jumper's knee." Mara nyingi hutokea kwa watu wanaofanya mazoezi ya kukimbia au kuruka sana.

3. Chondromalacia patellae: Inatokea wakati wa uharibifu wa giligili laini inayozunguka sehemu ya mbele ya goti, hasa kwenye "cap" ya goti, na inaweza kusababisha maumivu makali hasa wakati wa kuchuchumaa.

4. Ugonjwa wa goti la mbele (Anterior knee pain syndrome): Hii ni hali ambayo husababisha maumivu upande wa mbele wa goti na inaweza kuwa mbaya zaidi wakati unachuchumaa au unapanda ngazi.

5. Mishipa ya goti iliyovutika au majeraha ya meniscus: Mishipa na meniscus ni sehemu za goti zinazosaidia katika utulivu na harakati zake. Majeraha ya maeneo haya yanaweza kusababisha maumivu wakati unajaribu kuinama au kuchuchumaa.

6. Ugonjwa wa maambukizi au uvimbe (bursitis): Maambukizi au uvimbe kwenye viungo vya goti unaweza kusababisha maumivu na kushindwa kuchuchumaa.

Kama maumivu yanaendelea, ni vyema kumuona daktari kwa uchunguzi wa kina ili kubaini chanzo halisi na kupata matibabu sahihi.
97.9% ni namba moja hapo kama ukitumia hizo meloxicam na bado ikawa hausaidiki nifuate PM ujiandae na Surgery
 
una uric acid ya kutosha
●Acha kabisa kula nyama yoyote
samaki wabaharini dagaa wa baharini wanakiwango kikubwa cha kusababisha uric acid,
●Samaki wa maji baridi stop
●Acha kabisa soda...
baada ya mwezi njoo hapa ueleze kama una maumivu tena
Mimi ninavyopenda dagaa na sato mbona hapo umenimaliza kabisa?🤣🤣
 
Mimi ninavyopenda dagaa na sato mbona hapo umenimaliza kabisa?🤣🤣
nilienda hosp nimebebwa .siwez kukaa kbs..Dk aliponiona weight yangu akaniambia acha coca na hayo mazagazaga .sijui alijua mm mlevi wa coca! aise niliweweseka .nikaachabwiki 2 mzima kbs .mpk leo nadunda ila coca nimeshindwa kuacha
 
nilienda hosp nimebebwa .siwez kukaa kbs..Dk aliponiona weight yangu akaniambia acha coca na hayo mazagazaga .sijui alijua mm mlevi wa coca! aise niliweweseka .nikaachabwiki 2 mzima kbs .mpk leo nadunda ila coca nimeshindwa kuacha
Mimi nilikuwa mtu wa kula pipi 200 kwa siku, sukari kwenye chai nusu kikombe, mkate 1 breakfast peke yangu, supu, nyama choma, bia asubuhi mchana na jioni. Rafiki yangu mmoja akanishauri nipunguze, akisema "usiposhauriwa na mimi utashauriwa na daktari". Nikatafakari, nikaamua kuachana na pipi, sukari (vijiko vidogo viwili tu), mkate slices 2 au 3 tu, nikaachana na supu, bia nimeacha pia (kwa hiari) na nafanya mazoezi ya kuruka kama kuruka kamba (akini bila kamba) - asubuhi naruka mara 1,000 na pushup 30 na jioni pia mara 1,000 na pushup 30, then napumzika kama dk 10-15, kisha naoga. Safi sana!
 
Wapendwa Wana JF, Habari za Leo,

Naomba msaada kutoka kwa wale wataalamu wa kutibu ugonjwa wa magoti. Nina tatizo hili, na hata kuchuchuma nahisi maumivu makali.

Je, ni dawa gani ningeweza kutumia, ndugu zangu? Msaada wenu unahitajika.

Sent from my 23028RNCAG using JamiiForums mobile app
Kama sio gout bas uric acid
 
Mimi nilikuwa mtu wa kula pipi 200 kwa siku, sukari kwenye chai nusu kikombe, mkate 1 breakfast peke yangu, supu, nyama choma, bia asubuhi mchana na jioni. Rafiki yangu mmoja akanishauri nipunguze, akisema "usiposhauriwa na mimi utashauriwa na daktari". Nikatafakari, nikaamua kuachana na pipi, sukari (vijiko vidogo viwili tu), mkate slices 2 au 3 tu, nikaachana na supu, bia nimeacha pia (kwa hiari) na nafanya mazoezi ya kuruka kama kuruka kamba (akini bila kamba) - asubuhi naruka mara 1,000 na pushup 30 na jioni pia mara 1,000 na pushup 30, then napumzika kama dk 10-15, kisha naoga. Safi sana!
duh..mara 1000 wewe sio mwenzetu aise..hongera sana kujali afya yako
 
Back
Top Bottom