Msaada: Mjomba anatatizo la kupata choo

Msaada: Mjomba anatatizo la kupata choo

Akafanye x-ray ya tumbo na ultrasound ya abdominal-pelvis kwanza halafu lete picha hapa nikusaidie na ripoti ya ultrasound. Lakini pia mwili haumuwashi? muulize
Msaada plse
 
Kwa rangi hiyo ya hajja. Ndugu yako ana vidonda vya Tumbo mkuu. Akitumia dozi ya Heligo Kit kwa siku 14 then aaanze kumeza PANTOPRAZOLE SODIUM kwa siku 30 kupunguza acid kuzalishwa tumboni atapata choo kizuri na kilaini wakati woote. Kwa hali hiyo hata Nguvu za Kiume zimepotea na Tumbo ni mwendo wa kujaaa gesi na Usingizi hapati ng'ooo.
Napata raha sana haya maelezo,watu mko vizuri sana na fani zenu
 
Msaidie atumie shake off imemsaidia sana ndugu yangu alihangaika sana lakini hii kitu ilimtoa sana mkuu

Mtafute 0692948695alitupa msaada sana
 
umri wake ni miaka 47 Kwa Sasa amekuwa akisumbuliwa na tatizo la tumbu yaani akienda hospital kupima anakutana na shida za kawaida tu kama typhoid au minyoo au vidonda vya tumbo na wakati mwingine hakutwi na tatizo lolote. Na amekuwa akipewa dawa, lakini anapata unafuu wa mda mfupi.

Hali hiii imekuwa ya miaka mingi mpaka Kwa Sasa imempelekea kuwa na choo kigumu (nitaambanisha mwishoni).

Kutokana na alivyonieleza ilinilazimu kumwambia apige picha haja yake Ili tuambatanishe Kwa lengo la kupata uhalisia wa kitu ninachoeleza lakini pia kinisaidie kumwelezea Dr. Nitakapoenda Bugando ( Kwa yeye huwa anakigugumizi hawezi kujieleza Moja Kwa Moja, hivyo huwa naambatana naye kwenye shida zinazohusiana na kujieleza).

Licha ya yeye kukata tamaa, Nimemshauri twende Bugando Hospital nikishauri apimwe Kwa kutumia vipimo vikubwa kubaini tatizo.

Kwa upande mwingine nimeanzisha maada hii, Ili kupata ushauri wa watalaamu wa afya waliomo katika jukwa hili. Kwa hiyo naomba msaada Kwa yeyote anayejua/ au mwenye ushauri.

Update.
Mgonjwa alikutwa na tatizo la H.pyroli ( baadae nilifuatilia google nikagundua ni bacteria anayesababisha vidonda tumbo).

Akaandikiwa akanunue dawa inayoitwa Heligo-kit, lakini baada ya kwenda dukani waliponionesha hizo dawa nikagundua kuwa alishawahi kupewa zaidi ya mbili lakini anapata nafuu ya kama wiki mbili tu.

Sasa ikanibidi niingie google Ili kujua zaidi namna ya kukabiliana na changamoto hii.

Sasa katika mitandao nikaoata maple dekezo ya dose zifuatazo.

Wa kwanza.

Matibabu ya Siku 10
Siku 5 za mwanzo
1. Amoxicillin 2000mg Kwa siku.

Siku 5 baada ya Siku Tano za mwanzo
1.Clarithromycin 1000mg Kwa siku.
2.Tinidazole 1000mg Kwa siku.
3. Pantoprazole 1x2

Wa pili dozi aliyopendekeza
1. Amoxicillin 1g mara mbili Kwa siku 14.
2. Clarie OD 500mg mara 2 Kwa siku 14
3. Tinidazole 500mg mara 2 Kwa siku 7, then ornidazole 500mg mara 2 Kwa siku 7
Esomepraole 40 mg x 2 Kwa siku 14.

Na wa tatu.
Clarithrimycin extended 1x1
Tinidazole 1x2
Pantoprazole sodiam 1x2
............................................
Sasa wadau!
1. Je ipo tofauti kati ya hiyo Heligo-kit na hizi dozi.
2. Kati ya hizo dozi ipi inaweza kufaa au mchanganyiko mzuri.
3. Pia ule mchanganyiko wa dozi ya pili sijauelewa mnawaza nifafanulia?

Watalaamu naombeni msaada
Sangasanga ndo kiboko. 0699254400
 
Anayefahamu anisaidie
Tafuta periwrinkle plant (ingia google) lenye maua ya pink chemsha mizizi yake anywe kikombe cha robo kila siku asubuhi yaani tumbo likiwa tupu. Atasahau hiyo shida aliyonayo
 
Ndiyo! Tumbo kuwaka moto, mate kuwa machungu, mkojo kuwa wa langi na unaunguza wakati akojoapo, gesi tumboni, nguvu za kiiume zimepungua.
Huyo ni wewe mwenyewe. Siyo ndugu yako.
 
Back
Top Bottom