Msaada: Mke wa mtu anataka kuhamia kwangu

Msaada: Mke wa mtu anataka kuhamia kwangu

Baada ya kumfanya mke wa mtu single mother ndo unakuja na point kwamba utaki kuoa single mother , kwani ulimkuta single mother????????

Wewe ni mwanaume take responsibility of the problems you caused , umeshaharibu ndoa ya watu na unakimbia we ni fala...

Ushauri wangu ukijiridhisha jamaa kweli amempiga chini mchukue mkaishi mkoa mwingine sababu wewe ndo chanzo cha matatizo yote hayo.....
Haina shida bro! Ngoja mambo yatulie kwanza
 
Kwani wakati unamchakata hujui kama ni mke wa mtu? ila wee una roho ngumu kama paka, hadi unaenda kulala kwake? hadi watoto wake unawaletea zawadi? Kwa taarifa yako Hao watoto ndo informer wazuri kwa baba yao akirudi toka safarini. Vaa kiatu cha huyo mwanaume mwenzako mkeo afanyiwe hivyo unavyomfanyia ungemfanyia nini mwanaume anayetembea na mke wako? Kwa ufupi hujui tips za kudate mke wa mtu umejipeleka kichwa kichwa
Hata hivo nimetubu siwezi date tena Mke wa mtu...
 
Hata hivo nimetubu siwezi date tena Mke wa mtu...
Mkuu sisi wanaume tunajuana, kudate mke wa mtu watu wanafanya sana, ila kuna vigezo na masharti vya kuzingatiwa. Wewe nimekushangaa sana hapo kwenye kwenda kulala kwake hadi unacheza na watoto wa mwanaume mwenzako hapo nimeshangaa sana. au ndo ile kusema mapenzi upofu
 
Mkuu sisi wanaume tunajuana, kudate mke wa mtu watu wanafanya sana, ila kuna vigezo na masharti vya kuzingatiwa. Wewe nimekushangaa sana hapo kwenye kwenda kulala kwake hadi unacheza na watoto wa mwanaume mwenzako hapo nimeshangaa sana. au ndo ile kusema mapenzi upofu
Tena jamaa huyo mwenye mke ni boya sana. Alitakiwa amtegee ili amlawiti kabisa huyu dogo. Unaachake mkeo mwenye mtoto kiboya hivyo bila kushughulikia jamaa?
 
Khabarini wana jukwaa.

Mwaka 2021 nilikutana na dada mmoja mzuri sana, mrembo, mwenye kuvutia na mpole sana ambaye mwanaume yeyote mwenye akili timamu lazima tu angempenda. Basi nikafanya mchakato nikapata mawasiliano yake. Baada ya kuwasiliana na kumueleza shida yangu hakuwa na hiyana hivyo tukaingia katika mahusiano japo alinambia kuwa yeye ni mke wa mtu na ana Watoto wawili.

Kusema kweli tulipendana, mpaka sasa nampenda sana. Mme wake ni mtu wa mishemishe, mara nyingi hayupo. Hivyo nilikuwa naenda usiku kulala kwake na siku nisipoenda basi nilikuwa nampigia simu huyo mpenzi wangu tunazungumza hadi usiku wa manane. Au chatting kwa WhatsApp au sms za kawaida. Japo tulifanya kwa siri sana na mtu asingeweza kugundua, hata rafiki zangu wa karibu hawakujua na rafiki zake pia hawakujua lolote.

Penzi letu lilinoga mno, ilifikia hatua nikawa namiliki CREDIT CARD ya mme wake, na haikuwa issue kufanya miamala midogo midogo. (sio kwamba nilikuwa nalelewa sema tu alinipenda na kuniamini kiufupi tunapendana) pia nilimpenda mno mtoto wake mdogo, nilikuwa nampelekea vizawadi zawadi nikienda kulala, nacheza nako in short ni kacheshi mno kale katoto na kalinipenda pia.

Wakuu, hakuna marefu yasiyo na ncha, hatimaye mwenyemke akajua kwamba mke wake anachepuka, (hapo ndipo chanzo cha tatizo langu) akajaribu kutafuta ajue anachepuka na nani, akatafuta mpaka akapata namba yangu, mke wake akanambia kuhusu hili hivyo tukakubaliana tusitumiane sms na atakuwa ananitafuta yeye. Na mimi niliamua kuchukua extra precaution ikiwa ni Pamoja na kutopokea namba ngeni, pia mke wake alikuwa akinipigia nikipokea nasubiri aanze yeye kuongea ndo na mimi niongee. Baada ya jamaa kuona sipokei namba ngeni wala kujibu sms za namba ngeni aliamua kutafuta jina nililosajiria laini, nashukuru mungu laini yangu hiyo nilisajiri kwa jina la mtu mwingine na mtu huyo alikuwa mkoani hivyo asingeweza kunifahamu.

Baada ya harakati za kunitafuta kugonga mwamba, jamaa aliamua Kwenda mkoani kuendelea na mishe zake. Mimi na mpenzi wangu tukarudisha mapenzi na tukaendelea kuchati na kupeana mambo kama kawaida. Siku ya jumamosi mwezi wa nne tarehe 13 jamaa alirudi, na mke wake alinijuza juu ya ujio wake. Usiku mida ya saa 4 kuna message moja illingia WhatsApp kutoka namba ngeni nanukuu

“NIMEAMUA KUKUACHIA HUYO MWANAMKE, KESHO ATAKUJA MUANZE NAE MAISHA, MIMI NTABAKI NA WANANGU. ASANTE SANA MWANAUME MWENZANGU”

Ujumbe huu ulinishitua sana na ukizingatia ulikuwa umeeandikwa kwa maandishi makubwa kuonesha msisitizo, kusema kweli niliamua kuhama ghetto nikaenda logde kulala ili kulinda usalama wangu maana nilihisi kama naweza patwa na jambo baya. Pia simu nilizima ili isije kuwa tracked nikapatikana kiboya. Usiku sikupata usingizi hata kidogo yaani hata kufumba tu macho hakuna. (acheni jamani watu tunapitia shida sana hapa Tanzania duh) kuna mda natamani hata niwe mkimbizi Afghanistan kuliko kuishi hapa Bongo.

Kuna jambo moja ambalo mke wake hakunambia na alinambia ikiwa ni too late. Kumbe jamaa alimpa zawadi ya simu kabla hajarudi mkoani kwenye mishe zake, simu hiyo alikuwa ameihack achilia mbali normal sms and calls, hata chatting za WhatsApp alikuwa anaziona na kuzisoma. Jambo hili lilinishitua sana maana nilijua atakuwa amenasa pia picture zangu tunazotumiana na mkewe hivyo kudakwa ni suala la muda tu.

Kwa ufupi ni kwamba.

Jana Asubuhi na mapema nilihama huo mtaa, nikaenda mtaa mwingine mbali kabisaa maana nilihisi jamaa anaweza niletea huyo mke wake hadi kwangu. hivyo asubuhi na mapema niliita Kirikuu ikabeba vitu vyangu nikasepa. Leo saa 4 usiku nikapokea simu ya huyu mwanamke (mpenzi wangu) akanambia kwamba

baba jay (code) amekuja na mwanamke mwingine, mimi amenifukuza amekatalia watoto wake nimekuja hapo kwako wamesema umehama, kwanini umehama bila kunambia? Uko wapi nahitaji tuzungumze.

Ujumbe huu umefanya nikatetemeka kuanzia unyayo mpaka utosi, sikutarajia jambo kama hili, huyu mwanamke anasema anataka aje tuishi, pia nimsaidie afungue shauri mahakamani ili apewe talaka, mgawo wa mali na Watoto pia. Yaani niko njia panda nawaza nimuelekeze nilipo? Dah! Hata sielewi… na mimi sina mpango wa kuoa saa hizi. Yaani kimsingi sitaki kabisaa mambo ya kuoa iwe leo au kesho. Hata nikitaka kuoa siwezi oa single mother, nyumbani watanielewaje? Wakiskia story kuhusu huyu mpenzi wangu je itakuwaje? Duh.

Mambo ni mengi sema siwezi Andika yote ntapoteza muda wenu bure.

Ndugu zangu naombeni Mnishauri nina shida sana. Yaani dunia imekuwa chungu sana kwangu, naishi kwa kujificha kama mnyama duh! Nimechoka na maisha ya utumwa. (better die free than living as a slave)

Endelea 👇 👇

Msaada: Mke wa mtu anataka kuhamia Kwangu
Kubali kwanza umefanya makosa Kwa kujua kwakuwa mwanzoni alishakumbia ni mke wa mtu lakini bado ukaendekeza hisia bila kujali maumivu anayoyapitia mwanaume mwenzio Kwa kumharibia ndoa yake Wala hata hukujali Hadi anakutumia huo ujumbe kwamaana mahusiano yenu yamefikia hadharani ushauri wangu ondoka kwenye maisha yake Anza maisha Yako upya ikiwezekaza usitafute kabisa
 
We ruka ruka tu, soon utajaa kwenye Flame.
 
Hiyo technic ya kununua zawadi ya simu na kumpa mtu wako ukiw umeifanyia maumyama naifanya sana, ila wamefika watatu baada ya kupokea simu za zawadi tuliachana week hiyo hiyo sbabu ya uzinzi unaofanyika kwa kutumia simu yangu.
 
Mambo mengine wanaume huwa tunajisahau sana. Yaani ulitumia mpaka ATM yangu halafu bado ukaona wewe ni mjanja? Unakimbia nini sasa mwanamke nimekuachia unakimbia nini sasa wewe si ni kiume ambaye mpenzi wako ni mke wa mtu na ulijua tangu mwanzo? Mchukue mkaishi huko uliko wewe muendeleze Mapenzi.
 
Mkuu sisi wanaume tunajuana, kudate mke wa mtu watu wanafanya sana, ila kuna vigezo na masharti vya kuzingatiwa. Wewe nimekushangaa sana hapo kwenye kwenda kulala kwake hadi unacheza na watoto wa mwanaume mwenzako hapo nimeshangaa sana. au ndo ile kusema mapenzi upofu
Mungu anisamehe kaka.
 
Mambo mengine wanaume huwa tunajisahau sana. Yaani ulitumia mpaka ATM yangu halafu bado ukaona wewe ni mjanja? Unakimbia nini sasa mwanamke nimekuachia unakimbia nini sasa wewe si ni kiume ambaye mpenzi wako ni mke wa mtu na ulijua tangu mwanzo? Mchukue mkaishi huko uliko wewe muendeleze Mapenzi.
Naamini Mungu atanisamamia. Inshallah
 
Tena jamaa huyo mwenye mke ni boya sana. Alitakiwa amtegee ili amlawiti kabisa huyu dogo. Unaachake mkeo mwenye mtoto kiboya hivyo bila kushughulikia jamaa?
Usiniombee mabaya namna hiyo. Sisi sote ni wanaume... Leo Kwangu kesho kwako...
 
Mkuu tumedumu kwenye mahusiano almost 4 years sasa. To be honest alikuwa kama Mke wangu tu. Four years nyingi sana... Na hapo kuna mambo sijataka kuyaweka hadharani.
Sijajua umeboronga ukiwa mkoa gani na unahamia mkoa upi, ila nawaza tu kuwa ingefaa uzamie nchi nyingine kabisa kama DRC, Zambia, nk, utulie na kuanza upya. Ufanye mishe huko hata miaka 10 bila kukanyaga Tz.

Kuhusu huyo mpenzi wako (mke wa mtu) kujaribu kumrudia ni sawa tu na kuvaa bomu, utajuta
 
Sometimes we meet right peoples in wrong destination. I assure you "kama angekuwa hajaolewa basi ningemuoa" she is a good woman.
I hope watayajenga na mmewe waishi happy than ever. Inshallah
Nakumbuka kipindi fulani, jamaa nilimuachia demu wangu (mke wangu mtarajiwa) sijui walioana, sijui.
Kuishi na mwanamke msaliti, haitaji moyo wa chuma
 
Back
Top Bottom