Msaada: Mke wangu ana hasira kupita kiasi

Msaada: Mke wangu ana hasira kupita kiasi

kutibu ni shughuli maana itabidi umuaminishe kuwa anatatizo kitu ambacho hawezi kubali. sidhani kama sifa zake zinakidhi bipolar. atakuwa ana moja ya personality disorders.
 
Mke wangu alikuwa namna hiyo, alikuwa anakasirika ghafla afu baadae anapoa, nikaa nae kuongelea hali hiyo akasema hata yeye haipend ila inamtokea tu.nikawa namhimiza sana kusali kabla ya kulala nikawa nae karibu. Nikaacha kumkosoa hata akiharibu. Siku moja alinambia mambo flan mabaya niliyowahi kumfanyia. Aliongea sana akalia usiku kucha toka hapo hali hiyo ikaisha. Mkeo atakuwa amekaa na mengi moyoni mwake.
 
Jitahidi kumpa nafasi afungue moyo wake labda ana mazito moyoni.Hii inatokana na kufanyiwa mambo mabaya au kutokewa na jambo gum alaf hukupata wa kukufariji.Binadam yoyote ni mpweke anahitaji faraja.
Hii pia hutokea pale ambapo hujampa mwanamke attention kikamilifu.Mfano akiamka asubuhi anza kumsifia mwambie my dear hivi karibuni naaza kukuona unazidi kuwa mzuri.Yaani nakuwaza kila nikiwa kazini unanichanganya akili jitahidi uwe karibu na mimi.Jioni ukirudi mkumbatie vizuri.Akivaa mwambie umependeza .Ukiwa kazini mtumie meseji za mapenzi.Hata I love you honey inatosha(Wanaume mkishaishi na mtu meseji za mahaba hamtumi tena hii nayo inaongeza hasira.)Mwambie unajiskia vizuri kuwa nae maishani kama ana jambo lolote akushirikishe utafurahi sana kwani mapenzi juu yake yameongezeka mara dufu.Wanawake wenye hasira wanpenda kubembelzwa hatarii.Wewe mpe nafasi ya kumbembeleza uone atakavyokuwa mpole.
Hata kama atakuwa na hasira kama za nani sijui atashuka atakueleza kila kitu kinachomuumiza.
Pia jenga mazingira ya kuhakikisha anakunywa maji ya kutosha yanapunguza hasira.Ukiona ameanza kushuka mwambie sasa usivyopenda hiyo tabia ya hasira na umeanza kuiona sijui ndo mapenzi kuongezeka au nini ila awe anajiangalia ili asikupunguzie furaha uliyo nayo juu yake.
Baada ya kumwambia hivyo kiustaarabu atabadilika na hutoamini kama ni yeye.
Nina experience fuata maelekezo yangu it is somehow funny but it really works.
 
Back
Top Bottom