Msaada: Mke wangu anataka tuwe tunaishi na mtoto wa dada yake kila wikiendi na likizo

Viatu vyako vinatoshana na vyangu, ila akae na mkewe waongee, wapime umuhimu, waweke makubaliano, mwisho yeye kama baba asimamie maamuzi
Ukweli ndio huu, na hili sioni mantiki ya kushauriana na mkewe maana anaeza kumzidi kwa hoja[emoji23][emoji23][emoji23], hapo atoe amri tu kama baba mwenye nyumba na pia anaeza kumwondoa kisayansi tu.
 
Huyu mtoto tunaita ni mtoto wa nje, usijaribu kufanyia chuki na kumuonea huyo mtoto ata siku 1 yeye hana kosa lolote na kama utamlea utapata thawabu sana kwa Mungu, huyo unayesema ni baba yake na hamshughulikii huyo wala si baba yake kisheria ata mirathi hataweza kurithi kwa mujibu wa sharia yetu ya kiislam.

Kuwa na moyo wa kumsaidia huyo mtoto akue apate elimu kupitia mikononi mwako lakini madam amezoeana na mtoto wako huwezi jua mbele kutatokea nini juu ya huyo mtoto na hata kama hakutatokea hapa duniani basi utapata thawabu nyingi kwa Mola ambazo malipo yake ni pepo.

Huyo shemegi yako mama wa huyo mtoto unayesema ndugu na mke wako mnasihi aache umalaya ajitume akipata chochote juu ya mwanae amsaidie pia mtoto wake, lakini wewe kama wewe huyo mtoto kuwa naye baadae huyo mtoto atakuita baba wala usije kuchukia utapata thawabu kwa kumlea na atakuja kukusaidia na kukumbuka akikua maisha yake yote.
 
Kwani mtoto si ana wazazi?
Hata ikiwa anakula mlo mmoja kwani hatumii ela kununua?
Naona runadanganyana hapa kulea sio gharama
Mkuu ni kweli kila familia inatakiwa kuwa na sheria zake, misaada isizidi uwezo.U
Ulishawahi kubeba familia ya mtu Yaani mama na watoto wa3 wadogo kwa zaidi mwaka mzima hadi mambo yao yakakaa sawa, halafu siku ukapata dharura ukapiga sim kuomba mtoto wako mmoja tuu akashinde kwao siku moja tuu wakagoma? Tena wakakujibu watoto wetu wanajiandaa kwa mitihani huyo ataleta fujo😂😂😂

Walimwengu wa ajabu sana Samboko
Wasiokuelewa hayajawakuta
 
Huyo ataleta fujo[emoji38]
 
Kaka nyumba ni yako asikupangie mtu masharti, kila mzazi awajibike kwa watoto wake sio unazaa unategemea wengine wakulelee afu ukiambiwa ukweli unasema watu wachoyo

Sent from my SM-N960U using JamiiForums mobile app
Na ukifuatilia ijumaa,jumamosi na jumapili ndio masiku yao ya kudanga anaweza zaa mwengine anajua pa kupeleka pako.
Kama haupi tayari mwambie aende kwa bibi na sio kwenu.
Pili kila kisa alifanyalo mchape kighazabu mpaka mkeo ahisi mtoto utamtia kilema.
 
Yamenikuta hayo ndio maana napingana nao wananiona nna roho mbaya,

Mi na mdogo angu wa kiume tumezaliwa tumbo moja tena wa kufuatana hatuongei mwaka wa 6 huu wakati nmemlelea watoto wa3 tena wa2 mapacha alitekelezewa hata hawatembei nimemrudishia mwaka jana wana miaka 6 wakaanze shule bado analalamika kimyakimya[emoji23][emoji23][emoji23]
Mwingine wa kike upande wa baba "kamuua" baba wa mtoto wake na corona ili apate kuendelea kuishi kwangu akilea mwanae kwa mimi kujua mtoto hana baba, nimemtimua juzi tu kwa kuushtukia huo mchezo wao.
 
Haya mambo sio mepesi kama yanavyoongeleka. Mbeba mzigo ndio anajua uzito wake haki
 
Budget ya mtoto wa shemeji yako sidhani kama ni issue kubwa.

Nafikiri issue hapa ni huyo shemeji yako kumkatalia mtoto asiende kwa babake ilhali yeye hana muda wa kumlea.

Pengine huyo shemeji yako weekend anadanga na mkeo anajua.
Mkeo anasaidia dadake adange kwa amani.


Usimkataze mtoto kuja kwako weekend lakini mshaurini huyo mwanamke ampeleke mtoto kwa babake.
Aache ujinga.
 
Ukiachana na chakula watoto wa watu lawama mkuu...kila mmoja aishi na wanawe.
 
Hio hoja nyepesi sana, ni sawa na mtoto amuulize baba kwanini unalala na mama?

Kule kuna utaratibu rasmi uliowekwa na wale watoto wanakuwa managed na Taasisi.
Ankal umeshafeli kos una majibu mepesi sana
 
Orphanage zina utaratibu wake.
Hakuna utaratibu wa kwenda kumsaidia mtu, tumesaidia sana, maana ulicho nacho ndiyo utatoa, ndiyo maana nawaambia mnajifanya wema wakati pesa zenu zinaishia kwa madanga na pombe, shame
 
Uko sahihi sana ila kuna wanaojifanya hapa wema kos wako nyuma ya keypad, kwa ground hata mtoto yatima hawajawahi msaidia, wanaishia kula starehe za pombe na madanga lakini hapa wanajifanya kutetea eti jamaa amlee. Yaani baba yake yupo halafu ujifajye mwema, ni upuuzi sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…