Msaada: Mpira ulinipiga kichwani nasikia kichwa kizito

proxy

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2016
Posts
1,479
Reaction score
1,348
Wakuu,

Habarini za asubuhi,

Jana wakati nipo mazoezini nilipigwa mpira uliokuja kwa nguvu kichwani mpaka nikajisikia kizunguzungu lakini baada ya sekunde chache nikaendelea na game mpaka tulipomaliza, kutoka hapo nikarudi mojakwamoja home na kupiga maji ya baridi ila sasa bado najisikia kichwa kizito na kinauma kwa mbali na kizunguzungu kipo lakini kwa mbali sana.

Wataalam wa mambo kama haya naombeni ushauri nifanye nini au nitumie dawa gani kwa hii hali niliyokuanayo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…