Msaada,mtaji wa mil.3 kwa mwanza nifanye biashara ipi

Msaada,mtaji wa mil.3 kwa mwanza nifanye biashara ipi

Mkuu Kubota nimezipenda sana makala zako kuhusu ujasiriamali. Mi nataka kuwekeza kwenye kilimo eidha kwa kufuga mbuzi/kuku na au kulima mbogamboga na matunda. Ili kufanikiwa katika hayo, maji ni sehemu muhimu sana. Nilifanya survey ya kuchimba kisima cha maji kwenye kishamba changu ili niyatumie kwa umwagiliaji nikaambiwa yapo chini umbali wa mita 150 na bei ikawa iko juu mno kama 14M hivi. Nimepania sana kufanya shughuli hizo za kilimo ili niachane na mambo ya kuajiriwa lakini tatizo ni hayo maji. Kama naweza kupata mchimbaji ambaye atanifanyia kazi hiyo kwa bei ya chini nitafurahi, uwezo wangu haufiki hata nusu ya hiyo bei niliyoisema hapo juu. Naombeni ushauri na mawazo pia wana JF.

Mkuu kama una eneo zuri na unaipenda project unganisha na wadau nguvu kazi ifanyike!!!
Ni bora kupata kidogo kuliko kukosa kabisa
 
Anzisha stationary nyamalango italipa maana milion 1.5 utapata photocopy 1milioni chumba na laki tatu desktop laki mbili rim wino na extension cable..... all the best.

Thinkpad,

what about business licence, pango, set up costs, kuweka LUKU yake mwenyewe n.k ?
 
Bei za Balton ziko wazi kwa greenhouse za size 2; yaani 8m X 15m (6M) na 8m X 24m (7.7M)

Mheshimiwa sana SABAYI kuhusu kuagiza greenhouse ili kujua kujua kama inalipa inabidi kulinganisha bei ya Balton Tanzania (ambao ndiyo supplier ninaowafahamu kwa Tanzania) na bei za Kenya. Sijawahi kusikia wala kufahamu bei za Balton Tanzania nami nitajishughurisha kuulizia sasa. Kwa bei za Kenya ninakuwekea Attachment hapa ujionee mwenyewe bei zao na ulinganishe na bei za Balton. Kuna post hapo nyuma inacontacts zao na wewe utatuupdate kwa utakayoyaona huko. Kuagiza China ni cheap sana isipokuwa inategemea na mizengwe ya Bandarini Dar. Inaweza kuwa cheap sana sana sana kuagiza China lakini wachawi waliopo bandarini Dar es Salaam hilo ni janga la maendeleo ya kitaifa. Mimi niliagiza kifaa China meli ilishapakua mzigo tangu tarehe 25 Feb hadi leo tarhe 18 March karibia tutafunga mwezi bado wanajizungusha tu. Ukiagiza China uwe mvumilivu tu lakini inaweza kuwa nafuu zaidi na hasa mzigo ukiwa mkubwa.
 
Eneo ni zuri na project naipenda kwa vile ndo kimbilio langu la kupambana na umasikini, tatizo ni hiyo bei ya kuchimba hicho kisima. Wadau gani hao mkuu popular? kama unawafahamu washikaji wakuchimba niunganishe nao.
 
Aisee Kubota na Chasha ni noma! yaani mimi nanyonya mavitu yenu mwanzo mwisho!! Mnatuelimisha sana aisee, big up! Na wachangiaji wengine tunashukuru kwa kunogesha jukwaa la ujasiriamali
 
Asante sana Kubota kwa maelezo ya green house mwanzo wala sikuvutiwa na hii kitu ila kwa maelezo haya nimeelewa faida zake, kama inaweza kuzuia magonjwa basi ni mkombozi kwa mbogamboga na matunda kama nyanya na hoho. Binafsi napenda bustani niliwahi kutoka na roses (waridi) Iringa zikiwa nzuri nikasema kwanini Dar hazioti zilianza vizuri sana ila baada ya muda majani yakafa na ukungu na ikawa mwanzo wa magonjwa hadi zikawa hazipendezi kabisa zikafa, nimejaribu kuotesha nyanya hapa home pia zinapata ukungu najua kuna dawa ila sipendelei madawa mengi kwenye mbogamboga nadhani kwa green house itapunguza kama sio kuzuia uharibifu wa mimea hii. Pia kwa sie wa mjini nafasi ndogo huu ni ukombozi hasa. Labda haya maelezo mods watusaidie kuyanunga na ile thread nyingine ili ziwafae wengi. Kuna magazine nili subscribe online "Motherearth news" nayo imeelezea jinsi ya kutengeneza simple GH. Ngoja ni download hizi material nizipitie zaidi. asanteni
 
Naomba pia kufahamu hiyo green house inakuwa na mlango?

Je hewa inatoka wapi kama utafunga hiko kibanda kote kote

Hapo sasa niliposoma ile ya Mother earth news niliona wametaja inakuwa na fan kuwezesha hewa kuzunguka ina maana itahitaji umeme au?
 
fungua mult level marketing distribution company. unauhakika wa 2mil au zaidi baada ya miezi 4 na kila mwezi.
its risk free
haina haja ya kuwa na ofisi
huna haja ya kulipa property tax
huna haja ya system
huna haja ya kudesign product
unaweza expand kampuni yako mpaka nje ya nchi bila hata leseni
call me nikueleweshe zaidi.
0713297066
 
-mult level marketing
-fungua kampuni ndani ya kampuni.
-anza kutengeneza mil 2 kwa mwezi baada ya miezi 4
-haitaji ofisi,kulipia kodi,kulipia pango,wala bidhaa au service
-haina haja ya kudesign system.its already there.
-haina risk ya aina yoyote ile.
-maelezo zaidi 071329706
 
Kama kumbukumbu zangu ni sahihi, ndiyo leo nasoma uzi on Green house farming. Ninahamu sana na suala hili, ila sijui gharama na mbinu muafaka. Kwa maelezo na mwito wako, naomba maelezo zaidi on this issue. Mimi nina shamba la ekari mbili pale Kisarawe ningependa kujiingiza kwenye green house farming hasa kwa mahindi au nyanya kama ulivyo mshauri ndugu FRNK. Na mimi naomba ushauri wako. ASANTE

Huko kisarawe mashamba yanauzwaje? Huenda kukawa na fursa ya kuweka green houses huko.
 
Samaani ivi ulizipataje pesa hizo umelala zikaja au?
 
Bei za drip lines zikoje kwa sasa? anae fahamu atujuze
 
Back
Top Bottom