Msaada mtoto anaharisha.

Maziwa si ishu sana, japo haishauriwi sana kumpa aina mbalimbali za maziwa hasa akiwa chini ya miezi6 na vyema zaidi kuzingatia hilo hata kwa mtoto wa mwaka mmoja...

Mpeleke hospitali haraka, tatizo dogo tu hilo mkuu, huwezi kusaidiwa dawa hapa, mpakaa dokta aonane na mgonjwa, aone hali yake
 
Mwambie mama asisahau kupima ujauzito

love thé love or hâte thé love.....
 
Nashukuru sana mkuu kwa ushauri.
Nimekuelewa vizuri mno.

Pia mwanangu ameacha kuharisha anaendelea vizuri
 
Nashukuru kwa ushauri,mama ni mwajiriwa ndio maana wakati yupo kazini ndio huwa anapewa hayo maziwa.
 
Mkuu huyo bacteria asiekufa kwa kuchemsha anaitwaje? Jambo kubwa la kuzingatia mleta mada inashauriwa usimpe mtoto mchanga kitu chochote cha kula au kunywa hadi atimize miezi 6, isipokuwa dawa tu au hiyo ORS. Unaweza kuibia kumpa maji ya kawaida yaliyo chemshwa wakati akiwa mzima. Kama mama unakuwa mbali na mtoto basi mkamulie maziwa ya mama yake hifadhi ktk chupa maalum na usafi uzingatiwe sana. Maziwa ya kopo nayo kwa dunia hii iliyotawaliwa na bidhaa bandia hasa za mchina ni kubahatisha. Kumbuka kashikashi (scandal) la maziwa ya watoto yenye sumu kule uchina nadhani ni 2007/2008 ilivuma sana ktk vyombo vya habari.
Mimi binafsi watoto wangu wamekulia maziwa ya ng'ombe. Sikuona tatizo la huyo bacteria labda walikuwa wanakupa maziwa wakati ng'ombe amechomwa sindano. Tatizo kubwa la maziwa ya ng'ombe hasa yasipowekwa maji ni kuziba choo, yanatengeneza donge la chembechembe ngumu nyeupe na kuziba njia ya hajakubwa. Hii ni kwa mtoto mchanga tu wa chini ya miezi 8.
 
Nashukuru kwa ushauri,mama ni mwajiriwa ndio maana wakati yupo kazini ndio huwa anapewa hayo maziwa.
Mama akamue maziwa yake yawekwe kwenye chupa iliyo chemshwa. Hakikisha nyonyo ile ya chupa inachemshwa na kuzibwa na kifuniko wakati wote, pia inaoshwa kwa maji ya moto kila baada ya kunyonyeshwa mtoto. Maziwa ya mama yanakaa muda mrefu bila kuharibika. Mama ale chakula cha kutosha ili kupata maziwa mengi. Aflajiri kabla hajaondoka anaanza kukamua.
 
mpe ORS, ukipata ile yenye picha ya chungwa nzuri. harufu yake inapendwa na watoto. hii itamsaidia kurudisha Maji yalopotea mwilini na kumpa nguvu.
2. Mimi wangu hali ilipozidi walimpa prinagly kwa kuwa aliharisha hadi akapungua nusu kilo
 
kubwa kuliko yote ni kutafuta chanzo cha tatizo. inawezekana ni uchafu au aleji ya kitu either direct kwa mtoto mfano maziwa au chakula au kupitia mama. ndio maana kuna baadhi ya dawa zinakatazwa kwa wajawazito na wanyonyeshaji. KUNA SIKU NILIPEWA DAWA HOSP NIKANYWA J3 MCHANA. MARA JIONI MTOTO AKAANZA KUHARISHA. NIKAHISI KALA UCHAFU. Kutokana na kuharisha nami nikaongeza speed ya kunyonyesha, ikawa nambadili mtoto hata Mara 5 had 7, nampa dawa lakini wapi. nikaja kugundua Siku ya alhamis, nikaacha kutumia dawa, ijumaa mtoto akafunga. so chunguza nn tatizo ili utibu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…