MSAADA: Mtoto hataki kulala

GAZETI

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2011
Posts
5,286
Reaction score
6,736
Habari wakuu,

Kwa wale waliowahi kulea watoto wagumu kulala mlikuwa mnafanyaje? Yaani mtoto mpaka saa 6 usiku anakomaa na watu wazima kwenye Tamthilia. Hata ukisema ulale mapema huo usumbufu ndio balaa, ataanza kukuvuta hiki na kile yaani ni balaa tu.

Hivi hili ni tatizo au kitu gani? Yaani hata miaka miwili hajatimiza huyu akikua si ndo atalala nusu saa kwa siku?
 
Mwaka mmoja na miezi 5
 
Ana umri gani? Mpe maziwa ya vuguvugu jioni unaweza kuweka milo kidogo. Maziwa yana melatonin ambayo husaidia kuleta usingizi.
Mwaka mmoja na miezi 5
 
Huyo si mkubwa kabisa asee? Kuna mambo mawili.
1.Huyo mtoto ni sensitive.
2.Hiyo nyumba inahitaji maombi.
 
Mtoto akishiba atalala bila wasi na aogeshwe tena kabla ya kula na kushiba.

Pia kulala mchana kunachangia.. kama ni jioni analala badilisheni apumzike mapema.. asilale muda mrefu.
 
isee wa kwangu nae usingizi ukikata saa9 anataka mcheze sauti anayo toa kubwa utafikili ni saa 2 asbh.
 
Huyo mtoto atakuwa hashibi vizuri, anahitaji michezo zaidi na kuongezewa lishe ya ziada mbali na maziwa ya mama. Kuna uwezekano mkubwa kuwa mwili wake una uchakataji wa viinilishe uliopita juu ya kiwango cha kawaida kwa umri wake, hivyo ni vizuri ukamuongezea aina nyingine za vyakula,kiwango cha vyakula na kuweka utaratibu wa kumlisha kila baada ya masaa 2-3. Akiisha shiba hakikisha anacheza sana na usimruhusu kulala mchana.
 
My two cents from a distance:

Jaribu kuchunguza tena vyakula anavyokula na vimiminika anavyokunywa masaa matatu au manne kabla ya muda wa kulala.

Si ajabu akawa anaingiza kiwango cha caffeine mwilini mwake ambacho.

Nadhani utakuwa unazijua athari za caffeine kwenye mambo ya usingizi.
 
Mkuu, huyu mtoto anacheza kupita kiasi. Yaani kupita kiasi... Mchana sio mlalaji labda tuangalie ushauri
kuhusu Ulaji
 
Mkuu, huyu mtoto anacheza kupita kiasi. Yaani kupita kiasi... Mchana sio mlalaji labda tuangalie ushauri
kuhusu Ulaji
Ok hakikisha anapata milo midogo midogo mingi iliyo na virutubisho kamilifu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…