Msaada: Mtoto kulia kiajabu mfululizo kabla ya kulala

Kapuku83

Senior Member
Joined
Sep 8, 2012
Posts
146
Reaction score
35
Wadau habari zenu,nakuja tena hapa jukwaani kuomba msaada wenu kwa masahibu yanikutayo!nina mwanangu ana umri wa miaka miwili sasa,cha ajabu kila ifikapo usiku,hasa kuanzia saa tatu,uwa analia sana tena sana kwa kilio cha ajabu kwa muda hata wa masaa mawili mpaka matatu hivi,uwa pia analia kama vile kuna kitu kinamtisha na anajaribu kupambana nacho!tumempeleka hospital lakini hakuna kitu chochote kilichogunduliwa,hapa kichwa kinaniuma wandugu,sijui hata nianzie wapi na niishie wapi,naombeni ushauri wenu ndugu zangu!
 

Pole kwa ilo jambo ndugu yetu,najua kama mzazi utakua unaumia sana juu ya ilo,ushauri wangu ni kua,hii dunia ina mambo mengi sana mkuu,tembea ujionee,na hata haya mambo ya giza pia yapo japo hatuya amini sana,jaribu kuhangaika na mtoto upande mwingine pia mbali ya hospital pekee!jaribu kwa mapadri,masheikh na hata "wataalam" pia,kikubwa usimdhuru mtu
 
Mkuu.Kapuku83 kuna vitu vibaya ndani ya nyumba yenu vinamtisha ndio anapiga makele mtoto wenu fanya hivi jaribu kununuwa dawa moja inatwa Mvuje na upate na kitunguusaumu punje moja na kipande cha mkaa kimoja vitu vyote hivyo viwe vidogo vidogo funga katika kitambaa cheusi mfunge mkononi huyo mtoto. Na pia usimlaze giza mtoto wewe unapenda kumlaza giza ana inamiwa na pepo mbaya usiku huyo mtoto wako na chini ya mto wake huyo mtoto muwekee kisu kisichokuwa na mpini na ndimu moja na mkaa kipande kimoja fanya hivyo na uwe unamuombee dua kila usiku kisha uje unipe feedback.
 

Asante sana ndugu yangu,hata mimi hisia zangu zilinipelekea kuwaza kua hii nyumba ina vitu visivyo vya kawaida!maana si kawaida,ila pa kuanzia ndio nilikua sipajuhi!nashukuru sana ndugu yangu!
 

Nashukuru kwa ushauri wako mkuu
 
Mwanao analilia jina la mzazi mmoja wapo toka upande wa kiumeni. Kama ni Mtoto wa Kiume Mwite kwa jina na Baba yake Mumeo au kama ni mtoto wa kike mwite kwa jina la Mama yake Mumeo huwezi kuamini atanyamaza moja kwa moja na hayo ndiyo majina ambayo mtayatumia mara kwa mara ili asirudie kulia lia.
 
Mmejaribu kumpeleka kwenye maombi?
 

Kuna mtu nae amenigusia na kunisisitizia kuhusu ili mkuu!je jina lake la awali ambalo liko kwenye vyeti itabidi tuachane nalo kabisa au?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…