Msaada: Mwanangu hapati maziwa ya kutosha kutoka kwa mama yake

Msaada: Mwanangu hapati maziwa ya kutosha kutoka kwa mama yake

Phdum

JF-Expert Member
Joined
Apr 15, 2019
Posts
1,322
Reaction score
3,278
Habari zenu wana jf?

Ni mwezi sasa toka mama watoto wangu ajifungue lakini toka alivyojifungua alikuwa na tatizo la maziwa kuwa machache. Na tukafanya kila mbinu ili mziwa yaongezeke ikiwa ni pamoja na kumuwekea ratiba ya kunywa supu ya makongoro, kula ugali wa dona pamoja na kumtengenezea uji wa lishe bila kusahau pilipili manga kwenye uji na supu kwa sana.

Baada ya kufanya hivyo kidgo maziwa yalianza kutoka lakini sio katika kiwango kinachoridhisha, kwani mwanangu ana mwezi na wiki zake lakini afya yake kama ana wiki 2, Naombeni ushauri kwa wale wazoefu pamoja na ma dr wa hapa kama naweza nikamuanzishia mwanangu chakula mbadala kwa umri wake huo wa mwezi moja, au labda kama kuna namna nyingine ya kumfanya mama ake apate maziwa mengi na yakutosha.

Kwani kwa ma dr niliowaona wananiambia akazanie tu pilipili manga wakati mwanangu ukuaji wake ni wa kusuasua. Naomba kuwasilisha.

Updates.
Wana jf poleni na majukumu yenu ya kila siku.
Nimerudi tena kuleta mrejesho kuhusu andiko langu hapo juu, kwani nilijaribu kutumia mbinu na njia nilizoelekezwa na wadau, lakini naweza kusema kuwa njia moja tu ndio niliweza njia yenyewe ni kumpa mwanangu maziwa ya kopo.
Kulingana na mzingira ninayoishi maziwa yanayopatikana kwa urahisi ni lactogen na infacare hivyo nilimchukulia ya lactogen.
Lakini kwa masikitiko makubwa nasikitika na namwonea mwanangu huruma, kwani SITOWEZA TENA KUMUDU GHARAMA ZA MAZIWA YA KOPO. NA NATEGEMEA KUMUANZISHIA MAZIWA YA NG'OMBE NA KUMKOROGEA UJI MWEPESI (n.b mwanangu ana miezi 2).
Kwanini nimefikia hatua hii? Kusema ukweli najiskia vibaya sana ila kwa hali yangu kiuchumi imebidi nichukua maamuzi haya, kwani maziwa ya kopo ni tsh elf 25 na mwanangu anatumia ndani ya siku 2 siku ya 3 amemaliza kopo moja na hapo na maziwa ya mama pia ananyonya japo sio mengi na kijana mwenzenu sina ajira rasmi napambana tu mtaani kwa kweli hali ni mbaya, na mzunguko wa biashara umekuwa mdogo sana. Mwanangu nakupenda sana ila sina budi kukulisha uji kwa umri wako huo.
Pia nilijaribu kuwashauri baadhi ya wataalam wakaniambia maziwa sio mazuri kwa umri huo lakn nitafanyaje? Nimuache mwanangu akonde? Au alie usiku kucha kwa kutoshiba? Dah Japo nimeambiwa mwanangu hutokuwa na akili kwa aina ya vyakula unavyokula kwenye uchanga wako ila naamini Mungu atakusimamia tu na utakuwa na akili tu.
 
Tafuta maziwa ya unga ya watoto mfano ABC, lactogen lakini yawe gold. Asiache kunuonya maziwa ya mama pia.
 
Naamini huo ni uzao wa kwanza ndio first born, sidhani kama kuna ubishi ktk hilo.

Usijali mwambie ahakikishe anakunywa vimiminika kama hizo supu kwa sana na vyakula

vingine yani endeleeeni na utaratbu huo huo Chuchu zitafunguka tuu muhimu asiache mpa mtoto

nyonyo maana kadri mtoto anavyonyonya mara kwa mara ndio tatzo linaondoka na kupotea kabisa,usijali.

muhimu msisitize mkeo ashindilie msosi haswa hayo masupu supu mamitori yasicheze mbali,zitafunguka tu boss.
 
Kama anaweza amalize uji chupa ya vikombe vitano Kwa siku . Ambao unapilipili manga. Huku misosi ya supu isimchezee mbali
 
Tafuta maziwa ya unga ya watoto mfano ABC, lactogen lakini yawe gold. Asiache kunuonya maziwa ya mama pia.
huu ni ushauri wa pili napewa ila sina uzoefu na haya maziwa ya watoto samahani nitajuaje kuwa ni gold na haya maziwa hata supermakt yanapatikana? Pia kwenye kipimo cha kumpa au ni kumpa tu anyonye mpaka anaacha mwenyewe?
 
huu ni ushauri wa pili napewa ila sina uzoefu na haya maziwa ya watoto samahani nitajuaje kuwa ni gold na haya maziwa hata supermakt yanapatikana? Pia kwenye kipimo cha kumpa au ni kumpa tu anyonye mpaka anaacha mwenyewe?
Origin:AustraliaBrand:ABC Infant Formula GOLD
ABC Infant Formula GOLD AA + DHA

PRODUCT DESCRIPTION
A specifically developed blend of whey dominant milk Proteins, healthy fats, easily digested
carbohydrates and appropriate micronutrients (including minerals, vitamins, nucleotides and
immune system supportive additives) designed for an infant formula (from birth).
INGREDIENTS
Milk Solids (Demineralised Whey, Full Cream Milk, Whey protein Concentrate, Skim Milk), Vegetable
Oil, Lactose, Galacto-oligosaccharide (GOS), glucose syrup solids, Fructo-oligosaccharides (FOS),
tuna Oil, Maltodextrin, Lifes AA, Lecithin, Taurine, Choline.
Minerals: Potassium, Calcium, Sodium, Iron, Magnesium, Zinc, Copper, Iodine, Manganese,
Selenium.
Vitamins: Vitamins (A. B1, B3, B6, B12, C, D, E, K1), Pantothenic acid, Beta-Carotene, Folic acid,
Biotin.
Nucleotides: Cytidine-5 monophosphate, Uridine-5 monophosphate, Adenosine-5
monophosphate, Guanosine-5 monophosphate.
APPLICATIONS
Infant Formula 0 6 months.
PHYSICAL ASPECTS
Appearance creamy white to cream colour, free flowing
Flavour & Odour No off flavour or taste. Clean sweet creamy taste
PACKAGING
Multiwall Kraft paper bag with poly-inner liner (heat sealed & nitrogen gas flashed) of 25 kg net
weight.
TRANSPORT
20 ft. container = 16MT. Floor loaded.
40 ft. container = 24MT. Packed on I.P.P.C heat treated pallets and shrink wrapped.
STORAGE, HANDLING & SHELF-LIFE
Typical shelf-life is 12 months in the original unopened packing when kept under optimal storage
conditions (cool, dry and odour free - temperature <25 ºC., relative humidity below 65 %).
Packages should be kept in a dry ventilated facility and should not be placed in direct sunlight or in
direct contact with floors and walls.

Brand Name: ABC Infant Formula GOLDPlace of Ori
 
Habari zenu wana jf?

Ni mwezi sasa toka mama watoto wangu ajifungue lakini toka alivyojifungua alikuwa na tatizo la maziwa kuwa machache. Na tukafanya kila mbinu ili mziwa yaongezeke ikiwa ni pamoja na kumuwekea ratiba ya kunywa supu ya makongoro, kula ugali wa dona pamoja na kumtengenezea uji wa lishe bila kusahau pilipili manga kwenye uji na supu kwa sana.

Baada ya kufanya hivyo kidgo maziwa yalianza kutoka lakini sio katika kiwango kinachoridhisha, kwani mwanangu ana mwezi na wiki zake lakini afya yake kama ana wiki 2, Naombeni ushauri kwa wale wazoefu pamoja na ma dr wa hapa kama naweza nikamuanzishia mwanangu chakula mbadala kwa umri wake huo wa mwezi moja, au labda kama kuna namna nyingine ya kumfanya mama ake apate maziwa mengi na yakutosha.

Kwani kwa ma dr niliowaona wananiambia akazanie tu pilipili manga wakati mwanangu ukuaji wake ni wa kusuasua. Naomba kuwasilisha.
Hujasema hiyo pilipli Manga anatia kwenye nini na kuila? Fuata utaratibu huu hapa chini Maziwa yatatoka kwa kwa mke wako anaye nyonyesha mtoto wake.

VITU VINAVYOONGEZA MAZIWA KWA MAMA ANAYE NYONYESHA​

1605893747625.png


~Kuna baadhi ya akina mama wanapotoka kujifungua
katika kipindi kile muhimu cha kunyonyesha huwa
maziwa yanakuwa kidogo sana kiasi cha kutomtosheleza
mtoto


~tatizo hili ni baya kwa sababu mtoto anapozaliwa
anahitaji sana kupata maziwa ya mama ya kutosha kwa
muda usiopungua miezi 6


~maziwa ya mama yana lishe zote zinazohitajika kwa
mtoto na kama mtoto huyu atapata maziwa ya kutosha
basi bila shaka atakuwa ni mwenye afya njema na
watoto wanaopata maziwa kidogo afya zao huwa si
njema sana.


JINSI YA KUONDOA TATIZO HILI

~Kuna njia nyingi za asili katika kuondoa hili tatizo,lakini
kwa leo ntazungumzia njia chache tuu ambazo ni
muhimu zaidi na ndizo zinazojaza haraka maziwa kifuani
kwa mama mwenye mtoto mchanga


SUPU YA NG'OMBE,MBUZI NA KONDOO



1605893780764.png




~Mwanamama anapotoka kujifungua ni vizuri apate supu
kila asubuhi na ni vizuri zaidi akapata supu ya
kongoro,nyama ya ngombe au supu ya kondoo kwani
supu za namna hii ni tiba nzuri kwa mama mwenye
matatizo ya kutopata maziwa ya kutosha kwa ajili ya
mtoto wake na pia hurejesha nguvu zilizopotea wakati
wa mshikemshike wa kujifungua
.


NDIZI ZA KUCHEMSHA


1605893797421.png




~Pia ndizi za kuchemsha ni nzuri sana kwa kuondoa hili
tatizo la kukosa maziwa kwa mama
mjamzito,zichemshwe vya kutosha mpaka ziwe laini na
hata mtori pia unafaa katika kutibu hali hyo


MAJI



1605893811714.png




~Mzazi anapaswa awe ni mwenye kujitahidi kunywa maji
ya kutosha kila siku kwani nayo humsaidia kuongeza
maziwa kwa ajili ya mwanae mpya,pia mzazi kukandwa
maji ya moto sehemu za siri si chini ya wiki moja ni
vizuri zaidi kwani humsaidia kupata nguvu na kuufanya
uke hurudi katika hali ya kawaida kwa muda mfupi.


UJI WA MTAMA AU UWELE WENYE UNGA WA PILIPILI Manga (Mtama)



1605893827816.png



~Aidha mzazi anashauriuwa anywe uji wa Mtama au uwele wenye pilipili
manga (Mtama) na sio pilipili hizi za chachandu,kwani pilipili
Manga(mtama) zina faida mbili kwa mzazi

1.huondoa haraka makovu yaliyotokana na msuguano
wa mtoto tumboni

2.husaidia ongezeko la maziwa ya mama ili yapatikane
ya kutosha kuweza kumnyonyesha mwanae na akapata
afya njema. chanzo Herbalist Doctor MziziMkavu.
 
Dah mwanangu now tabidi ujipigilie tu maziwa ya ng'ombe maana hakuna namna.
 
Pole sana mkuu nimesoma mpaka nimejisikia vibaya sana. Maziwa ya ng'ombe sio mazuri kabisa kwa mtoto chini ya mwaka mmoja. Natamani ningeweza kukusaidia ila sina uwezo.

Mama amejaribu kutumia mbegu za maboga pia imeshindikana?? Lakini wataalamu wanasema hata kama maziwa yanatoka kidogo amnyonyeshe hvyo hvyo mara kwa mara maana navyonyonya ndio yanazidi kujitengeneza.

Kungekuwa na uwezekano wa mama kunyonyeshea mtoto mwingine ningekusaidia mkuu nimeumia sana sababu binti yangu amefunga miaka 2.2 ndio ameacha kunyonya ninahangaika na maziwa kujaa kupitiliza.
 
Anywe maji yenye unga/mbegu uwatu
Kama mnywaji anywe pombe sisi wachaga Hufanya hivyo kupata maziwa
 
Hakikisha mama anakula vizuri ikiwemo matunda na kunywa maji mengi, uji wa pili-pili manga na maziwa.
Habari zenu wana jf?

Ni mwezi sasa toka mama watoto wangu ajifungue lakini toka alivyojifungua alikuwa na tatizo la maziwa kuwa machache. Na tukafanya kila mbinu ili mziwa yaongezeke ikiwa ni pamoja na kumuwekea ratiba ya kunywa supu ya makongoro, kula ugali wa dona pamoja na kumtengenezea uji wa lishe bila kusahau pilipili manga kwenye uji na supu kwa sana.

Baada ya kufanya hivyo kidgo maziwa yalianza kutoka lakini sio katika kiwango kinachoridhisha, kwani mwanangu ana mwezi na wiki zake lakini afya yake kama ana wiki 2, Naombeni ushauri kwa wale wazoefu pamoja na ma dr wa hapa kama naweza nikamuanzishia mwanangu chakula mbadala kwa umri wake huo wa mwezi moja, au labda kama kuna namna nyingine ya kumfanya mama ake apate maziwa mengi na yakutosha.

Kwani kwa ma dr niliowaona wananiambia akazanie tu pilipili manga wakati mwanangu ukuaji wake ni wa kusuasua. Naomba kuwasilisha.

Updates.
Wana jf poleni na majukumu yenu ya kila siku.
Nimerudi tena kuleta mrejesho kuhusu andiko langu hapo juu, kwani nilijaribu kutumia mbinu na njia nilizoelekezwa na wadau, lakini naweza kusema kuwa njia moja tu ndio niliweza njia yenyewe ni kumpa mwanangu maziwa ya kopo.
Kulingana na mzingira ninayoishi maziwa yanayopatikana kwa urahisi ni lactogen na infacare hivyo nilimchukulia ya lactogen.
Lakini kwa masikitiko makubwa nasikitika na namwonea mwanangu huruma, kwani SITOWEZA TENA KUMUDU GHARAMA ZA MAZIWA YA KOPO. NA NATEGEMEA KUMUANZISHIA MAZIWA YA NG'OMBE NA KUMKOROGEA UJI MWEPESI (n.b mwanangu ana miezi 2).
Kwanini nimefikia hatua hii? Kusema ukweli najiskia vibaya sana ila kwa hali yangu kiuchumi imebidi nichukua maamuzi haya, kwani maziwa ya kopo ni tsh elf 25 na mwanangu anatumia ndani ya siku 2 siku ya 3 amemaliza kopo moja na hapo na maziwa ya mama pia ananyonya japo sio mengi na kijana mwenzenu sina ajira rasmi napambana tu mtaani kwa kweli hali ni mbaya, na mzunguko wa biashara umekuwa mdogo sana. Mwanangu nakupenda sana ila sina budi kukulisha uji kwa umri wako huo.
Pia nilijaribu kuwashauri baadhi ya wataalam wakaniambia maziwa sio mazuri kwa umri huo lakn nitafanyaje? Nimuache mwanangu akonde? Au alie usiku kucha kwa kutoshiba? Dah Japo nimeambiwa mwanangu hutokuwa na akili kwa aina ya vyakula unavyokula kwenye uchanga wako ila naamini Mungu atakusimamia tu na utakuwa na akili tu.
 
Anywe maji yenye unga/mbegu uwatu
Kama mnywaji anywe pombe sisi wachaga Hufanya hivyo kupata maziwa
mkuu we acha tu uji wa lishe nilisaga na nikaweka mazaga yote na kila akinywa uji lazima atie pilipili manga kwa sana.
Ila matokeo yake wife ndio ananenepa mtoto anakonda na kinachoniumiza zaidi na maneno ya majirani kwa wife kwamba "wewe unanenepa mtoto anakonda au mumembemenda mtoto" dah hakika hili nalo litapita.
 
Wakuu yaani kusema ukweli nimejaribu sana kila njia kwani kama ni matunda wife anakula sana na mazingira ninayokaa upatikanaji wa matunda ni rahisi sana, kama hyo haitoshi nimempeleka wife kwa masheikh na wachungaji kufuatia ushauti wa watu kuwa aidha katupiwa jini mnyonya maziwa lkn wapi.
 
Nimekuonea huruma sana mzee, nakumbuka mjomba wangu flani hv alikuwa ananunua maziwa ya unga (kopo) kwa sh. 85000 na hayamalizi wiki yanakuw yameisha (sijajua kama mke wake alikuwa na upungufu wa maziwa)

Ushauri wangu kwako ni afadhali uendelee kumkazania mkeo kumnyonyesha mtoto mara kwa mara ht kama ni machache kuliko kumpa mtoto maziwa ya unga/ng'ombe .
 
Wakuu yaani kusema ukweli nimejaribu sana kila njia kwani kama ni matunda wife anakula sana na mazingira ninayokaa upatikanaji wa matunda ni rahisi sana, kama hyo haitoshi nimempeleka wife kwa masheikh na wachungaji kufuatia ushauti wa watu kuwa aidha katupiwa jini mnyonya maziwa lkn wapi.
Mtoto anyonye hvy hvy hata kama ni machache
 
Mtoto anyonye hvy hvy hata kama ni machache
sawa mkuu namkazia lakini huyu mtoto sijui ndio niseme kwamba ana njaa kubwa yaani akiwa ananyonya mwanzoni kidogo anapata maziwa na kutulia ila yakianza kukata hakukaliki ndani ni kilio haswa.
 
Mchemshie mama tangawizi ya nguvu anywe itamsaidia
 
Mchemshie mama tangawizi ya nguvu anywe itamsaidia
mama nshamfanyia vitu vingi sana mzee labda ngja nijaribu na hili la tangawizi tuone
 
Mbegu za maboga ni uhakika, mpe mkeo atafune na apikie, utaleta mrejesho chanya humu mkuu...
 
Back
Top Bottom