Pole sana. Mwanangu ana miaka mitatu na miezi nne sasa. Naye ana tatizo kama hilo la kukosa usingizi. Ilitusumbua kiasi. Jambo moja nililogundua ni kuwa hapati michezo mingi ya kumfanya achoke. Niligundua hivyo kwasababu ilikua tukienda kijijini ambapo anahangaika kutwa nzima (kuchunga, kulima, kuchota maji, kukimbiza kuku, na kila aina ya mchezo) basi atalala mchana na usiku mapema tu analala. Sasa huku mjini anachezea sebuleni tu, atachokaje? atapataje usingizi?
Nawashauri muongezeeni michezo (vifaa vya kuchezea na kumweka busy zaidi. Ale kwa ratiba inayoeleweka na kwa kiasi fulani ratiba ya kulala iwepo na izingatiwe sana. Pia mkamuone mtaalamu wa watoto atawashauri vyema zaidi.