Msaada: Nahitaji kufika Mwanza saa 7 mchana kesho na ndege zimejaa, kuna option nyingine yoyote?

theprogrammer C++

Senior Member
Joined
May 17, 2013
Posts
106
Reaction score
226
Wakuu nimekuja kwenu Kwa msaada, kama Kuna njia nyengine ya kufika Mwanza kabla ya saa 6 kesho mchana nisaidieni. Nina shughuli muhimu na ninahitajika niwepo muda huo.

Kama Kuna msaada wa option nyingine hata private car niko tayari pia kwenda pamoja na kuchangia chochote.

Asanteni.
 
Ndege za Kigoma mpaka Mwanza zipo mbona, jioni sa 10 leo
 
Unaenda kufanyaje kwanza
 
Sasa hata hujasema, wewe uko wapi.
Anyway huwa kuna flights za Air Tanzania asubuhi saa 12 na saa 3 kama unatokea dar es salaam
 
Kuna basi 24 hrs , sa mbili usku unaamsha DSM , sa 4 asubh upo mwanza , Ila kiukweli ifikie hatua serikali iruhusu mashirika shindani ya ndege , Kwa mwanza abiria ni wengi mno wa ndege , Yani ndani ya masaa 24 hupati tiketi asa ndo nini
 
Chukua IT zinazoenda Rwanda,Burundi na Congo zinakuacha Tinde,zinapatikana sheli ya ya Oil com pale njia panda ya Keko,Jengo la Water front pale bandarini ndipo zinapotoka au misugusugu mizani yao ilipo njia ya Mlandizi na Ubungo pia unaweza zitega Kila la kheri.
 
Upo wapi Kwa sasa!l?
 

We jamaa wewe!
Tumewaza kitu kimoja, tofauti tu ni kwamba wewe umetoka maelekezo Rafiki zaidi kueleweka.

Akipata IT mapema atafika huo muda anaoutaka.
 
Nenda pale ubungo kibo panda IT za mwanza kesho saa 12 asubuhi upo jijini.
 
Fursa kwa wafanyabiashara kuingia kwenye soko la usafiri wa anga kama ndege zinajaa lakini mabasi hayajai
 
Nenda ubungo katege special hire
Nenda karikaoo lori nyingi za mizigo zipo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…