Msaada: Nataka kuanzisha magazine

Msaada: Nataka kuanzisha magazine

Wana JF, Namwomba aliye na ufahamu,utayari anisaidie katika hatua zote zinazohitajika kuanzisha Magazine ya kila mwezi.Tatizo langu ni sifahamu hatua hizo. Tuwasiliane..0765410726.

Upo wapi.. tuwasiliane.. mimi pia nina hizo interest
 
Magazine ni jarida, gazeti ni newspaper. Kuna tofauti kati ya magazine na gazeti, but anyway nenda ofisi za IDARA YA HABARI MAELEZO utapewa utaratibu kamili. Gharama ya kusajili gazeti au magazine ni shilingi LAKI TANO.

UTARATIBU KAMILI UPO HIVI :

1. Unaandika barua ya maombi ya usajili wa gazeti/jarida kwa MSAJILI, IDARA YA HABARI MAELEZO.
2. Viambatanisho ;
i. Jina la biashara ( Sole Proprietorship ) au jina la kampuni kama una miliki kampunu, pamoja na certificate ya usajili wa jina la biashara au kampuni kutoka BRELA.

iii. Utapendekeza majina kuanzia matatu ambayo utapenda gazeti/jarida lako liitwe

iv. Taarifa za akaunti yako ya benki zinazo onyesha kuwa una uwezo wa kutoa mfululizo wa matoleo kumi ya gazeti lako bila kutegemea chanzo kingine cha mapato .

N.B: Kuhusu taarifa za akaunti usiogope sana, unaweza kueleza kuwa utakuwa unatoa labda nakala mia kwa wiki some thing which means that akaunti yako inaweza ikawa hata na sh laki mbili na bado ukawa na uwezo wa kusajili gazeti lako.. Hope maelezo yangu yatakuwa na msaada kwako. God Bless U
Ahsante Mkuu, Mungu akubariki

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom