Msaada: Nawezaje kuchunguzwa kansa na magonjwa ya figo?

Msaada: Nawezaje kuchunguzwa kansa na magonjwa ya figo?

ndege JOHN

JF-Expert Member
Joined
Aug 5, 2015
Posts
21,643
Reaction score
51,642
Kwa mfano Kama Nilikuwa mlevi sana wa pombe kali na mvuta sigara kwa zaidi ya miaka 20 Sasa nikataka kujua hali yangu ya organ za ndani zipoje; yaani nijue kama kuna dalili za kansa ya mapafu,ini na Koo na pia nifanye kipimo Cha magonjwa ya Figo.

Je, hiyo check-up ya mwili hufanywa kwa vipimo gani mashine ipi na je hospital za hadhi gani?

Nina Bima ya afya NHIF so nielekezwe nafanyaje au namwombaje daktari ili akubali kunipima hata kama siumwi dalili zozote?
 
Ajabu hayo magonjwa huwapata hata sio walevi wala wavuta sigara!!

Kuna msela wangu ni mlevi wa kufa mtu!

Mvuta bangi na pariki lakini amepimwa yupo INTACT.
 
Ajabu hayo magonjwa huwapata hata sio walevi wala wavuta sigara!!

Kuna msela wangu ni mlevi wa kufa mtu!
Mvuta bangi na pariki lakini amepimwa yupo INTACT.
Hata Kuna ndugu yangu alifariki kwa homa ya ini kapimwa muhimbili kaambiwa limeshaliwa ini Ni Kama cancer hakuchukua Mwezi akafa
 
Kwa check up ya afya, unakwenda kwa daktari na kumwambia kama ulivyoandika. Bima ya afya inafanya Vipimo vingi Hapo. Vichache kama hepatitis B unaweza kulipia.

Cha msingi wewe nenda kwenye hospital level ya mkoa, sema shida yako vipimo utafanyiwa. Kama havilipiwi na kadi ya Bima, unaachia cash mambo yanakwenda!
 
Kwa mfano Kama Nilikuwa mlevi sana wa pombe kali na mvuta sigara kwa zaidi ya miaka 20 Sasa nikataka kujua Hali yangu ya organ za ndani zipoje yaani nijue Kama Kuna dalili za kansa ya mapafu,ini na Koo na pia nifanye kipimo Cha magonjwa ya Figo..je hio check up ya mwili hufanywa kwa vipimo gani mashine ipi na je hospital za hadhi gani?Nina Bima ya afya NHIF so nielekezwe nafanyaje au namwombaje daktari ili akubali kunipima hata Kama siumwi dalili zozote?
Kama huna dalili zozote hawawezi kukupima,ila kansa hupimwa kwa kukatwa sehemu ya nyama kwenye eneo lenye kidonda na hicho kinyama kinaitwa biopsy,kinapelekwa kwenye idara ya histopathology ili kupimwa kansa
 
Nimeshawahi kuzini na baba yako au na wewe?
288034818_091547.jpg
 
Nikupe hongera kwa kujua kuwa afya ni mtaji sawa na gari ambyo ucpoipatia services hutapatata hesabu nzuri. Kama una bima utaenda kwa dr ila inabidi dr akutengenezee ugonjwa maana nhif hawana packege ya check up wao hutoa packege ya wagonjwa tu. Kwa upande wa saratan zpo njia nyingi za uchunguzi. Anaekatwa kinyama ni mtu ambaye labda kuna uvmbe mahali au kidonda cha muda mrefu hukatwa na kupelekwa maabara ili kuangalia je? Seli zlzopo hiyo sehemu zimebadilka tabia zkawa za saratani?. Upande wa magonjwa ya fgo vpmo vya maabara au vya radiolojia kuangalia ufanyaji kaz wake. Literature zinasema sio kwamba kila mtu anaweza kuugua saratan au ugonjwa wwte. Kinga ya kila mtu ndio jambo pekee linalomuepusha na magonjwa. Ila kuna mazngra ambayo mtu unaweza kupitia ambyo yanamfanya au yanafanya kinga kuwa chini.
 
Kwa mfano Kama Nilikuwa mlevi sana wa pombe kali na mvuta sigara kwa zaidi ya miaka 20 Sasa nikataka kujua hali yangu ya organ za ndani zipoje; yaani nijue kama kuna dalili za kansa ya mapafu,ini na Koo na pia nifanye kipimo Cha magonjwa ya Figo.

Je, hiyo check-up ya mwili hufanywa kwa vipimo gani mashine ipi na je hospital za hadhi gani?

Nina Bima ya afya NHIF so nielekezwe nafanyaje au namwombaje daktari ili akubali kunipima hata kama siumwi dalili zozote?

Vipimo vya kansa mwilini vyaweza kufanyika kwa kutegemea na athari ya kansa husika kwenye mwili. Mfano: kuongezeka kwa uvimbe/size huweza kuleta maumivu ambayo huweza kuwa dalili inayomleta mgonjwa hospitali. mfano: kansa ya ziwa, kuongezeka kwa vichocheo/hormone mfano: bhcg kwenye ujauzito ulioshindwa kuendelea kukua kwa makosa ya ki-jenetiki, PSA kwenye kansa kwenye tezi dume.

Hivyo unaweza kuanza kupima kulingana na chanzo na dalili:

1: Uvimbe (Xray/CT scan, Echomammography na MRI)

2: Vidonda na uvimbe (biopy)

3: Matezi (kupima kemikali husika/ ultrasound/biopsy)

4: Kemikali zinazopatikana mwilini kutokana na uwepo wa aina fulani ya kansa (tumor markers).

5: Kuchukua ulojo kwenye maeneo kama kakikati ya mifupa.

6: Nuclear medicine: sifa za uwezo wa kuchukua baadhi ya madini mwilini.

7: Multi-cancer DNA screening test/artificial intelligence. From blood biopsy

8: Kucheki figo, hii haina shida sana maana ni vipimo kama viatu kulingana na hali yako(Creatinine, Urea na Ultrasound). Labda kama kutakuwa na shida yoyote.


Kila kipimo hapo kina umuhimu kulingana na asili ya tatizo/kansa na ni kwa kiasi gani tatizo lilivyo.

Hivyo, upime nini kwenye check up hutegemea ni nini unataka kutokana na nini kufikia kama mwafaka. Mfano: kulingana na asili ya kazi, umri, jinsia na historia nyingine vyaweza kuwa na nafasi ya mtoa huduma aseme afanye nini kama vipimo baseline na non invasive/visivyo na madhira makubwa kwako kulingana na umuhimu.

NB: Kama ulivyoelezwa kuwa bima hazilipii check up. Inabidi kujua jinsi ya kucheza huu mdundo.
 
Back
Top Bottom