Msaada: Nawezaje kuziba matundu kwenye bati zilizowahi kutumika ili niezekee kwenye nyumba nyingine?

Msaada: Nawezaje kuziba matundu kwenye bati zilizowahi kutumika ili niezekee kwenye nyumba nyingine?

Tumia tina
Hivi unajua matumizi ya Tina (Thinner)...???..bora hata ungesema Aladite ningesema una idea kidogo ...waliosema silicon wako sahihi pia...sema silicon mi naona ni maalumu sana kwa vitu vya plastic...ningekuwa mimi ningetumia aladite.
 
Nenda duka lolote la vifaa vya ujenzi watakupa gundi fulani hivi ipo kawa dawa ya meno ila ni nyeusi,utaiweka kwenye matundu ya bati lako,pia hii hutumika kubandikia vioo kwenye madirisha,nimesahau jina kwa sababu mara ya mwisho niliiona mwaka 2007
Silicone, sikaflex etc.
 
Mkuu njia rahisi na nafuu ni kutumia kipimo kilekile yaani unapiga Mbao kulingana na matundu ya bati unarudishia misumali mlemle.

Pili wakati unapinga bati hakikisha migongo ya matundu inakuwa juu. ukiwa chini utaona matundu ila maji hayataingia labda mvua iwe kubwa na hiyo ikilenga direct kwenye hayo matundu.
Tatu ngundi nzuri ni maroo. Huwa nyeusi kama rami hivi inauzwa elfu tatu nusu kilo.
 
Mkuu njia rahisi na nafuu ni kutumia kipimo kilekile yaani unapiga Mbao kulingana na matundu ya bati unarudishia misumali mlemle.

Pili wakati unapinga bati hakikisha migongo ya matundu inakuwa juu. ukiwa chini utaona matundu ila maji hayataingia labda mvua iwe kubwa na hiyo ikilenga direct kwenye hayo matundu.
Tatu ngundi nzuri ni maroo. Huwa nyeusi kama rami hivi inauzwa elfu tatu nusu kilo.

Maroo sio nzuri mkuu,,, nimeitumia sana, Maroo ni nyeusi kama lami, ukiiweka kwenye bati baada ya muda ikipigwa na jua Kali inayeyuka, au nyingine baada ya kuganda inapasuka pasuka kama lami,

Labda hao waliosema silicon sealant au Aladite! maana sijawahi kujaribu hizi.

Maroo sio nzuri mkuu,,,
 
Mkuu njia rahisi na nafuu ni kutumia kipimo kilekile yaani unapiga Mbao kulingana na matundu ya bati unarudishia misumali mlemle.

Pili wakati unapinga bati hakikisha migongo ya matundu inakuwa juu. ukiwa chini utaona matundu ila maji hayataingia labda mvua iwe kubwa na hiyo ikilenga direct kwenye hayo matundu.
Tatu ngundi nzuri ni maroo. Huwa nyeusi kama rami hivi inauzwa elfu tatu nusu kilo.
Nami akili yangu ilikuwa humo humo kwenye Maroo. Ndo suluhisho kuu ya bati lenye matundu.
 
Gundi kwa ajiri ya Bati Zipo aina nyingi ikitofautiana matumizi!

Kama ni Matundu ya Bati yaliyotokana na Misumari, kwa kawaida Msumari hugongwa kwenye Mgongo, hivyo kama Matundu yakiwa juu ya Mgongo ni ngumu Bati kuvuja... But ikibidi ndo unaweza kutumia Gundi!

Gundi ya Moto ni Bora kuliko Silicone inapokuja kuziba Matundu, Ila Gundi ya Moto na Silicone ni Bora zaidi Kama Bati linavuja pale Msumari ulipopigwa, Binafsi napendekeza Gundi ya Moto kwa sababu kadri inavyoanza kukauka Huwa inavimba hivyo kujaa kwenye Tundu!

Kama ni kuziba Tundu ambalo lipo wazi, Tumia Gundi ya Rami kwa ajiri ya Mabati, hii unaziba Matundu yaliyowazi kwa usahihi, na Kama Tundu ni kubwa unaweza kuchomeka Pamba kidogo then kwa juu ukasiriba na Gundi hiyo.

Bei ya Gundi zote ni kati ya 5,000 mpaka 10,000, haizidi 10,000.
 
Habari zenu wana jf,kutokana na bomoabomoa zinazoendelea kupisha ujenzi wa barabara nimejikuta naambulia bati na vitu vingine kama milango na madirisha.

Ninawaza kutumia bati zilezile pamoja na baadhi ya mbao,ili niezekee nyumba mpya kupunguza gharama za ujenzi ,bati ni za geji 28

Ni kwa namna gani naweza kuzuia bati hizo kuvuja wakati wa mvua?
Mkuu nenda hardware yyte ulizia silicone itakufaa
 
Nenda duka lolote la vifaa vya ujenzi watakupa gundi fulani hivi ipo kawa dawa ya meno ila ni nyeusi,utaiweka kwenye matundu ya bati lako,pia hii hutumika kubandikia vioo kwenye madirisha,nimesahau jina kwa sababu mara ya mwisho niliiona mwaka 2007
Silicone thn inapatikana kwa rangi tofaut kuna white,black na ile transparent
 
Habari zenu wana jf,kutokana na bomoabomoa zinazoendelea kupisha ujenzi wa barabara nimejikuta naambulia bati na vitu vingine kama milango na madirisha.

Ninawaza kutumia bati zilezile pamoja na baadhi ya mbao,ili niezekee nyumba mpya kupunguza gharama za ujenzi ,bati ni za geji 28

Ni kwa namna gani naweza kuzuia bati hizo kuvuja wakati wa mvua?
Mtafute huyu fundi yupo vizuri sana kwenye kuziba bati: Fundi wa Kuziba Bati linalovuja kwa Silicone
 
Back
Top Bottom