Msaada ni sababu zipi zinafanya mimba kutunga nje ya mfuko wa uzazi?

Van Pauser

JF-Expert Member
Joined
Mar 21, 2017
Posts
417
Reaction score
420
Habari za asubuhi wapendwa natumaini ni Jumatatu nyingine tena ambapo kila mmoja anajiandaa kwenda katika majukumu ya ujenzi wa taifa niende moja kwa moja kwenye mada husika hapo juu.

Je kwa wataalamu wa masuala ya uzazi ni zipi sababu zinazofanya mimba kutunga nje ya mfuko wa uzazi..??

Je ikiwa mimba imetunga nje ya mfuko wa uzazi ni madhara yapi anayapata mwanamke..??

Je kuna uwezekano asilimia ngapi mtoto aliyeko tumboni kuweza ku_survive..???

Nawasilisha....
 
Mimba kutungwa nje ya mfuko wa uzazi hutokea pale yai lililorutubishwa kushindwa kujishikiza katika mji wa mimba(uterus) na kujishikiza katika mirija ya uzazi au sehemu nyingine ya tumbo.

Sababu zipo nyingi hizi ni baadhi kama magonjwa ya zinaa, maambukizi katika via vya uzazi (PID), uwepo wa kovu kama alishawai kufanyiwa upasuaji, matumizi ya dawa za uzazi n.k
Mwanamke anapokua na tatizo hilo hupata maumivu makali ya tumbo, kizunguzungu, kutapika na hutokwa na damu nyingi ukeni.

Mimba ikitungwa nje ya mji wake mtoto hawezi kusurvive mara nyingi mwanamke akikutwa na tatizo hilo hutibiwa kwa kupewa dawa au kufanyiwa upasuaji.
 
Asante sana kwa majibu yako mazuri..!!
 
Mimba inatungwa kwenye mirija ya fallopian badae yai inabidi lishuke mpk kwenye mji wa uzazi sasa ikishindwa kumove ndo linakulia hapo hapo. Mkiwahi kuna dawa za kunyausha huo utungo nabadae vitu km damu na uchafu mwingine unatoka kupitia papuchi. Wakat huo unapewa na dawa za kusafisha za antibiotics km Amoxlin na flagile. Mkichelewa upasuaji lazima
 
Asante mkuu kwa majibu yako mazuri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…